Waweza Kuishi na Yesu, lakini huwezi kuishi bila Yesu.Yohan 3:16


TWAWEZA KUIAMINI BIBLIA
Mabaharia waasi maarufu walioizamisha meli ya Kiingereza iliyoitwa Bounty waliishia kufanya makazi yao wakiwa pamoja na wanawake, wenyeji wa eneo lile katika kisiwa cha Pitcairn katika Bahari ya Pasifiki ya Kusini. Kundi lile lilikuwa mabaharia tisa wa Kiingereza, wanaume wa Kitahiti sita, wanawake wa Kitahiti kumi, na msichana wa miaka kumi na mitano. Mmojawapo wa mabaharia wale alivumbua namna ya kutonesha [kugeuza kuwa mvuke] alkoholi, na baada ya muda mfupi ulevi ukaliharibu koloni lile lililokuwa katika kisiwa kile. Ugomvi kati ya wanaume na wanawake ukageuka na kuwa wa kutumia nguvu.
Baada ya kupita muda fulani mmoja tu kati ya wanaume wale wa kwanza waliofika mle kisiwani ndiye alibaki kuwa hai. Lakini mtu huyo, Alexander Smith, alikuwa ameigundua Biblia katika mojawapo la makasha yaliyochukuliwa kutoka katika ile meli. Alianza kuisoma na kuwafundisha wengine juu ya kile ilichosema. Alipofanya hivyo maisha yake yeye mwenyewe yakabadilika na hatimaye maisha ya wote waliokuwa katika kisiwa kile.
Wakazi wa kisiwa kile walikuwa wametengwa na ulimwengu wa nje mpaka ilipowasili meli ya Kimarekani iliyoitwa Topaz katika mwaka wa 1808. Wafanyakazi katika meli hiyo wakakikuta kisiwa kile kikiwa na jumuia inayokua na kusitawi, bila ya kuwa na pombe kali (wiski), gereza, wala uhalifu. Biblia ilikuwa imekigeuza kisiwa kile kutoka jehanamu ya duniani kwenda katika kielelezo cha vile Mungu atakavyo ulimwengu huu uwe. Na mpaka leo hii kinaendelea kuwa katika hali hiyo.
Je, hivi Mungu bado anaendelea kusema na watu kupitia katika kurasa hizo za Biblia? Bila shaka anafanya hivyo. Ninapoandika haya, naliangalia karatasi la majibu lililotumwa kwetu na mwanafunzi mmojawapo wa kozi zetu za Biblia. Maelezo chini yake yanasema hivi "Mimi nimo gerezani, niko katika orodha ya watu wanaostahili kunyongwa, nimehukumiwa kufa kwa kutenda kosa la jinai. Kabla ya kuchukua kozi hii ya Biblia, nilikuwa nimepotea lakini sasa ninacho kitu cha kutumainia tena nimeupata upendo mpya."
Biblia inao uwezo unaoweza kuyabadilisha kabisa maisha ya watu. Kwa kweli, watu wanapoanza kujifunza Biblia, maisha yao hubadilika kwa namna ya kuvutia sana.

1. Jinsi Mungu Anavyozungumza Nasi Kupitia Katika Biblia

Baada ya kumwumba Adamu na Hawa, yaani, yule mwanaume na mwanamke wa kwanza wa duniani, Mungu alizungumza nao uso kwa uso. Lakini Mungu alipokuja kuwatembelea baada ya wao kutenda dhambi, je, wale watu wawili walifanya nini?
"Mwanaume yule na mkewe wakasikia sauti ya BWANA Mungu alipokuwa akitembea mle bustanini wakati wa jua kupunga, nao WAKAJIFICHA ASIWAONE BWANA MUNGU katikati ya miti ya bustani." (Mwanza 3:8). 
Dhambi ilikata mawasiliano ya ana kwa ana kati ya mwanadamu na Mungu. Baada ya dhambi kuingia katika ulimwengu huu, je, Mungu aliwasilianaje na watu?
"Hakika Bwana Mwenyezi hafanyi kitu, bila kuwafunulia watumishi wake manabii nia yake." - Amosi 3:7.
Mungu hakutuacha sisi gizani kuhusu maisha haya tuliyo nayo na maana yake. Kupitia kwa manabii wake - yaani, watu wale aliowaita Mungu kuwa wanenaji na waandishi wake - wamefunua majibu yake kwa maswali makuu yahusuyo maisha yetu.

