UCHUNGUZI WA KINA WA MAMBO MBALI MBALI YA KIROHO KATIKA BIBIBLIA NA ROHO YA UNABII.
JE UMEMPENDA AU UMEMTAMANI
Na Petro tumaini
Na Petro tumaini
![]() |
| Tofauti kati ya upendo na tamaa ni dhahiri, zingatia haya ili ujenge mahusiano yenye afya. |
Kati ya changamoto zitukumbazo vijana ni kukurupuka katika mahusiano bila kuelewa ni nini tunafanya. Kwa upande wa wanandoa changamoto nyingi huwapata kwasababu wameingia katika mahusiano na watu waliodhani wanawapenda kumbe wamewatamani.
Kati ya mambo yasumbuayo katika mahusiano ni watu kudhani upendo ni ngono , lakini ukweli ni kwamba ngono ni sehemu ndogo sana ihusikayo katika upendo kwa wanandoa. Wengi wamevunja ndoa zao kwasababu wameingia katika mahusiano wakidhani kuwa ngono ni kila kitu kumbe kuna majukumu makubwa katika ndoa kuliko ngono.
UPENDO HUUNDWA NA PANDE KUU TATU
Kwa mujibu wa mwanasaikolojia Robert Stenberg, ili watu wafikie katika mahusiano sahihi ya ndoa ni lazima wapitie hatua tatu
![]() |
| Upendo sahihi katika mahusiano huanza na Mawasiliano (Intimacy), maamuzi ya kufunga ndoa ( |
- Intimacy , hii ni sehemu ya mahusiano iundwayo na ukaribu wa kimawasiliano. Kubadilishana mawazo , kufanya kazi pamoja , kufahamiana ,kusaidiana katika shida na raha .
- Commitment , ni sehemu ya pili ya upendo inayohusiana na kuweka mkataba wa makubaliano ya kuwa wachumba mtakaooana na kufikia hatua ya kula kiapo (comitment) ya kuishi pamoja hata mauti itakapowatenga.
- Passion , ni sehemu ya tatu ya upendo ambayo huundwa na mahusiano ya kimwili ambayo ambayo kilele chake huwa ni tendo la ndoa.
Kumekuwa na kampeni ambazo ni kinyume cha maandiko matakatifu , ikiwamo ''Kampeni ya kucheza ngono salama" , Kibliblia hakuna ngono salama , aziniye baada ya kuthibitisha afya yake na mwenzi wake au kwa kutumia mpira Biblia humuhesabu kama mzinzi / mwasherati.
KANUNI ZA BIBLIA KUHUSU NGONO KABLA YA NDOA
1 Wakorintho 6:18 Ikimbieni zinaa. Kila dhambi aitendayo mwanadamu ni nje ya mwili wake; ila yeye afanyaye zinaa hutenda dhambi juu ya mwili wake mwenyewe.
2 Timotheo
2:22 Lakini
zikimbie
tamaa
za
ujanani;
ukafuate
haki,
na
imani,
na
upendo,
na
amani,
pamoja
na
wale wamwitao
Bwana kwa
moyo
safi.
Kumbukumbu la Torati 5:18 Wala usizini
INFATUATION(KUGHURIKA)
Jambo lipaswalo kufanywa wakati wa uchumba ni , mawasiliano (intimacy) , ya ukaribu kufahamiana na kusaidiana katika mambo ya kawaida (si matakwa ya ashiki za ngono).
Jambo la Pili katika mahusiano ya uchumba ni kufanya makubaliano ya kuoana na kufunga ndoa (commitment).
Baada ya kupitia hayo mawili ( 1-Intimacy, 2- commitment ) ndipo wanandoa hufaidi mbaraka wa tendo la ndoa (Passion). Wachumba waingiao katika maghusiano bila kupitia hatua hizo tatu hutafuta laana katika ndoa yao watakayo funga.
HATUA ZA UCHUMBA MPAKANDOA YENYE MBARAKA
- Intimacy
- Commitment.
- Passion.
- Intimacy
- Passion
- Commitment
AU
- Passion
- Intimacy
- Commitmet
SOMO HILI LIMEANDALIWA NA PETRO TUMAINI
Email -petro.tumaini@gmail.com
Mtu mmoja aliye na Yesu ni Yote, Kitu cha pekee kuwa na Shauku kwacho ni
uhakika wa Kuwa na Yesu siku zote, kitu cha pekee kuwa na hofu kwacho ni
kutengwa na upendo wa Yesu.
Hakuna jambo
tulitafutalo katika dunia hii ambalo Yesu hawezi kulitimiza. Mtu akimpata Yesu,
amepata yote katika dunia hii na Zaidi Uzima wa milele .
Mathayo 19:29 Na kila mtu aliyeacha nyumba, au ndugu wa kiume au wa kike, au baba, au
mama, au watoto, au mashamba, kwa ajili ya jina langu, atapokea mara mia, na
kuurithi uzima wa milele.
Ukweli
ni kwamba , kama huna Yesu, hata usome elimu yote ya dunia , ufanye kazi kuliko
watu wote duniani, umiliki mali na kuwekeza katika kila nchi duniani, uwe na
fedha katika kila Benki uijuayo chini ya jua, Uwe tajiri wa kwanza duniani, hayo
Yote Bila Yesu ni Bure.
Kama ni
hivyo Basi Swali la Msingi ni hili, Kama nimempata Yesu ni kitu gani chenye
mamlaka ya kunitenga na Kristo? Wapo wanaomwacha Yesu kwasababu ya mali, wapo
watengwao nae kwasababu tofautitofauti. Swali bado linabaki, Je Ni nini Kitakachotutenga na Kristo? Paulo
alijiuliza swali na kutoa majibu katika mafungu yafuatayo.
Warumi 8:35 Ni
nani atakayetutenga na upendo wa Kristo? Je! Ni dhiki au shida, au adha, au
njaa, au uchi, au hatari, au upanga?
