Waweza Kuishi na Yesu, lakini huwezi kuishi bila Yesu.Yohan 3:16

BIBLIA IZUNGUMZIAVYO NAFASI YA MWANAMKE KATIKA KATISA NA UTUME.

KWANINI TUNACHAGUA WAZEE WA KANISA WA KIUME TU, HATUCHAGUI NA WA KIKE.
By Petro Tumaini

Ofisi ya kanisa la agano jipya inataja vyeo vikubwa viwili vya uongozi wa kanisa amabavyo ni mashemasi na wazee wa kanisa. Umuhimu wa ofisi hizi unaelezewa kwa kiwango cha hali ya juu ya kiroho na kimaadili kwa wale watakiwao kushikilia nafasi hizi.

Kanisa linatambua utakatifu kwa  wito wa utume huu kwa kuwekea mikono na ndiyo maana baada ya kanisa la Mitume kuanzishwa na kupata viongozi ambao ni Stefano, Filipo, Prokoro, Nikanori , Timothi, Parmena, na Nikolao  waliwekewa mikono .
Tokea agano la kale Mungu aliwaweka wakfu wanaume waweze kufanya kazi katika Hekalu lake takatifu, lakini bado kuna kazi za kiroho zilifanywa na wa wanawake kama vile kazi ya nabii.

Mwanamke aliumbwa kama msaidizi (ezer-help) hii humaanisha mtendakazi pamoja na mwanaume wa Mwanaume na si wa kukanyagwa.

Jambo hili halikumtenga na shughuli za kanisa, japokuwa kunashughuli zilizofanywa na wanaume tu hekaluni na kanisani kama tutakavyoona, lakini hebu tuangalie shughuli walizoshiriki wanawake tokea agano la kale.

Nafasi ya Mwanamke kanisani
ØNabii.Wanawake walishiriki katika nafasi ya kuzungumza na Mungu tokea agano la kale hadi Jipya (Manabii)

ØMiriam

Kutoka 15:20. Na Miriam Nabii mke Ndugu yake Haruni, , akatwaa tari mkononi mwake; wanawake wakatoka wote wakaenda nyuma yake, wenye matari na kucheza.

ØDebora
Waamuzi 4:4. Basi Debora, nabii mke , mkewe  Lapidothi, ndiye aliyekuwa mwamuzi wa Israeli wakati ule.

ØMke wa Isaya

Isaya 8:3. Nami nikamwendea Huyo nabii Mke, naye akapata miimba, akazaa motto mwanamume. Kisha nikamwambia Mwite jina lake Maher- Shalal-Hash-Bazi.

ØWatoto wa Filipo

MAtendo 21:9. Mtu huyu alikuwa na binti wane, mabikira waliokuwa wakitabiri.(whp prophesized NKJV)

ØKatika huduma (Ibada) .
Wao walifika kusikiliza tu neno la Mungu.
ØNehemia 8:2-3

Ø    Muziki

ØKutoka 15:20-21

Ø1 Nyakati 25:5




Wakati wowote tokea anguko mwananamke aliwekwa kuwa chini ya mwanaume , ni kusudi la Mungu mwanamke atawaliwe ,na mdiyo maana katika Biblia mwanamke aliyetaka kumtawala mwanaume ilikuwa ni hukumu.

ØIsaya 3:12. Katika habari za watu wangu, watoto ndio wanaowaonea, na wanawake ndio wanaowatawala. Enyi watu wangu, wakuongozao wakukosesha, waiharibu njia ya mapito yako.


Kwa kifupi ,majuikumu ya mwanamke tokea dhambi iingie,  dhambi iliingilia kupitia kwake- vilevile mkombozi alizaliwa kupitia mwanamke mwaminifumwaminifu - huyo pia alishiriki katika kuomba ujio wa Roho mtakatifu matendo 1:13-14, Lidya alimkarimu Paulo Mdo 16:14, mwongofu wa Kwanza Ulaya ni mwanamke .

Paulo alipopata maono kumwendea mtu wa mataifa alikuta wanawake wakisali, kwahiyo tokea agano la kale hadi agano jipya wanawake wameshiriki kikamilifu katika huduma za kanisa na ukombozi .

Pamoja na hayo yote bado kuna mipaka ya huduma za wanawake katika kanisa. Kwa mfano Paulo na wazee wenzake walisaidiwa na wanawake katika huduma, hii haimaanishi kwamba wanawake walichukua vyeo vya wazee hao.