2. Ni Nani Aliyeiandika Biblia?

Manabii waliutoa ujumbe wa Mungu kwa kutumia sauti na kalamu zao katika kipindi chao walichoishi, na walipokufa, maandiko yao yaliendelea kuwapo baada yao. Kisha ujumbe huo wa manabii ulikusanywa pamoja chini ya uongozi wake Mungu, na kuwekwa katika kitabu tunachokiita Biblia.
Lakini maandiko yao hayo yanaaminika kwa kiasi gani?
"Zaidi ya hayo, lakini kumbukeni kwamba hakuna mtu ye yote awezaye kufafanua mwenyewe unabii ulio katika Maandiko Matakatifu. Maana hakuna ujumbe wa kiunabii unaotokana na matakwa ya binadamu bali watu walitoa unabii wakiongozwa na Roho Mtakatifu" (2 Petro 1:20,21).
Waandishi wa Biblia waliandika si kwa kufuata mapenzi au tamaa yao, bali kama walivyoongozwa au kuvuviwa na Roho wa Mungu. Biblia ni kitabu cha Mungu!
Katika Biblia hiyo Mungu hutuambia habari zake Mwenyewe, tena hutufunulia makusudi yake aliyo nayo kwa ajili ya wanadamu. Inaonyesha mtazamo wa Mungu kwa mambo yale yaliyopita, kisha inatufunulia mambo ya mbele, ikitueleza jinsi tatizo la uovu litakavyotatuliwa mwishoni na jinsi amani itakavyokuja katika dunia yetu.
Je, hivi Biblia yote ni ujumbe utokao kwa Mungu?
"Maandiko yote, Matakatifu yameandikwa kwa uongozi wa Mungu, na yanafaa kuonya, kusahihisha makosa yao, na kuwaongoza, katika kufundishia ukweli, mtu wa Mungu awe mkamilifu na tayari kabisa kufanya kila kazi njema, waishi maisha adilifu" - (2 Timotheo 3:16,17).
Biblia Takatifu huyabadilisha kabisa maisha ya wanadamu kwa sababu Biblia "yote" ina "pumzi ya Mungu," ni hati iliyovuviwa, ni kitabu cha Mungu. Manabii walisimulia kile walichokiona na kukisikia kwa kutumia lugha ya wanadamu, lakini ujumbe wao ulitoka moja kwa moja kwa Mungu. Kwa hiyo, ukitaka kujua maisha haya yana maana gani, soma Maandiko Matakatifu. Kuisoma Biblia kutayabadilisha kabisa maisha yako. Kadiri unavyozidi kuisoma kwa maombi, ndivyo utakavyozidi kupata amani moyoni mwako.
Roho Mtakatifu yule yule aliyewavuvia manabii kuandika, Biblia hiyo, atayafanya mafundisho ya Biblia, injili yake, ifae kuyabadilisha kabisa maisha yako ukimwalika Roho kuwapo wakati unapoisoma hiyo Biblia.