Miongoni mwa Ahadi tamu za Biblia ni Uhakika kwamba
Aliye na Yesu ni Yote. Waati wa Matatizo wengi hutetereka na kudhani kwamba
Yesu kawaacha laini ukweli ni kwamba SHIDA NI NJIA YA KUTUPELEKA KWA YESU MAANA
YEYE NDIYE KIMBILIO LETU
2 Wakorintho 1:3,4 Na ahimidiwe Mungu, Baba wa Bwana
wetu Yesu Kristo, Baba wa rehema, Mungu wa faraja yote; 4 atufarijiye katika
dhiki zetu zote ili nasi tupate kuwafariji wale walio katika dhiki za namna
zote, kwa faraja hizo, tunazofarijiwa na Mungu.
Swali
la Msingi ni hili, Kati ya Mauti na Yesu ni lipi lenye mamlaka na uwezo kuliko
jingine, Jibu rahisi ni Yesu. Yeye aliishinda mauti, wapo ambao wakimfuata Yesu wako tayari
kumwacha ili wasipatwe na mauti ya muda mfupi lakini bbiblia inatupatia tumaini
Mathayo
5:10
10 Heri wenye kuudhiwa (kuuliwa) kwa
ajili ya haki; Maana ufalme wa mbinguni ni wao.
Ayubu
5:20
20 Wakati wa njaa atakukomboa
na mauti; Na vitani atakukomboa na nguvu za upanga.
Waebrania
11:4 Kwa
imani Habili alimtolea Mungu dhabihu iliyo bora kuliko Kaini; kwa hiyo
alishuhudiwa kuwa ana haki; Mungu akazishuhudia sadaka zake, na kwa hiyo, ijapokuwa amekufa, angali
akinena.
Yohana 11:25 Yesu akamwambia, Mimi ndimi huo ufufuo,
na uzima. Yeye aniaminiye
mimi, ajapokufa, atakuwa anaishi;
Ufunuo wa Yohana 14:13 Nikasikia sauti kutoka mbinguni
ikisema, Andika, Heri wafu wafao katika Bwana tangu sasa. Naam,
asema Roho, wapate kupumzika baada ya taabu zao; kwa kuwa matendo yao yafuatana
nao.
Yohana 8:51 Amin, amin, nawaambia, Mtu akilishika neno langu, hataona mauti milele.
Warumi 8:38 Kwa maana nimekwisha kujua hakika ya
kwamba, wala mauti,
wala uzima, wala malaika, wala wenye mamlaka, wala yaliyopo, wala
yatakayokuwapo, wala wenye uwezo, 39 wala yaliyo juu, wala yaliyo chini, wala
kiumbe kinginecho chote hakitaweza kututenga na upendo wa Mungu ulio katika
Kristo Yesu Bwana wetu.
Mungu anamamlaka juu ya hatari zote ziwezazo kutupata
katika duinia hii, Paulo alikutana na hatari karibu aina zote akiwa kwenye kazi
ya ya Mungu kama adhihirishavyo katika
waka ufuatao
2 Wakorintho 11:26 katika kusafiri mara nyingi; hatari za mito; hatari za wanyang'anyi; hatari kwa taifa langu; hatari
kwa mataifa mengine; hatari za mjini; hatari za jangwani; hatari za baharini;
hatari kwa ndugu za uongo;
Pamoja
na hatari zote Paulo alikuwa na tumaini moja na akazishinda
2 Wakorintho 12:9 Naye akaniambia, Neema yangu
yakutosha; maana uweza wangu hutimilika katika udhaifu. Basi
nitajisifia udhaifu wangu kwa furaha nyingi, ili uweza wa Kristo ukae juu yangu.
Uwe
katika shida kama Ayubu , uwe katika raha kama Sulemani, katika utajiri kama
Ibrahimu au katika umaskini , katika hali yoyote uliyonayo kumbuka wapo
walioitwa na Mungu katika hali kama Yako . JINSI ULIVYO UWAPO NA YESU HAKUNA LA KUKUTENGA NAE ,NEEMA YAKE YATOSHA .
TWAWEZA KUIAMINI BIBLIA
Baada ya kupita muda fulani mmoja tu kati ya wanaume wale wa kwanza waliofika mle kisiwani ndiye alibaki kuwa hai. Lakini mtu huyo, Alexander Smith, alikuwa ameigundua Biblia katika mojawapo la makasha yaliyochukuliwa kutoka katika ile meli. Alianza kuisoma na kuwafundisha wengine juu ya kile ilichosema. Alipofanya hivyo maisha yake yeye mwenyewe yakabadilika na hatimaye maisha ya wote waliokuwa katika kisiwa kile.
Wakazi wa kisiwa kile walikuwa wametengwa na ulimwengu wa nje mpaka ilipowasili meli ya Kimarekani iliyoitwa Topaz katika mwaka wa 1808. Wafanyakazi katika meli hiyo wakakikuta kisiwa kile kikiwa na jumuia inayokua na kusitawi, bila ya kuwa na pombe kali (wiski), gereza, wala uhalifu. Biblia ilikuwa imekigeuza kisiwa kile kutoka jehanamu ya duniani kwenda katika kielelezo cha vile Mungu atakavyo ulimwengu huu uwe. Na mpaka leo hii kinaendelea kuwa katika hali hiyo.
Je, hivi Mungu bado anaendelea kusema na watu kupitia katika kurasa hizo za Biblia? Bila shaka anafanya hivyo. Ninapoandika haya, naliangalia karatasi la majibu lililotumwa kwetu na mwanafunzi mmojawapo wa kozi zetu za Biblia. Maelezo chini yake yanasema hivi "Mimi nimo gerezani, niko katika orodha ya watu wanaostahili kunyongwa, nimehukumiwa kufa kwa kutenda kosa la jinai. Kabla ya kuchukua kozi hii ya Biblia, nilikuwa nimepotea lakini sasa ninacho kitu cha kutumainia tena nimeupata upendo mpya."
Biblia inao uwezo unaoweza kuyabadilisha kabisa maisha ya watu. Kwa kweli, watu wanapoanza kujifunza Biblia, maisha yao hubadilika kwa namna ya kuvutia sana.