ØWarumi 16:6. Nisalimieni Mariamu, aliyejitaabisha sana kwaajili yetu.

ØWarumi 16:3 Nisalimieni Prisca na akila, watenda kazi pamoja nami katika kristo Yesu.

ØWarumi 16:1-2. Namkabidhi kwenu Fibi, ndugu yetu, ndiye mhudumu wa kanisa lililoko Kenkrea. Neno mhudumu lililotumika hapa limetokana na neon DEACENESS ambaye ni mtumishi wa kawaida wa kanisa yaani shemasi.


Shughuli Zilizofanywa na wanaume tu
Ø    Ukuhani.
Ø Hesabu 28:1 Nawe umlete Haruni ndugu yakokaribu nami, na wanawe pamoja naye, miongoni mwa wana wa Israeli, ili anitumikie katika kazi ya ukuhani. Haruni na Nadabu, na Abihu, na Eliazari, na Ithamari, wana wa Haruni.  Mafungu Mengine kuhusu kazi hii ni Hesabu 18:1-7.

ØWazee (maaskofu)

Ni wazee waliowahi kuhudumu kama waamuzi, viongozi wa familia

Matendo 6:6. ambao akawaweka mbele ya mitume, na walipokwisha kuomba wakaweka mikono yao juu yao.

Matendo 13:2,3. Basi hawa walipokuwa wakimfanyia Bwna ibada na kufunga, Roho Mtakatifu  akasema , Nileteeni Barnaba na Sauli kwa kazi ile niliyowaitia. Ndipo wakiisha kufunga na kuomba , wakaweka mikono yao juu yao , wakawaacha waende zao. Pia waweza kusoma  1 Timotheo 4:14; 5:22


Uongozi wa Kanisa unawekwa na Mungu kwahiyo hata viongozi wake ni sharti watimize maagizo na kanuni zilizowekwa na Mugu japokuwa huchaguliwa na wanadamu .

Nafasi ya wazee ambao leo tunawatambua kama maaskofu au wazee wa kanisa ni nafasi inayotajwa kushikiliwa na wanaume tu pote katika Biblia , hii ndiyo sababu hata katika kanisa letu leo hatuchagui wazee wa kanisa wa kike.


MAANA YA MZEE WA KANISA

Biblia katika agano jipya iliandikwa katika ligha ya kigiriki, kwa lugha hii neno wazee limetokana na neno presbuteros au askofu( bishop). Linamaanisha mtu  mzee au mwenye mamlaka nah ii ni kwasababu biblia inamfananisha na mtu anayelisimamia kanisa kwahiyo ni mtu wa kuheshimiwa sawasawa na jina lake linavyomaanisha.

Neno askofu (Bishop) pia lilimaanisha mtawala na Paulo aliyatumia maneni yote mawili kwambadilishano.

Matendo 20:17,28. Toka Mileto Paulo akatuma watu kwenda Efeso, akawaita wazee wa kanisa. 

Tito 1:5,7 .Kwasababu hii nilikuacha Krete, ili uyatengeneze yaliyopunguka, na kuweka wazee katika kila mji kama vile nilivyokuamuru . Maana imempasa askofu awe mtu asiyeshtakiwa neno , kwa kuwa ni wakili wa mungu; asiwe mtu wa kujipendeza nafsi yake, asiwe mwepesi wa hasira, asiwe mlevi wala mgomvi, asiwe mpenda mapato ya aibu.

Katika kanisa lililounwa upya Mzee wa kanisa  kilikuwa ni cheo cha kiofisi halafu askofu ikamaanisha majukumu ya ofisisi.

SIFA ZA MZEE WA KANISA
Hizi ni sifa za kiroho , na wala si sifa za kimwili kama zitumiwazo kuwachagua Viongozi wa kidunia.  Zinatajwa katika kitabu vifuastavyo 1Timotheo 3:1-7. Tito 1:5-9.

Ni wazi kabisa kutokana na sifa ambazo Biblia imeziainisha kuhusiana na mzee wa kanisa zinadhihirisha wazi kwamba Mungu alikusudia wazee wa kanisa kuwa Wanaume na ndio maana katika msingi wa  mafungu hayo hapo juu tunapata sifa zifuatazo.