3. Umoja wa Biblia

Kwa kweli Biblia ni maktaba ya vitabu 66. vitabu 39 vya Agano la Kale viliandikwa kuanzia karibu na mwaka wa 1450 K.K hadi 400 K.K, Vitabu 27 vya Agano Jipya viliandikwa kati ya mwaka wa 50 B.K na mwaka wa 100 B.K.
Nabii Musa alianza kuandika vitabu vitano vya kwanza wakati fulani kabla ya mwaka wa 1400 K.K. Mtume Yohana alikiandika kitabu cha mwisho cha Biblia, yaani, kitabu cha Ufunuo, karibu na mwaka wa 95 B.K. Katika kipindi cha miaka 1,500 kati ya kuandikwa kitabu cha kwanza na cha mwisho cha Biblia, walau watu wengine wapatao 38 waliovuviwa walitoa mchango wao. Wengine walikuwa wafanya biashara, wengine wachungaji wa kondoo, wengine wavuvi, wengine askari, matabibu, wahubiri, wafalme - wanadamu toka katika tabaka zote za maisha. Mara nyingi waliishi katika utamaduni na falsafa vilivyohitilafiana.
Lakini hapa ndipo yalipo maajabu ya maajabu yote: Vitabu hivyo 66 vya Biblia pamoja na sura zake 1,189 zenye idadi ya mafungu 31,173 vikiwekwa pamoja, tunaona umoja na mwafaka katika ujumbe vinaoutoa.
Hebu na tuseme kwamba mtu mmoja anagonga mlangoni pako, halafu anapokaribishwa ndani, anaweka kipande cha marumaru chenye umbo la ajabu juu ya sakafu ya chumba chako cha kuongea, halafu anaondoka bila kusema neno lo lote. Wageni wengine wanamfuata, mmoja baada ya mwingine, mpaka takribani watu 40 wanaweka kila mmoja kipande chake cha marumaru mahali pake.
Wa mwisho anapokwenda zake, kwa mshangao wewe unaona jengo zuri limesimama mbele yako. Ndipo wewe unajifunza kwamba sehemu kubwa ya "mafundi hao wanachonga mawe" hawajawahi kuonana kamwe, wakiwa wamekuja, kama walivyofanya, kutoka Amerika ya Kusini, China, Urusi, Afrika na sehemu nyingine za ulimwengu.
Je, wewe ungeamua nini? Ya kwamba mtu fulani alipanga umbo hilo lililojengwa kwa mawe ya kuchonga naye alimtumia kila mtu vipimo sahihi kutokana na kipande chake kile kimoja cha marumaru.
Biblia nzima inatoa ujumbe mmoja unaoshikamana - sawasawa tu na lile jengo la mawe yaliyochongwa ya marumaru. Mtu fulani mmoja mwenye akili alipanga yote hayo, yaani, ni akili za Mungu. Umoja wa kushangaza wa Maandiko Matakatifu unatoa ushahidi wake kwamba ingawa ni wanadamu walioyaandika mawazo yale, yalikuwa yamevuviwa naMungu.