1. Jinsi Mungu Anavyozungumza Nasi Kupitia Katika Biblia
Baada ya kumwumba Adamu na Hawa, yaani, yule mwanaume na mwanamke wa kwanza wa duniani, Mungu alizungumza nao uso kwa uso. Lakini Mungu alipokuja kuwatembelea baada ya wao kutenda dhambi, je, wale watu wawili walifanya nini?
"Mwanaume yule na mkewe wakasikia sauti ya BWANA Mungu alipokuwa akitembea mle bustanini wakati wa jua kupunga, nao WAKAJIFICHA ASIWAONE BWANA MUNGU katikati ya miti ya bustani." (Mwanza 3:8).
Dhambi ilikata mawasiliano ya ana kwa ana kati ya mwanadamu na Mungu. Baada ya dhambi kuingia katika ulimwengu huu, je, Mungu aliwasilianaje na watu?
"Hakika Bwana Mwenyezi hafanyi kitu, bila kuwafunulia watumishi wake manabii nia yake." - Amosi 3:7.
Mungu hakutuacha sisi gizani kuhusu maisha haya tuliyo nayo na maana yake. Kupitia kwa manabii wake - yaani, watu wale aliowaita Mungu kuwa wanenaji na waandishi wake - wamefunua majibu yake kwa maswali makuu yahusuyo maisha yetu.
2. Ni Nani Aliyeiandika Biblia?
Manabii waliutoa ujumbe wa Mungu kwa kutumia sauti na kalamu zao katika kipindi chao walichoishi, na walipokufa, maandiko yao yaliendelea kuwapo baada yao. Kisha ujumbe huo wa manabii ulikusanywa pamoja chini ya uongozi wake Mungu, na kuwekwa katika kitabu tunachokiita Biblia.
Lakini maandiko yao hayo yanaaminika kwa kiasi gani?
"Zaidi ya hayo, lakini kumbukeni kwamba hakuna mtu ye yote awezaye kufafanua mwenyewe unabii ulio katika Maandiko Matakatifu. Maana hakuna ujumbe wa kiunabii unaotokana na matakwa ya binadamu bali watu walitoa unabii wakiongozwa na Roho Mtakatifu" (2 Petro 1:20,21).
"Zaidi ya hayo, lakini kumbukeni kwamba hakuna mtu ye yote awezaye kufafanua mwenyewe unabii ulio katika Maandiko Matakatifu. Maana hakuna ujumbe wa kiunabii unaotokana na matakwa ya binadamu bali watu walitoa unabii wakiongozwa na Roho Mtakatifu" (2 Petro 1:20,21).
Katika Biblia hiyo Mungu hutuambia habari zake Mwenyewe, tena hutufunulia makusudi yake aliyo nayo kwa ajili ya wanadamu. Inaonyesha mtazamo wa Mungu kwa mambo yale yaliyopita, kisha inatufunulia mambo ya mbele, ikitueleza jinsi tatizo la uovu litakavyotatuliwa mwishoni na jinsi amani itakavyokuja katika dunia yetu.
Je, hivi Biblia yote ni ujumbe utokao kwa Mungu?
"Maandiko yote, Matakatifu yameandikwa kwa uongozi wa Mungu, na yanafaa kuonya, kusahihisha makosa yao, na kuwaongoza, katika kufundishia ukweli, mtu wa Mungu awe mkamilifu na tayari kabisa kufanya kila kazi njema, waishi maisha adilifu" - (2 Timotheo 3:16,17).
"Maandiko yote, Matakatifu yameandikwa kwa uongozi wa Mungu, na yanafaa kuonya, kusahihisha makosa yao, na kuwaongoza, katika kufundishia ukweli, mtu wa Mungu awe mkamilifu na tayari kabisa kufanya kila kazi njema, waishi maisha adilifu" - (2 Timotheo 3:16,17).
Biblia Takatifu huyabadilisha kabisa maisha ya wanadamu kwa sababu Biblia "yote" ina "pumzi ya Mungu," ni hati iliyovuviwa, ni kitabu cha Mungu. Manabii walisimulia kile walichokiona na kukisikia kwa kutumia lugha ya wanadamu, lakini ujumbe wao ulitoka moja kwa moja kwa Mungu. Kwa hiyo, ukitaka kujua maisha haya yana maana gani, soma Maandiko Matakatifu. Kuisoma Biblia kutayabadilisha kabisa maisha yako. Kadiri unavyozidi kuisoma kwa maombi, ndivyo utakavyozidi kupata amani moyoni mwako.
Roho Mtakatifu yule yule aliyewavuvia manabii kuandika, Biblia hiyo, atayafanya mafundisho ya Biblia, injili yake, ifae kuyabadilisha kabisa maisha yako ukimwalika Roho kuwapo wakati unapoisoma hiyo Biblia.
3. Umoja wa Biblia
Kwa kweli Biblia ni maktaba ya vitabu 66. vitabu 39 vya Agano la Kale viliandikwa kuanzia karibu na mwaka wa 1450 K.K hadi 400 K.K, Vitabu 27 vya Agano Jipya viliandikwa kati ya mwaka wa 50 B.K na mwaka wa 100 B.K.
Nabii Musa alianza kuandika vitabu vitano vya kwanza wakati fulani kabla ya mwaka wa 1400 K.K. Mtume Yohana alikiandika kitabu cha mwisho cha Biblia, yaani, kitabu cha Ufunuo, karibu na mwaka wa 95 B.K. Katika kipindi cha miaka 1,500 kati ya kuandikwa kitabu cha kwanza na cha mwisho cha Biblia, walau watu wengine wapatao 38 waliovuviwa walitoa mchango wao. Wengine walikuwa wafanya biashara, wengine wachungaji wa kondoo, wengine wavuvi, wengine askari, matabibu, wahubiri, wafalme - wanadamu toka katika tabaka zote za maisha. Mara nyingi waliishi katika utamaduni na falsafa vilivyohitilafiana.
Lakini hapa ndipo yalipo maajabu ya maajabu yote: Vitabu hivyo 66 vya Biblia pamoja na sura zake 1,189 zenye idadi ya mafungu 31,173 vikiwekwa pamoja, tunaona umoja na mwafaka katika ujumbe vinaoutoa.