1)Asiyelaumika.
2) Mume wa mke mmoja na sio mke wa mume mmoja.
3)Mwenye kiasi na busara
4)Mwenye kiasi, utaratibu.
5)Mkarimu.
6) Asiyezoea ulevi  watu hutumia usemi huu kumaanisha kuwa askofu awe mtu mlevi lakini asijizoeshe ulevi lakini  Tito anasema asiwe mlevi wala mgomvi..
7)Mpole.n.k

Pote ambapo eidha wazee wanachaguliwa, au sifa za mzee wa kanisa zinatajwa zinadhiirisha kwamba nafasi hii ni ya kushikiliwa na wanaume tu.

ØKUFUNDISHA KANISANI(SPIRITUAL AUTHORITY).

1 Timotheo  2:11-12.Mwanamke na ajifunze kwa utulivu, akitii kwa kila namna. Simpi mwanamke ruhusa ya kufundisha wala kumtawala mwanaume bali awe katika utulivu. Kwa maana Adam ndiye aliyeumbwa kwanza na Hawa baadae. Wala Adam hakudanganywa, ila mwanamke alidanganywa kabisa akaingia katika hali yua kukosa.

1 Kor 14:34-35.  Wanawake na wanyamaze katika kanisa, maana hawana ruhusa ya kunena bali watii, kama vile inenavyo torati nayo. Nao wakitaka kujifunza neon lolote, na wawaulize waume zao wenyewe nyumbani mwao; maana ni aibu mwanamke kunena katika kanisa.

Wanazuoni wamekuwa na mitazamo tofauti kuhusiana na Ayah hii..

1)Paulo alikuwa analenga kwa wanawake wa Efeso ambao walikuwa wanashuhudia  wanawake wa kipagani wakiendesha Ibada katika hekalu la atemi na hivyo aliwaonya wanawake wa Efeso ili wasiende katika mahekalu hayo na wasilete utamaduni huo. Upungufu unaonekana pale anapowaandikia na wakorintho kwahiyo pamoja na kwamba hoja inaweza kuwa na ukweli bado inamapungufu.

SDA Bible commentary ukurasa wa 792 . Inaelezea kama ifuatavyo..


Fungu hili limeunganishwa na fungu la 33 ambalo linasomeka hivi  “Kwa maana Mungu si Mungu wa macahafuko, bali wa amani, vilevile kama ilivyo katika makanisa yote ya watakatifu…Kutokana na maelezo hayo wanawake kunyamaza kimya inaonyeshwa kuwa si msimamo uliosababishwa na mmatatizo ya sehemu mahalia tu , lakini ni kuakisi utaratibu wa jumla katika makanisa yote. Ili kutdhihirisha kuwa huo ni msimamo wa makanisa yote   inaonekana pia katika  2 Timotheo 2:11,12.

Katika fungu la timotheo Paulo anatoa katazo bila kutaja kanisa moja na kusema   “Mwanamke na ajifunze kwa utulivu, akitii kwa kila namna. Simpi mwanamke ruhusa ya kufundisha wala kumtawala mwanaume bali awe katika utulivu”

Wengi wamepata ugumu kuelewa fungu hili si kwasababu tu ya nafasi aliyonayo mwanamke katika kanisa la leo bali pia nafasi na huduma ya Mwanamke katika historia.

ØWaamuzi 4:4
Ø2 Wafalme 22:14
ØLika 2:36,37
ØMatendo 21:9

KAMA VILE INENAVYO TORATI

Maandiko yanafundisha kwamba , kwa upande wa mwanamke katika anguko, mwanamke amepewa jukumu na Mungu kuwa na nafasi ya kuwa chini ya (subordination) na Mwanaume.

ØMwanzo 3:6,16
ØWaefeso 5:22-24
Ø1 Timotheo 2:11
ØTito 2:5
Ø1 Petro 3:1,5,6

“Kwa kujisababishia kubadilisha asili yake kwa kuleta uzoefu wa dhambi katika maisha yake, maisha ya amani ambayo mwanadam aliyajua hapo mwanzo yalifikia mwisho. Haikuwezekana tena kiutendaji kwa mwanaume na mwanamke kuwa na usawa katika uongozi wa nyumbani, na mungu alichaguwa kuweka kwa mwanaume jukumu la kufanya maamuzi ya familia yake.


AU JE NENO LA MUNGU LILITOKA KWENU

Kanisa la wakorintho halikuwa la kwanza kuanzisha bali miongoni mwa makanisa ya mwisho, hivyo halikutakiwa kuanzisha taratibu zake kama linavyjitakia bali lilitakiwa kufuata taratibu zinazotumiwa na makanisa mengine katika utaratibu wa kuendesha Ibada.