4. Waweza Kuiamini Biblia

1. Kuhifadhiwa kwa Biblia ni jambo la ajabu sana. Maandiko yote ya awali ya Biblia yalinukuliwa kwa mkono - muda mrefu kabla ya kuwako
mitambo ya kuchapisha vitabu. Waandishi wale walitayarisha nakala za maandiko ya mkono ya asilia na kuzitawanya. Maelfu ya nakala kama hizo za maandiko ya mkono au sehemu zake bado ziko mpaka sasa.
Maandiko ya mkono ya Kiebrania yanayorudi nyuma hadi ule mwaka wa 150 mpaka 200 kabla ya Kristo yalipatikana karibu na Bahari ya Chumvi mnamo mwaka 1947. Ni jambo la kushangaza sana kwamba magombo hayo mawili yenye umri wa miaka elfu mbili yanazo kweli zile zile tunazozikuta katika Agano la Kale la Biblia zinazochapishwa siku hizi. Huu ni ushahidi wenye nguvu unaoonyesha jinsi Neno la Mungu linavyoaminika.
Mitume waliandika kwanza sehemu kubwa ya Agano Jipya kama nyaraka walizozituma kwa makanisa ya Kikristo yaliyoanzishwa baada ya kifo na ufufuo wake Kristo. Zaidi ya maandiko ya mkono 4,500 ya Agano Jipya lote au sehemu yake yanapatikana katika nyumba za Makumbusho na maktaba za Ulaya na Amerika. Baadhi yake yanakwenda nyuma hadi karne ile ya pili. Kuyalinganisha maandiko hayo ya mkono ya awali na biblia ya siku hizi, twaweza kuona kwa urahisi kwamba kwa kawaida Agano Jipya limeendelea pia kubaki bila mabadiliko yo yote tangu lilipoandikwa kwa mara ya kwanza.
Siku hizi Biblia au sehemu zake zimetafsiriwa katika lugha zaidi ya 2,060 na (dialects). Ni kitabu kinachouzwa sana ulimwengu: zaidi ya Biblia milioni 150 na sehemu za Biblia huuzwa kila mwaka.
2. Usahihi wa Biblia kihistoria ni wa kushangaza sana. Uvumbuzi mwingi wa elimu ya mambo ya kale (akiolojia) umethibitisha kwa namna ya kuvutia sana usahihi wa Biblia. Wanahistoria wamevigundua vibao vya udongo wa mfinyanzi pamoja na majengo ya kumbukumbu ya mawe ambayo yameonyesha majina, mahali, na matukio yaliyojulikana kuhusu siku za nyuma kutokana na Biblia tu.
Kwa mfano, kulingana na Mwanzo 11:31, Ibrahimu na familia yake "wakatoka wote katika Uru... waende katika nchi ya Kanaani." Kwa kuwa ni Biblia peke yake iliyosema juu ya Uru, mabingwa fulani wa Biblia walisema kwamba mji kama huo ulikuwa haujapata kuwako kamwe. Ndipo wachimbaji wa mambo ya kale wakagundua mnara wa hekalu katika nchi ya Iraki Kusini ukiwa na kwenye msingi wake iliyoandikwa katika maandishi ya kikabari yaliyokuwa na jina la Uru. Ugunduzi wa baadaye ulionyesha kwamba Uru ulikuwa ni mji mkuu ambao ulikuwa unasitawi wenye ustaarabu wa hali ya juu uliokuwa umefikiwa. Sura ya mji ule ilikuwa imesahaulika ni Biblia peke yake iliyolihifadhi jina lake - mpaka pale koleo ya mwanaakiolojia mmoja ilipouthibitisha ukweli wa kuwako kwake. Na huo Uru ni mmoja tu miongoni mwa mifano mingi ya akiolojia inavyothibitisha usahihi wa Biblia.
3. Kutimia kwa usahihi kabisa kwa utabiri wa Biblia hukuonyesha wewe kwamba unaweza kuitegemea Biblia. Maandiko hayo yana utabiri mwingi wa kushangaza sana wa matukio ya siku za usomi ambayo hivi sasa yanaendelea kutimia mbele ya macho yetu. Tutauchunguza baadhi ya unabii huo wa kusisimua katika masomo ya mbele.