Wa mwisho anapokwenda zake, kwa mshangao wewe unaona jengo zuri limesimama mbele yako. Ndipo wewe unajifunza kwamba sehemu kubwa ya "mafundi hao wanachonga mawe" hawajawahi kuonana kamwe, wakiwa wamekuja, kama walivyofanya, kutoka Amerika ya Kusini, China, Urusi, Afrika na sehemu nyingine za ulimwengu.
Je, wewe ungeamua nini? Ya kwamba mtu fulani alipanga umbo hilo lililojengwa kwa mawe ya kuchonga naye alimtumia kila mtu vipimo sahihi kutokana na kipande chake kile kimoja cha marumaru.
Biblia nzima inatoa ujumbe mmoja unaoshikamana - sawasawa tu na lile jengo la mawe yaliyochongwa ya marumaru. Mtu fulani mmoja mwenye akili alipanga yote hayo, yaani, ni akili za Mungu. Umoja wa kushangaza wa Maandiko Matakatifu unatoa ushahidi wake kwamba ingawa ni wanadamu walioyaandika mawazo yale, yalikuwa yamevuviwa naMungu.
4. Waweza Kuiamini Biblia
1. Kuhifadhiwa kwa Biblia ni jambo la ajabu sana. Maandiko yote ya awali ya Biblia yalinukuliwa kwa mkono - muda mrefu kabla ya kuwako
mitambo ya kuchapisha vitabu. Waandishi wale walitayarisha nakala za maandiko ya mkono ya asilia na kuzitawanya. Maelfu ya nakala kama hizo za maandiko ya mkono au sehemu zake bado ziko mpaka sasa.
mitambo ya kuchapisha vitabu. Waandishi wale walitayarisha nakala za maandiko ya mkono ya asilia na kuzitawanya. Maelfu ya nakala kama hizo za maandiko ya mkono au sehemu zake bado ziko mpaka sasa.
Mitume waliandika kwanza sehemu kubwa ya Agano Jipya kama nyaraka walizozituma kwa makanisa ya Kikristo yaliyoanzishwa baada ya kifo na ufufuo wake Kristo. Zaidi ya maandiko ya mkono 4,500 ya Agano Jipya lote au sehemu yake yanapatikana katika nyumba za Makumbusho na maktaba za Ulaya na Amerika. Baadhi yake yanakwenda nyuma hadi karne ile ya pili. Kuyalinganisha maandiko hayo ya mkono ya awali na biblia ya siku hizi, twaweza kuona kwa urahisi kwamba kwa kawaida Agano Jipya limeendelea pia kubaki bila mabadiliko yo yote tangu lilipoandikwa kwa mara ya kwanza.
Siku hizi Biblia au sehemu zake zimetafsiriwa katika lugha zaidi ya 2,060 na (dialects). Ni kitabu kinachouzwa sana ulimwengu: zaidi ya Biblia milioni 150 na sehemu za Biblia huuzwa kila mwaka.
Kwa mfano, kulingana na Mwanzo 11:31, Ibrahimu na familia yake "wakatoka wote katika Uru... waende katika nchi ya Kanaani." Kwa kuwa ni Biblia peke yake iliyosema juu ya Uru, mabingwa fulani wa Biblia walisema kwamba mji kama huo ulikuwa haujapata kuwako kamwe. Ndipo wachimbaji wa mambo ya kale wakagundua mnara wa hekalu katika nchi ya Iraki Kusini ukiwa na kwenye msingi wake iliyoandikwa katika maandishi ya kikabari yaliyokuwa na jina la Uru. Ugunduzi wa baadaye ulionyesha kwamba Uru ulikuwa ni mji mkuu ambao ulikuwa unasitawi wenye ustaarabu wa hali ya juu uliokuwa umefikiwa. Sura ya mji ule ilikuwa imesahaulika ni Biblia peke yake iliyolihifadhi jina lake - mpaka pale koleo ya mwanaakiolojia mmoja ilipouthibitisha ukweli wa kuwako kwake. Na huo Uru ni mmoja tu miongoni mwa mifano mingi ya akiolojia inavyothibitisha usahihi wa Biblia.
3. Kutimia kwa usahihi kabisa kwa utabiri wa Biblia hukuonyesha wewe kwamba unaweza kuitegemea Biblia. Maandiko hayo yana utabiri mwingi wa kushangaza sana wa matukio ya siku za usomi ambayo hivi sasa yanaendelea kutimia mbele ya macho yetu. Tutauchunguza baadhi ya unabii huo wa kusisimua katika masomo ya mbele.
5. Jinsi Ya Kuielewa Biblia
Unapolichunguza Neno la Mungu, weka kanuni hizi mawazoni mwako:
2. Soma Biblia kila siku. Kujifunza Biblia kila siku ni ufunguo wa kupata nguvu katika maisha yetu, ni kukutana na mawazo ya Mungu (Warumi 1:16).
3. Unapoisoma, iache Biblia ijieleze yenyewe. Uliza: mwandishi huyu wa Biblia alikusudia kusema nini? Kwa kuzingatia kile limaanishacho fungu hilo, twaweza kuitumia kwa akili katika maisha yetu ya leo hii.
4. Soma Biblia kwa kufuata somo. Linganisha andiko na andiko. Yesu alitumia mbinu hii kuthibitisha kwamba yeye alikuwa ndiye Masihi:
"Akaanza kutoka Musa na Manabii wote, akawaeleza katika maandiko yote mambo yaliyomhusu yeye mwenyewe."
"Akaanza kutoka Musa na Manabii wote, akawaeleza katika maandiko yote mambo yaliyomhusu yeye mwenyewe."
5. Jifunze Biblia ili kupokea uwezo wa kuishi kwa ajili ya Kristo. Neno la Mungu limeelezwa katika Waebrania 4:12 kama upanga mkali ukatao kuwili. Ni zaidi ya maneno tu yaliyo juu ya ukurasa, ni silaha iliyo hai mikononi mwetu ya kupigia na kuyaondolea mbali majaribu yale yanayotushawishi kutenda dhambi.