Kanisa lilianzisha taratibu zisizo zakawaida , kama vile kumruhusu mwanamke kuonekana katika huduma za jumuiya bila kufunika kichwa.

1 Wakorintho 11:5,16. Bali kila mwanamke asalipo au anapohutubu, bila kufunikwa kichwa, yuaibisha kichwa chake: kwa maana ni sawasawa na yule saliyenyolewa.  Maana mtu yeyote akitaka kuleta fitina sisi hatuna desturi hiyo wala makanisa ya mungu.

Wanawake walikuwa na kawaida ya kutoa unabii tokea agano la kale, ilifikia hatua wanawake wa Korintho walitaka wanapotoa unabii wasifunike vichwa kama wanaume.. 1 Kor 11:4.
Agenda ya idara ya wanawake ni  mbinu atumiayo shetani kufanya kanisa la Mungu likiuke maagizo ya biblia na roho ya Unabii.
Katika taarifa ya mkutano wa Vatikan City  uliofanyika tar 28/02/1999, ukiwa na wajumbe 1000 na viongozi wa serikalini 3000 ambao miongoni mwa wajumbe wake walikuwemo Roman Catholic,Lutheran church,Seventh Day Adventist Church.Jehova’s Wtness, Church of jesus Christ of latter dat saints (mormons), All Pentecostal Churches,Brethren Assemblies, Salvation Army, Church of England (Anglican), Presbyterian Church, London Missionary Society, Baptist church, Methodist Church.
Katika agenda ya MUUNGANO WA MAKANISA, moja ya dondoo za barua imenukuliwa kama ifuatavyo. “Makanisa katoliki yametenga mfuko wa kuendesha chombo kinachoitwa Davidian movement ndani ya kanisa ili kuwasaidia akina mama makanisani, nakwahiyo jina dorkas halina budi kubadilishwa na kuitwa huduma za akina mama kanisani (Women’s Ministry).
Kwa mujibu wa kikao hicho inamaanisha agenda ya idara ya wanawake ni fundisho kutoka rumi na si la biblia wala roho ya unabii.
JE NABII ELLEN G WHITE ALISEMAJE KUHUSU KUPIGANIA HAKI ZA WANAWAKE KANISANI?
  (1T,page 421… Those who feel called out to join the movement in favor of woman's rights and the so-called dress reform might as well sever all connection with the third angel's message. The spirit which attends the one cannot be in harmony with the other. The Scriptures are plain upon the relations and rights of men and women…)
Maana yake “wale wanaojisikia kwamba wanaitwa kuungana na wapiganiaji wa haki za wanawake na na kile kiitwacho matengenezo ya mavazi wanapaswa pia kuuondoa muungano ujumbe wa malaika watat. Roho ijihudhurishayo kwa mmoja haiwezi kufungamana na nyingine.Maandiko yako wazi juu ya mahusiano ya mwqanaume na mwanamke.”( Shuhuda kwa Kanisa, Gombo la kwanza uk 421.)


Mwanamke kwa mtazamo wa kibliblia hawezi kushikilia wadhifa kama mzee wa kanisa, askofu au mchungaji kama ijulikanavyo leo. Hii haimaanishi kwamba hawapaswi kushiriki katika uinjilisti, bali katika kushughulika kwao waweza kufanya majulumu mengine ya kanisa lakini wadhifa na majukumu ya mzee wa kanisa, askofu na wachungaji biblia huonyesha kwamba ni ya wanaume tu.

Eastern Tanzanian Conference yaanzisha Shule ya Sekondari.

Mapema mwaka huu, kanisa la Waadventista Wasabato kupitia uongozi wa kanda ya Mashariki (ETC) limeanzisha shule ya sekondari mkoani morogoro ambayo tayari inawanafunzi zaidi ya 30 wa kidato cha kwanza.
Kwa mujibu wa mmojawapo wa watenda kazi katika shule hiyo iitwayo Kitungwa Sekondari alisema   usajili tayari uko katika mchakato na unatarajiwakukamilika hivi karibuni kwani masharti yaliyotakiwa kutimizwa tayari yameshakamilishwa.