5. Jinsi Ya Kuielewa Biblia

Unapolichunguza Neno la Mungu, weka kanuni hizi mawazoni mwako:
1. Jifunze Biblia ukiwa na moyo wa maombi. Ukiyaendea Maandiko Matakatifu kwa moyo na mawazo yaliyofunguliwa kwa maombi, yatageuka na kuwa mawasiliano kati yako na Yesu (Yohana 16:13-14).
2. Soma Biblia kila siku. Kujifunza Biblia kila siku ni ufunguo wa kupata nguvu katika maisha yetu, ni kukutana na mawazo ya Mungu (Warumi 1:16).
3. Unapoisoma, iache Biblia ijieleze yenyewe. Uliza: mwandishi huyu wa Biblia alikusudia kusema nini? Kwa kuzingatia kile limaanishacho fungu hilo, twaweza kuitumia kwa akili katika maisha yetu ya leo hii.
4. Soma Biblia kwa kufuata somo. Linganisha andiko na andiko. Yesu alitumia mbinu hii kuthibitisha kwamba yeye alikuwa ndiye Masihi:
"Akaanza kutoka Musa na Manabii wote, akawaeleza katika maandiko yote mambo yaliyomhusu yeye mwenyewe."
5. Jifunze Biblia ili kupokea uwezo wa kuishi kwa ajili ya Kristo. Neno la Mungu limeelezwa katika Waebrania 4:12 kama upanga mkali ukatao kuwili. Ni zaidi ya maneno tu yaliyo juu ya ukurasa, ni silaha iliyo hai mikononi mwetu ya kupigia na kuyaondolea mbali majaribu yale yanayotushawishi kutenda dhambi.
6. Sikiliza Mungu anapozungumza nawe kupitia katika Neno lake. Endapo mtu anataka kuujua ukweli wa Bilbia juu ya somo fulani, basi, ni lazima awe tayari kufuata yale inayofundisha (Yohana 7:17), sio yale anayofikiri mtu fulani, au yale yanayokaziwa na fundisho lolote la kanisa lake.

6. Biblia Yaweza Kubadilisha Maisha Yako

"Kuyafafanua maneno yako [Mungu] kwatia nuru, kunampa ufahamu mjinga" - (Zaburi 119:130).
Kujifunza Biblia kutauimarisha "ufahamu" wako, kutakupa nguvu ya kuyashinda mazoea yale yaletayo madhara, na kukuwezesha kukua kimwili, kiakili, kimaadili na kiroho.
Biblia inazungumza na moyo. Inashughulika na mambo yale yanayowapata wanadamu katika maisha yao - yaani, upendo, ndoa, uzazi na kifo. Inaliponya jeraha lenye kina kirefu sana katika tabia ya mwanadamu, pamoja na dhambi na taabu inayotokana nayo.
Neno la Mungu si kitabu cha jamii moja, kizazi kimoja, taifa moja, au utamaduni mmoja. Japokuwa liliandikwa katika nchi ya Masharikiya kati, linawavutia pia wanaume na wanawake wa Magharibi. Linaingia katika nyumba za wanyonge na katika majumba makubwa ya matajiri. Watoto wanazipenda hadithi zake zinazosisimua. Mashujaa wake wanawavutia sana vijana. Wagonjwa, wanaoishi katika hali ya upweke, na wazee wanagundua ndani yake faraja na tumaini la kuwa na maisha bora.
Kwa kuwa Mungu anafanya kazi yake kupitia katika Biblia, basi, inao uwezo mkubwa. Inaivunjavunja hata mioyo iliyofanywa migumu dhidi ya hisia zote za kibinadamu, inailainisha na kuijaza na upendo. Tumeona Biblia ikimbadilisha haramia wa zamani na mvuta bangi na kumfanya mhubiri aliye motomoto. Tumeona Biblia ikimbadilisha mwongo na mdanganyaji na kumfanya kuwa mwalimu mwaminifu na mwenye kuheshimika. Tumeona kitabu hicho kikiwanyakua watu wakiwa karibu na kujiua wenyewe na kuwapa tumaini la kuanza maisha upya. Biblia inaamsha upendo miongoni mwa maadui. Inawafanya wenye majivuno kuwa wanyenyekevu, na wachoyo kuwa wakarimu. Biblia inatutia nguvu tunapokuwa dhaifu, inatuchangamsha tunapokuwa katika hali ya kukata tamaa, inatufariji tunapokuwa na huzuni, inatuongoza tunapochoka sana. Inatuonyesha jinsi ya kuishi kwa ujasiri na jinsi ya kufa bila hofu.
Kitabu hicho cha Mungu, yaani, Biblia kinaweza kuyabadilisha maisha yako! Utagundua hivyo kwa dhahiri zaidi na zaidi, kadiri unavyoendelea kujifunza miongozo hii ya GUNDUA.
Kwa nini Biblia hiyo iliandikwa kwa ajili yetu? Yesu anatoa jibu: "Lakini hizi [kweli za Biblia] zimeandikwa; ili mpate kuamini ya kwamba Yesu ndiye Kristo, Mwana wa Mungu; na kwa kuamini muwe na uzima kwa jina lake" - (Yohana 20:31).
Sababu kuu kuliko zote kwa nini sisi tunapaswa kuyafahamu Maandiko Matakatifu ni kwamba yamejaa picha zinazomfunua Yesu Kristo na kutuhakikishia sisi uzima wa milele. Kwa kumtazama Kristo katika Biblia nzima, tunabadilika na kufanana naye zaidi. Basi, kwa nini wewe usianze sasa kugundua uwezo huo wa Neno la Mungu uwezao kukufanya wewe kufanana zaidi na Yesu?