6. Sikiliza Mungu anapozungumza nawe kupitia katika Neno lake. Endapo mtu anataka kuujua ukweli wa Bilbia juu ya somo fulani, basi, ni lazima awe tayari kufuata yale inayofundisha (Yohana 7:17), sio yale anayofikiri mtu fulani, au yale yanayokaziwa na fundisho lolote la kanisa lake.
6. Biblia Yaweza Kubadilisha Maisha Yako
"Kuyafafanua maneno yako [Mungu] kwatia nuru, kunampa ufahamu mjinga" - (Zaburi 119:130).
Kujifunza Biblia kutauimarisha "ufahamu" wako, kutakupa nguvu ya kuyashinda mazoea yale yaletayo madhara, na kukuwezesha kukua kimwili, kiakili, kimaadili na kiroho.
Biblia inazungumza na moyo. Inashughulika na mambo yale yanayowapata wanadamu katika maisha yao - yaani, upendo, ndoa, uzazi na kifo. Inaliponya jeraha lenye kina kirefu sana katika tabia ya mwanadamu, pamoja na dhambi na taabu inayotokana nayo.
Kwa kuwa Mungu anafanya kazi yake kupitia katika Biblia, basi, inao uwezo mkubwa. Inaivunjavunja hata mioyo iliyofanywa migumu dhidi ya hisia zote za kibinadamu, inailainisha na kuijaza na upendo. Tumeona Biblia ikimbadilisha haramia wa zamani na mvuta bangi na kumfanya mhubiri aliye motomoto. Tumeona Biblia ikimbadilisha mwongo na mdanganyaji na kumfanya kuwa mwalimu mwaminifu na mwenye kuheshimika. Tumeona kitabu hicho kikiwanyakua watu wakiwa karibu na kujiua wenyewe na kuwapa tumaini la kuanza maisha upya. Biblia inaamsha upendo miongoni mwa maadui. Inawafanya wenye majivuno kuwa wanyenyekevu, na wachoyo kuwa wakarimu. Biblia inatutia nguvu tunapokuwa dhaifu, inatuchangamsha tunapokuwa katika hali ya kukata tamaa, inatufariji tunapokuwa na huzuni, inatuongoza tunapochoka sana. Inatuonyesha jinsi ya kuishi kwa ujasiri na jinsi ya kufa bila hofu.
Kitabu hicho cha Mungu, yaani, Biblia kinaweza kuyabadilisha maisha yako! Utagundua hivyo kwa dhahiri zaidi na zaidi, kadiri unavyoendelea kujifunza miongozo hii ya GUNDUA.
Kwa nini Biblia hiyo iliandikwa kwa ajili yetu? Yesu anatoa jibu: "Lakini hizi [kweli za Biblia] zimeandikwa; ili mpate kuamini ya kwamba Yesu ndiye Kristo, Mwana wa Mungu; na kwa kuamini muwe na uzima kwa jina lake" - (Yohana 20:31).
Sababu kuu kuliko zote kwa nini sisi tunapaswa kuyafahamu Maandiko Matakatifu ni kwamba yamejaa picha zinazomfunua Yesu Kristo na kutuhakikishia sisi uzima wa milele. Kwa kumtazama Kristo katika Biblia nzima, tunabadilika na kufanana naye zaidi. Basi, kwa nini wewe usianze sasa kugundua uwezo huo wa Neno la Mungu uwezao kukufanya wewe kufanana zaidi na Yesu?
YACHUNGUZENI MAANDIKO
TWAWEZA KUMWAMINI MUNGU
Siku moja Jimi alimwuliza mtu mmoja anayekana kuwa kuna Mungu endapo alipata kujaribu sana, hata kwa dakika chache tu, kupigana na wazo lisemalo kwamba huenda Mungu yuko.
1. Kila Kitu Kilichobuniwa Kina Mbunifu Wake
Muundo wa mwili wa kibinadamu unafanya iwepo haja ya kuwako mbunifu wake. Wanasayansi wanatuambia kwamba ubongo wetu hukusanya na kukumbuka picha elfu nyingi katika mawazo yetu, huyaunganisha matatizo yetu yote na kuyatatua, hufurahia kuona uzuri, huitambua nafasi ya mtu, na kutaka kukuza yaliyo bora ndani ya kila mtu. Chaji za umeme zitokazo katika ubongo huongoza shughuli zote za misuli ya miili yetu.
Kompyuta pia zinafanya kazi kwa njia ya mikondo ya umeme. Lakini ilichukua akili ya mwanadamu katika kuitengeneza hiyo kompyuta na kuiambia la kufanya.
Si ajabu, basi, kwamba mtunzi wa Zaburi alihitimisha kwa kusema kwamba mwili wa mwanadamu unasimulia habari za Muumbaji huyo wa ajabu kwa sauti kubwa iliyo wazi:
"Nakusifu maana nimefanywa kwa namna ya ajabu, matendo yako ni ya ajabu, wewe wanijua kabisa kabisa" - (Zaburi 139:14)
"Nakusifu maana nimefanywa kwa namna ya ajabu, matendo yako ni ya ajabu, wewe wanijua kabisa kabisa" - (Zaburi 139:14)
Hakuna pampu yoyote iliyotengenezwa na mwanadamu inayoweza kulinganishwa na moyo wa mwanadamu. Hakuna mtandao wo wote wa kompyuta uwezao kuwa sawa na mfumo wetu wa mishipa ya fahamu. Hakuna mfumo wo wote wa Televisheni unaofanya kazi yake vizuri kama sauti, sikio, na jicho la mwanadamu. Hakuna kiyoyozi kikuu cho chote (central air conditioning) wala mfumo wa kuipasha joto nyumba uwezao kushindana na kazi inayofanywa na pua, mapafu, na ngozi yetu. Mfumo wenye sehemu nyingi za ajabu wa mwili wa mwanadamu unadokeza kwamba mtu fulani alihusika katika kuubuni, na Mtu huyo fulani ni Mungu.