MUNGU ATABIRI ANGUKO LA SHETANI




Adam na hawa walijikuta katika uadui na Mungu baada ya kufuata
udanganyifu wa shetani badala ya kushikiia ahadi za Mungu





SHETANI APONDWA KICHWA
By Petro Tumaini.
Akiwa amefanikiwa kumdanganya Hawa na Hatimaye Adam, ni ndani ya muda mfupi tu uongo wake ulioneka wazi.Kifuatacho ni kiini cha uongo aliotamka shetani akimshawishi Eva kula tunda la mti wa ujuzi wa mema na mabaya:-

Ø    Mwanzo 3:4. Nyoka akamwambia Mwanamke, Hakika hamtakufa

Baada ya  Eva kula tunda la ujuzi wa mema na mabaya na hatimaye mumewe Adam kushawishika kula tunda hili kwa kumhurumia mkewe, kwa mara ya kwanza Mungu akatamka sentesi ya kifo ,kauli iliyoanika uongo wa ibilisi alioutumia akimshawishi Eva kula tunda alilokataza Mungu.

AKIDHIIRISHA UONGO WA IBILISI HIVI NDIVYO MUNGU ALIVYOSEMA
Ø    Mwanzo 3:19. Kwa jasho la uso wako utakula chakula, hata utakapoirudia ardhi, ambayo katika hiyo ulitwaliwa; kwa maana u mavumbi wewe, nawe mavumbini nutarudi.

Laana kubwa iliyoletwa na dhambi ni kifo, lakini ni dhumuni la shetani kuwadanganya wanadamu hasa katika siku hizi za mwisho kwamba watakapotenda dhambi hakika hawatakufa, kama alivyomdanganya Hawa .

Fundisho la kwanza ambalo kwalo shetani alilitumia kumdanganya Eva ndilo fundisho kuu atumialo kuwadanganya waumini wengi katika siku hizi za mwisho, nalo “Mwanadamu akifa rho yake huendelea kuishi”.Ili utambue kuwa fundisho hili limekubaliwa na jopo kubwa la jamii ya wanadamu ni rahisi tu hudhuria misiba mingi nawe utasikia kauli hii “Mungu ailaze pema roho ya marehemu”. Huu ni uongo usio na chembe ya ukweli ndani yake.

Ø    Mwanzo 3:4,5. Nyoka akamwambia mwanamke, hakika hamtakufa. Kwa maana Mungu anajua ya kwamba siku mtakapokula matunda ya mti huo,mtafumbuliwa macho, nanyi mtakuwa kama Mungu, mkijua mema na Mabaya.

Udanganyifu wa shetani atumiao kuudanganya ulimwengu watu wa leo hauna tofauti na ule wa pale edeni, hujaribu kuonyeshadhambi kama kitu kizuri kana kwamba mtu atendapo dhambi anafumbuliwa macho na kuwa na uelewa mpana zaidi jambo ambalo si la ukweli.

Wakati huohuo humuweka Mungu katika sura ambayo humfanya aeleweke vibaya, na ndo maana alimwambia Eva kuwa Mungu kwa kuwakataza wasile mti wa ujuzi wa mema na mabaya aliwafumba macho, si jambo la kushangaza kuona leo vijana wakidanganyana kufanya uzinzi ili kupata maarifa ya ndoa na uzoefu wa maisha hayo.

Aidha shetani huwashawishi watu kunywa pombe ili kuchangamsha akili, kiukweli haya yote yanatudhihirishia kuwa historia inajirudia, Adam na Hawa walipokula tunda la ujuzi wa mema na mabaya walifumbuliwa macho na kuona mabo ya kusikitisha na kuumaza.

Hili lilidhiirisha kwamba Mungu hakuwa na nia mbaya alipowakataza wasile tunda la ujuzi wa mema na mabaya, kwanza walijitambua kuwa wako uchi. Utukufu wa Mungu uliowasitiri hapo mwanzo uliwatoka baada tu ya kutenda dhambi.

Wakati huo huo hofu na uoga uliwaingia, tofauti na walivyozoea kuzungumza na Mungu ana kwa ana hatimaye walianza kumkimbia mungu.

Baya zaidi ni Pale Mungu alipozungumza kwa mara ya kwanza sentensi ya kifo kwa wanadamu ambao alikusudia waishi milele katika maoisha ya furaha yasiyo na kifo, huzuni , uadui wala magonjwa.

Ø    Warumi  6:23. Kwa maana mshahara wa dhambi ni mauti; bali karama ya Mungu ni uzima wa milele katika Kristo Yesu Bwana wetu.

“Ikumbukwe kwamba lilikuwa ni kusudi la mungu mwanadamu aendelee kukua kiakili na kimwili endapo tu asingekubali kujiingiza katika mtego wa kutenda dhambi baada ya kushawishiwa na shetani.”

Kwa Kuwadanganya Adam na Hawa shetani alifanikiwa kuingiza laana ya kifo katika jamii ya wanadamu. Ni kama vile alionekana kupata ushindi juu ya wanadamu kwa kuwaweka chini ya laana hiyo kwa kuvunja maagizo na namri za Mungu ambazo ni ufunuo wa mapenzi yake na Msingi wa serikali yake Mbinguni.

MUNGU ATANGAZA VITA NA NAMNA YA KUPATA USHINDI.

Akizungumza laana ya dhambi juu ya Mwanamke, Mwanaume , Shetana na Ardhi katika kitabu cha MWanzo 3:13-19. Mungu alionyesha Tumaini la Pekee kwa wanadam ambao tayari walijiingiza katika laana ya dhambi ambayo ni kifo.

TUMAINI LILIONEKANA MUNGU ALIPOTANGAZA VITA KUU KATI YA  SHETANI NA KANISA LA MUNGU.


Shetani alipondwa kichwa (alimalizwa nguvu na kushindwa) kupitia kifo cha
Yesu pale msalabani.(Warumi 16:20)


Ø    Mwanzo 3:14,15. BWANA Mungu akamwambia nyoka, Kwasababu umefanya hayo,umelaaniwa wewe kuliko wanyama wote, na kuliko hayawani wote walioko Mwituni; kwa tumbo utakwenda, na mavumbi utakula siku zote za maisha yako; nami nitaweka uadui kati yako na huyo mwanamke, na kati ya uzao wako na uzao wake; huo utakuponda kichwa nawe utamponda kisigino.

UADUI GANI ULITANGAZWA.

Ø    Bila shaka huu ni uadui kati ya nyoka ( Ibilisi ) na kanisa la Mungu (MWanamke.)

NI MBINU GANI ATUMIAYO SHETANI KATIKA VITA BAINA YAKE NA KANISA LA MUNGU?

Ø    KItabu cha Ufunuo wa Yohana kinatupa picha zaidi kuhusu nyoka na mbinu atumiayo kushinda vita.

NI UDANGANYIFU / UONGO
Ø    Ufunuo 3:9. Yule joka akatupwa, nyoka wa zamani ,aitwae Ibilisi na Shetani, audanganyae ulimwengu wote; akatupwa hata nchi, na malaika zake wakatupwa pamoja nae.

Ø    Kanuni kuu aitumiayo shetani ni kudanganya, yani kila jambo aliloagiza Mungu yeye huwashawishi wanadamu kutenda kinyume, pale Edeni Mungu aliwaambia Adam na Hawa  wasile tunda la ujuzi wa mema na Mabaya shetani yeye akawaambia wale hatimaye walipo kula kwa njia hiyo shetani akapata ushindi wa mda mfupi.

KATIKA BIBLIA MWANAMKE HUWAKILISHA NINI?

Ø    Waefeso 5:22,23. Enyi wake, watiini waume zenu kama kumtii Bwana wetu. Kwa maana Mume ni kichwa cha mkewe, kama Kristo naye ni kichwa cha kanisa; naye ni mwokozi wa mwili.


Ø    Kwahiyo hii ni vita baina ya shetani na kanisa la Mungu, kwa kuwa Mpaka kiipindi hiki kanisa la Mungu lilisha ingia katika laana ya dhambi kwa kukutwa na kifo Mungu alitengeneza mpango wa kuweza kumponda shetani kwa kuleta Mkombozi ambaye katika Mwanzo 3:15 ametajwa kama uzao wa mwanamke.


Ø    Ufunuo 12:11, Nao wakamshinda kwa kwa Damu ya Mwana- Kondoo, na kwa neno la ushuhuda wao; ambao hawakupenda maisha yao hata kufa.


Ø    Sheria ya Mungu iliyovunjwas pale edeni ni takatifu kama Mungu aliyeitoa kwa hiyo kiumbe kilichopaswa kuja kufanya ukombozi ni lazima kiwe na hali ya Uungu, ndiyo maana mungu alimtuma Yesu kuja kufanya ukombozi hakutuma viumbe wengine walioko mbinguni kama vile malaika.


Ø    Mungu ameliahidi kanisa lake kumshinda Ibilisi kwanza kwa  DAMU YA MWANA KONDOO  , halafu  na kwa NENO LA USHUHUDA WAO.