Mwili wa mwanadamu ni mfumo kamili wa viungo mbali mbali - vyote vikiwa vinashirikiana, vyote vikiwa vimeumbwa kikamifu. Mapafu na moyo, mishipa ya fahamu na misuli, hiyo yote hufanya kazi za ajabu mno kiasi cha kuwa vigumu kusadikika ambazo hutegemezwa juu ya kazi nyingine zilizo za ajabu mno kiasi cha kutufanya sisi tushindwe kusadiki.
Endapo ungetakiwa kuzipa nambari sarafu kumi kuanzia moja mpaka kumi, na kuziweka mfukoni mwako, na kuzitikisa-tikisa huku na huku, kisha kuzitoa mfukoni mwako na kuziweka tena mfukoni moja moja, je, kuna uwezekano gani kwamba ungefanya hivyo kwa kufuata mfuatano wa nambari zake sawa sawa? Kwa sheria ya mahesabu unayo bahati moja tu katika bilioni kumi ya kuzitoa kwa mpangilio wake kuanzia ya kwanza mpaka ile ya kumi.
Sasa, basi, hebu fikiria ni bahati ngapi tumbo la chakula, ubongo, moyo, ini, arteri, vena, figo, masikio, macho, na meno vingekuwa nazo vikikua vyote pamoja na kuanza kufanya kazi yao kwa dakika ile ile ya wakati mmoja.
Hivi maelezo ya busara kabisa ni yapi kuhusu ubunifu huo wa mwili wa mwanadamu?
"Kisha Mungu akasema, 'Natumfanye mtu kwa mfano wetu, kwa sura yetu,'..............Hivyo Mungu Akamwuumba Mtu Kwa Mfano Wake,...... mwanamume na mwanamke aliwaumba" - (Mwanzo 1:26,27).
Mwanaume na mwanamke wa kwanza wasingeweza kuwa wametokea wenyewe tu. Biblia inathibisha kwamba Mungu alitubuni sisi kwa mfano wake. Alituwaza katika mawazo yake na kutuumba.
2. Kila Kitu Kilichoumbwa Kina Muumbaji Wake
Lakini ushahidi wa kuwako kwake Mungu haufungamani tu na ubunifu wa miili yetu; pia umetandaa huko mbinguni. Acha taa za mjini, angalia juu katika mbingu ya usiku. Wingu lile jeupe kama maziwa lenye nyota, tunaloliita Mkanda wa Nuru (Milky Way) ambalo kwa kweli ni kundi la mabilioni ya majua (galaxy) yanayotoa mwanga mkali wa moto sawa na ule wa jua letu ambao unaweza kuonekana hapa duniani kwa kupitia katika darubini kubwa zilizopo hapa duniani kama ile darubini iitwayo "Hubble Telescope" iliyo katika anga za juu.
Si ajabu, basi, kwamba mtunga Zaburi alihitimisha kwa kusema kwamba nyota zinamtangaza Muumbaji Mtukufu:
"Mbingu zatangaza utukufu wa Mungu, anga ladhihirisha kazi ya mikono yake" (Zaburi 19:1-3).
"Mbingu zatangaza utukufu wa Mungu, anga ladhihirisha kazi ya mikono yake" (Zaburi 19:1-3).
Je, hivi sisi twaweza kutoa hitimisho gani la busara kwa kuangalia mpangilio huo unaotatanisha sana na ukubwa wa malimwengu yote?
"Yeye [Mungu] alikuwako kabla ya vitu vyote; vyote hudumu mahali pale kwa uwezo wake" (Wakolosai 1:17).
Viumbe vyote humshuhudia yule Mungu Mbunifu Mkuu na Muumbaji asiye na Mwisho. Katika maneno haya rahisi, "Hapo mwanzo Mungu," tunalipata jibu la siri ile ya uhai. Yuko Mungu aliyeumba kila kitu.
Wanasayansi wakuu wengi siku hizi wanamwamini Mungu. Dk. Arthur Compton, mwanafizikia mshindi wa tuzo ya Nobel, akitoa maoni yake juu ya fungu hilo la Maandiko, siku moja alisema hivi:
"Kwangu binafsi, imani huanza ninapotambua kwamba yule aliye na akili isiyo na kifani ndiye aliyeyaweka hayo malimwengu na kumwumba mwanadamu. Kwangu mimi si vigumu kuwa na imani hii, kwa maana ni dhahiri kwamba po pote pale palipo na mpango yupo Mungu mwenye akili. Malimwengu yaendayo kwa utaratibu, na kujifunua kwetu hushuhudia ukweli wa usemi huu adimu mno uliopata kunenwa - 'Hapo mwanzo Mungu'"
"Kwangu binafsi, imani huanza ninapotambua kwamba yule aliye na akili isiyo na kifani ndiye aliyeyaweka hayo malimwengu na kumwumba mwanadamu. Kwangu mimi si vigumu kuwa na imani hii, kwa maana ni dhahiri kwamba po pote pale palipo na mpango yupo Mungu mwenye akili. Malimwengu yaendayo kwa utaratibu, na kujifunua kwetu hushuhudia ukweli wa usemi huu adimu mno uliopata kunenwa - 'Hapo mwanzo Mungu'"
Biblia haijaribu kumthibitisha Mungu inatangaza kuwako kwake. Dk. Arthur Conklin, mwana biolojia, siku moja aliandika hivi: "uwezekano kwa uhai kutokea kwa ajali ni sawa na uwezekano kwa kamusi kamili kutokea kutokana na mlipuko katika kiwanda cha kuchapisha vitabu".
Twajua kwamba wanadamu hawawezi kutengeneza kitu cho chote bila kutumia kitu kingine. Twaweza kujenga vitu, kuvumbua vitu, kuunganisha vitu, lakini kamwe hatujapata kufanya kitu cho chote bila kuwa na kitu kingine cha kuanzia, awe ni chura mdogo kabisa ua la kawaida kabisa. Vitu vituzungukavyo pande zote hupiga kelele vikisema Mungu ndiye aliyevibuni, Mungu ndiye aliyeviumba, Mungu ndiye anayevitegemeza. Jibu pekee linaloaminika kuhusu chimbuko la malimwengu hayo, dunia hii, na wanadamu - ni Mungu.