Ø    Ni kupitia kifo cha Yesu pale msalabani, mwanadamu anapomwamini Yeye na kupmpokea anajiweka katika mpango wa kurejeshewa uzima wa milele hapa ndipo Mwananamu au wanadamu wanaounda kanisa la Mungu wanamshinda Ibilisi kwa DAMU YA MWANAKONDOO ..


Ø    Yohana 3;16. Kwa maana jinsi hii Mungu alliupenda ulimwengu, hata akamtoa Mwanawe pekee, ili kila mtu amwaminiye asipotee, bali awe na uzima wa milele.     


Ø    Yesu ni mwanakondoo aliyemwaga damu kwa ajili ya ukombozi wa ulimwengu wote.


Ø    Yohana 1:36. Akamtazama Yesu akitembea, akasema, Tazama Mwana-konoo wa Mungu.

NENO LA USHUHUDA WAO

Ø     Ufunuo 12:11 imetaja kitu kingine kinachofanya kanisa la Mungu kumshinda Ibilisi nacho ni NENO LA USHUHUDA WAO , tena fungu la mbele limeenda mbali zaidi


Ø     Ufunuo 12:17.Joka akamkasirikia yule mwanamke, akaenda zake afanye vita juu ya wazao wake waliosalia, wazishikao Amri za Mungu, na kuwa na ushuhuda wa Yesu.


Ø     Ushuda wao, au ushuhuda wa Yesu ni Maandiko matakatifu ( Biblia) kwasababu hiyo ndiyo imuonyeshayo mwanadamu yeyote ukombozi.Wanadamu wanateseka tu kwasababu hawajamjua Yesu, wanadamu hawajamjua Yesu kwasababu hawayajayajua maandiko eidha kwa kuyasoma au kufundishwa.


Ø    Akiongea na mafurisayo ambao walikuwa wachunguzaji wazuri sana wa maandiko Yesu alisema maneno yafuatayo.


Ø    Yohana  5:39. Mwayachunguza maandiko , kwasababu mnadhani ninyi mna uzima wa milele ndani yake; na hayo ndiyo yanayonishuhudia.


Ø    Hata Nabii Yohana katika kitabu ncha ufunuo alifunuliwa zaidi na mjumbe kutoka Mbunguni kuhusu maana ushuhuda wa Yesu


Ø    Ufunuo 19:10, Nami nikaanguka mbele ya miguu yake, ili nimsujudu; akaniambia, angalia ,usifanye hivi; mimi ni mjoli wako na wa ndugu zako walio na ushuhuda wa Yesu. Msujudie  Mungu. Kwa maana ushuhuda wa Yesu ndio Roho ya unabii.



POTE KATIKA BIBLIA TOKEA MWANZO MPAKA UFUNUO MAANDIKO MATAKATIFU HUMSHUUDIA YESU AMBAYE KWA KIFO CHAKE ALIMPONDA SHETANI KICHWA NA  KUFUMBUA FUMBO LA MAUTI

Ø    Jambo baya na la kusikitisha zaidi ni mbinu atumiayo shetani  ambayo ni kufundisha maandiko nusunusu, hawafundishi wanadamu kuzishika amari za Mungu kwasababu Uadui wake upo dhidi ya kanisa lizishikazo amri za Mungu na kuwa na Imani ya Yesui.


Ø    Waweza kudhani kwamba mtu yeyote ashikae Biblia na kuhubiri ni mtumishi wa Mungu la hasha, hata shetani hutumia biblia lakini jhutumia vifungu vya bibilia kutetea hoja zake na siyo Biblia nzima ionyeshe uhalisia wa hoja mbali mbali.


Ø    Watumishi wa Mungu hutumia Mafungu na vitabu vya kutosha katika biblia ili kuonyesha msimamo wa maandiko kuhusiana na hoja mbalimbali badala ya kujetretea kwa kusimamia kifungu kimoja tu cha biblia.
 

 
KITAMBULISHO CHA  KANISA LA  MUNGU LINALOCHUKIWA NA SHETANI NI LILE LISHIKALO AMRI ZOTE KUMI ZA MUNGU NA KUWA NA IMANI YA YESU
Ø   Je wew ni miongoni kanisa la mungu lizishikazo amri kumi za mingu?
Ø   Je unasoma maandiko ili upate kujua mbinu za shetani katika vita hii ili umshinde?
Ø   Ili kuzijua amri kumi za Mungu soma Kutoka 20.Mungu akubariki.
Ø   Kwa ukweli zaidi tembelea kanisa lolote la WAADVENTISTA WASABATO LILILOPO JIRANI NA MAHALI UISHIPO.

Endelea kutembelea blog yetu upate kujua mengi zaidi…

Silaha kubwa ya vita ya shetani kuwaongoza wanadam kuvunja eidha
amri moja au zaidi katika amri kumi za Mungu.

VAZI AMBALO MUNGU ALIMVIKA MWANADAM.

Mavazi ya Kikristo.
By Petro Tumaini.

    Watu wengi hudhani kwamba biblia haijawa wazi hususani tunapozuingumzia suala la Mavazi, lakini Miongoni ya mambo aliyo yashughulikia mungu mwenywe  likiwamo na na ukombozi wa Mwanadam ni kutengeneza na kuwavika mavazi ya kusetiri mwili adam na Hawa.

Adam na Eva Walijitrambua kuwa wako nuchi, wakajitengenezea Mavazi.

Ø    Mwanzo  3:7. Wakafumbuliwa macho wote wawili wakajiona kuwa wa uchi, wakashona majani ya mtini, wakajifanyia nguo.

    Ni wazi kwamba  utukufu wa Mungu uliowafunika Adam na Eva kabla ya dhambi lakini mara tu baada ya kukubali kula tunda la ujuzi wa mea na mabaya alilowakataza Mungu utukufu wa mungu uliwaacha na wakaanza kujisikia aibu kuwa wako uchi wakajitengenezea majani ya mtini ambayo Mungu hakuridhika nayo na kuamua kuwatengenezea vazi yeye mwenyewe.

Ø    Mwanzo 3:21. Bwana Mungu akawafanyia Adam na mkewe mavazi ya ngozi akawavika.

     Vazi alilowatengenezea Mungu lilikuwa ni ngozi ya kondoo, liliwakilisha Utukufu wa Yesu ambao unatufunika uchi wa dhambi zetu.Mungu aliwavika ngozi kwasababu vazi la majani ya mtini waliyojitengenezea hayakusitiri uchi wao.

“Kitendo cha Mungu kuwatengenezea vazi na kuwavika Adam na Eva kinaashiria namna Mungu anavyozingatia sana umuhimu wa mavazi kwa wafuasi wake.”

    Neno la kiebrania lizungumzialo vazi alilotengeneza mungu kwa kutumia ngozi ya kondoo limejengwa kaytika mzizi wa neno ktnvt ambalo humaanisha (to cover), yaani kusitiri au kufunika.
 
    Katika biblia ya kiingereza limetumika vizuri zaidi, limeitwa (tunics), ambalo lilmetokana na neno la kilatini tunicas.

    Tunics ni mavazi yaliyovaliwa na wtu wa Mungu tokea agano la kale, yalikuwa ni mavazi marefu yanayofunika mikono , mwili na kufuka chini ya magoti.


     Waweza kusema Mungu anaangalia moyo na si mavazi kwahiyo hata nikivaa vazi lisilositiri ni sawa maana moyo wangu utabaki kuwa msafi,  neno ambalo limekuwa likisemwa na wengi wanaotetea uvaajio wa nguo za kihuni.  Biblia inasema Mungu anataka tuwe safi ndani na nje, yani wasafi wa moyo na mwili pia.

Ø    I Wathesolanike 5:23. Mungu wa amani mwenyewe awatakase kabisa: na miili yenu muhifadhiwe muwe kamili, bila lawama, wakati wa kuja kwake Bwana wetu yesu krist.

   Mwanadamu huona nje, aonaye ndani ya moyo ni mungu peke yake, hata hivyo waweza ukawa msafi nje lakini moyoni ukawa mchafu, lakini huwezi ukawa msafi ndani halafu nje ukwa mchafu. Huwezi kutembea nusu uchi halafu wanadami wakadhania kuwa moyo wako ni msafi.

“Waweza ukawa samba aliyejivija ngozi ya kondoo, lakini huwezi kuwa kondoo halafu ukavaa ngozi ya samba.”

    Tokea dhambi iingie mungu hakupenda mwanadam atembee bila kuusitiri mwili wake, hata makuhani waliohudumu hekaluni alitaka wasogee mbele zake wakiwa wamesitiri miili yao.


Ø    Kutoka 20:26. Tena hutapanda kwenda madhabahuni kwangu kwa daraja, uchi wako usidhihirike juu yake.

Itaendelea, endelea kutendembelea blog yetu…