3. Mungu Huingia Katika Mahusiano Na Watu Binafsi
Mungu yule aliyezibuni mbingu hizo na nyota, aliyeyaumba malimwengu hayo, anatafuta kuwa na uhusiano nasi binafsi. Alikuwa na uhusiano wake binafsi na Musa: "Bwana akasema na Musa....kama vile mtu asemavyo na rafiki yake" (Kutoka 33:11). Mungu Mwenyewe anataka kuingia katika uhusiano nawe na kuwa Rafiki yako. Yesu aliwaahidi wale wanaomfuata, akisema "Ninyi mmekuwa rafiki zangu" (Yohana 15:14).
Sisi sote tumeshughulika sana na wazo hilo la Mungu, kwa kuwa wanadamu kwa asili wanapenda dini. Hakuna mnyama yeyote ajengaye madhabahu kwa ajili ya ibada. Lakini kila mahali unapowakuta wanaume na wanawake, unawakuta wakiabudu. Ndani ya kila moyo wa mwanadamu kuna ufahamu kuwa Mungu yuko, tamaa ya kuwa rafiki wa Mungu. Tunapoitikia hiyo tamaa yetu na kumpata Mungu, hatuwi na mashaka tena juu ya kuwako kwake na hitaji letu.
Katika miaka ile ya 1990 mamilioni ya wanaomkana Mungu katika nchi ya Urusi waliachana na imani yao hiyo ya kumkana Mungu, kisha wakamgeukia Mungu. Profesa wa Chuo Kikuu cha St. Petersburg alitoa kauli yake inayofanana na maoni yaliyotolewa na wakana Mungu wengi katika Umoja wa Kisovieti iliyopita:
"Nimetafuta maana ya maisha katika utafiti wangu wa kisayansi, lakini sikuona kitu chochote cha kutegemea. Wanasayansi wanaonizunguka mimi wanazo hisia hizo hizo za ukiwa. Nilipoangalia ukubwa wa malimwengu katika somo langu la elimu ya nyota, kisha nikaangalia ukiwa uliomo moyoni mwangu, niliona kwamba ni lazima pawe na maana fulani. Kisha nilipoipokea Biblia uliyonipa na kuanza kuisoma, ukiwa katika maisha yangu ukajazwa. Nimeiona Biblia kuwa ndiyo chimbuko la pekee la matumaini kwa nafsi yangu. Nimempokea Yesu kama Mwokozi wangu, nami nimepata amani ya kweli pamoja na kuridhika katika maisha yangu".
Mkristo anamwamini Mungu kwa sababu yeye amekutana naye na kugundua kwamba anayatosheleza mahitaji makubwa sana ya moyo wake. Mungu ambaye Wakristo wamemuona kuwa yuko, anatupatia mtazamo mpya, maana mpya, makusudi mapya na furaha mpya.
Katika miaka ile ya 1990 mamilioni ya wanaomkana Mungu katika nchi ya Urusi waliachana na imani yao hiyo ya kumkana Mungu, kisha wakamgeukia Mungu. Profesa wa Chuo Kikuu cha St. Petersburg alitoa kauli yake inayofanana na maoni yaliyotolewa na wakana Mungu wengi katika Umoja wa Kisovieti iliyopita:
"Nimetafuta maana ya maisha katika utafiti wangu wa kisayansi, lakini sikuona kitu chochote cha kutegemea. Wanasayansi wanaonizunguka mimi wanazo hisia hizo hizo za ukiwa. Nilipoangalia ukubwa wa malimwengu katika somo langu la elimu ya nyota, kisha nikaangalia ukiwa uliomo moyoni mwangu, niliona kwamba ni lazima pawe na maana fulani. Kisha nilipoipokea Biblia uliyonipa na kuanza kuisoma, ukiwa katika maisha yangu ukajazwa. Nimeiona Biblia kuwa ndiyo chimbuko la pekee la matumaini kwa nafsi yangu. Nimempokea Yesu kama Mwokozi wangu, nami nimepata amani ya kweli pamoja na kuridhika katika maisha yangu".
Mkristo anamwamini Mungu kwa sababu yeye amekutana naye na kugundua kwamba anayatosheleza mahitaji makubwa sana ya moyo wake. Mungu ambaye Wakristo wamemuona kuwa yuko, anatupatia mtazamo mpya, maana mpya, makusudi mapya na furaha mpya.
Mungu hatuahidi sisi kwamba tutakuwa na maisha yasiyo na taabu, wala mapambano, ila yeye anatuhakikishia kwamba atatuongoza na kutusaidia kama tutakuwa na uhusiano binafsi naye. Na mamilioni ya Wakristo wanaweza kutoa ushuhuda wao kwamba ingekuwa heri kwao kuacha kila kitu kuliko kuyarudia maisha yale yasiyokuwa na Mungu.
Hii ndiyo ajabu kuu kuliko zote kwamba yule Mungu Mwenyezi aliyeyabuni, aliyeyaumba na kuyategemeza malimwengu hayo anataka kufanya uhusiano na kila mwanaume na mwanamke, kila mvulana na msichana. Daudi alishangaa sana kuhusu jambo hilo alipoandika maneno haya:
"Nikiangalia mbingu, kazi ya vidole vyako, mwezi na nyota ulizozimika huko, mtu ni nini ee Mungu hata umfikirie mwanadamu ni nini hata umjali?" - (Zaburi 8:3,4).
Muumbaji wetu ana "mjali" kila mmoja wetu. Yeye binafsi anakupenda sana wewe kana kwamba wewe ulikuwa ni kiumbe chake cha pekee alichokiumba.
Basi tunaweza kumwamini Mungu:
(1) Kwa sababu ya ubunifu wake wenye sehemu nyingi katika kila kitu alichokiumba ambacho kinatuzunguka sisi.
(2) Kwa sababu shauku ile iliyomo ndani yetu juu ya Mungu inatufanya tusiwe na raha mpaka tupatapo pumziko letu ndani yake tena.
(3) Kwa sababu tunapomtafuta na kumpata, Mungu hutosheleza kila haja tuliyo nayo pamoja na shauku yetu - kikamilifu!
(1) Kwa sababu ya ubunifu wake wenye sehemu nyingi katika kila kitu alichokiumba ambacho kinatuzunguka sisi.
(2) Kwa sababu shauku ile iliyomo ndani yetu juu ya Mungu inatufanya tusiwe na raha mpaka tupatapo pumziko letu ndani yake tena.
(3) Kwa sababu tunapomtafuta na kumpata, Mungu hutosheleza kila haja tuliyo nayo pamoja na shauku yetu - kikamilifu!
4. Ni Mungu Wa Aina Gani?
Ni jambo la busara tu kwamba Mungu aliye na nafsi yake apende kujifunua mwenyewe kwa viumbe wake kama vile baba atakavyo watoto wake wamjue. Na katika Biblia Mungu anatuambia yeye ni nani, tena anafananaje.
Ni mfano gani alioutumia Mungu katika kuwaumba wanaume na wanawake?
"Hivyo Mungu akaumba mtu kwa mfano wake, kwa mfano wa Mungu alimwumba" (Mwanzo 1:27).
Kwa kuwa sisi tumeumbwa kwa mfano wa Mungu, basi, uwezo wetu wa kufikiri na kujisikia, kukumbuka na kutumaini, kutafakari na kuchambua mambo - chimbuko lake lote latoka kwake. Je, tabia kuu ya Mungu ni ipi?
"Mungu ni upendo" (1 Yohana 4:8).
Mungu hufanya uhusiano wake na wanadamu kutokana na moyo wake wa upendo. Hakuna kitu cho chote alichofanya au atakachopata kufanya ambacho hakijasababishwa na upendo wake usio na ubinafsi, ujitoao mhanga.
5. Jinsi Yesu Anavyotufunulia Alivyo Mungu
Katika Biblia Mungu anarudia tena na tena kueleza habari zake Mwenyewe kwamba Yeye ni Baba.
"Je! Sisi sote si watoto wa baba mmoja"?
"Je, sisi sote hatukuumbwa na Mungu yule yule?" Malaki 2:10.
"Je, sisi sote hatukuumbwa na Mungu yule yule?" Malaki 2:10.
Baadhi ya mababa tuwaonao leo si cho chote, bali hawapendezi. Kuna mababa wasiojali, mababa wanaotukana matusi. Mungu si kama hao. Yeye anajali, ni Baba anayeguswa sana na mambo yetu. Ni Baba apendaye kucheza na mwanawe au binti yake, ni Baba anayewafurahisha sana watoto wake kwa kuwasimulia hadithi kabla hawajaenda kulala usiku.
Baba yetu huyo mwenye upendo alitaka kufanya zaidi ya kule kujifunua Mwenyewe kwa njia ya maneno ya Maandiko. Alijua kwamba yule mtu tunayeishi naye ni mtu halisi kuliko yule tunayesikia tu habari zake au tunayesoma habari zake. Kwa hiyo yeye akaja katika dunia yetu kama mtu halisi - yaani, yule mtu Yesu.
Basi kama wewe umemwona Yesu, utakuwa umemwona Mungu. Alijishusha hadhi yake na kuwa sawa sawa na sisi akawa kama sisi - ili apate kutufundisha jinsi ya kuishi na kuwa na furaha, ili kwamba sisi tupate kuona jinsi Mungu alivyo hasa. Yesu ni Mungu aliyeonekana kwa macho. Yeye mwenyewe alisema, "Aliyeniona mimi amemwona Baba" (Yohana 14:9).
Usomapo kisa cha Yesu katika vitabu vinne vya Injili, yaani, vitabu vinne vya kwanza vya Agano Jipya, utagundua picha ya kuvutia sana ya Baba yetu aliye mbinguni. Wavuvi wale wa kawaida tu walizitupa nyavu zao ili kumfuata Yesu, na watoto wadogo wakasongamana kwenda kwake kupokea baraka zake. Aliweza, kumfariji mwenye dhambi aliyeharibika kabisa na kuzivunja nguvu za mnafiki sugu aliyejihesabia haki yeye mwenyewe. Aliponya kila maradhi kuanzia upofu hadi ukoma. Katika matendo yake yote Yesu alidhihirisha kwamba Mungu ni upendo! Alikidhi haja ya mwanadamu kwa namna ambayo hakuna mtu ye yote aliyepata kufanya hivyo kabla yake au tangu wakati wake!
Ufunuo wa Yesu wa mwisho ambao unaonyesha utukufu wa jinsi Mungu alivyo ulitokea pale msalabani.
"Kwa maana jinsi hii Mungu aliupenda ulimwengu, hata akamtoa Mwanawe pekee, ili kila mtu amwaminiye asipotee, bali awe na uzima wa milele" - (Yohana 3:16).
Yesu alikufa sio tu kutupatia maisha yenye furaha sasa, bali kutupa uzima wa milele pia. Kwa vipindi virefu watu walishangaa, na kutumaini, na kuota
ndoto juu ya Mungu. Waliiona kazi ya mikono yake mbinguni na katika uzuri wa viumbe vya asili. Kisha pale msalabani, Yesu alikivunjilia mbali kimya cha vizazi vingi, na watu wakajikuta wanautazama ana kwa ana uso wa Mungu, wakimwona yeye kama alivyo hasa - yeye ni upendo, wa milele, tena ni upendo udumuo milele!
ndoto juu ya Mungu. Waliiona kazi ya mikono yake mbinguni na katika uzuri wa viumbe vya asili. Kisha pale msalabani, Yesu alikivunjilia mbali kimya cha vizazi vingi, na watu wakajikuta wanautazama ana kwa ana uso wa Mungu, wakimwona yeye kama alivyo hasa - yeye ni upendo, wa milele, tena ni upendo udumuo milele!
Wewe waweza kumgundua Mungu sasa hivi Yesu anapomfunua kwako. Ugunduzi huo utakufanya utoe uthibitisho wako binafsi, ukisema: "Baba, nakupenda!"
Subscribe to:
Posts (Atom)