YACHUNGUZENI MAANDIKO

TWAWEZA KUMWAMINI MUNGU
Siku moja Jimi alimwuliza mtu mmoja anayekana kuwa kuna Mungu endapo alipata kujaribu sana, hata kwa dakika chache tu, kupigana na wazo lisemalo kwamba huenda Mungu yuko.
"Sawa kabisa!" mkana Mungu yule akajibu, akimwacha Jimi na mshangao. "Miaka mingi iliyopita, mimi nilikuwa karibu sana nigeuke na kuwa mtu anayemwamini Mungu. Nilipokiangalia kile kiumbe kidogo sana - lakini - kikamilifu katika kitanda chake kidogo, nilipochungulia na kuviona vidole vile vidogo fahamu za kwanza za kutambua, nilipita katika kipindi cha miezi kadhaa ambayo katika hiyo mimi nilikuwa karibu kabisa niache kuwa mkana Mungu. Kule kumwangalia mtoto yule kulikuwa kumenishawishi karibu kabisa kuwa hapana budi Mungu alikuwa yuko."
1. Kila Kitu Kilichobuniwa Kina Mbunifu Wake
Muundo wa mwili wa kibinadamu unafanya iwepo haja ya kuwako mbunifu wake. Wanasayansi wanatuambia kwamba ubongo wetu hukusanya na kukumbuka picha elfu nyingi katika mawazo yetu, huyaunganisha matatizo yetu yote na kuyatatua, hufurahia kuona uzuri, huitambua nafasi ya mtu, na kutaka kukuza yaliyo bora ndani ya kila mtu. Chaji za umeme zitokazo katika ubongo huongoza shughuli zote za misuli ya miili yetu.
Kompyuta pia zinafanya kazi kwa njia ya mikondo ya umeme. Lakini ilichukua akili ya mwanadamu katika kuitengeneza hiyo kompyuta na kuiambia la kufanya.
Si ajabu, basi, kwamba mtunzi wa Zaburi alihitimisha kwa kusema kwamba mwili wa mwanadamu unasimulia habari za Muumbaji huyo wa ajabu kwa sauti kubwa iliyo wazi:
"Nakusifu maana nimefanywa kwa namna ya ajabu, matendo yako ni ya ajabu, wewe wanijua kabisa kabisa" - (Zaburi 139:14)

Hatuna haja ya kwenda mbali ili kuyaona hayo "matendo" ya Mungu. Umbo la ubongo wetu wenye sehemu nyingi za ajabu na viungo vyetu vingine ni "matendo" ya Mungu, nayo husonda kidole chake kwa yule mbunifu stadi kabisa.
Hakuna pampu yoyote iliyotengenezwa na mwanadamu inayoweza kulinganishwa na moyo wa mwanadamu. Hakuna mtandao wo wote wa kompyuta uwezao kuwa sawa na mfumo wetu wa mishipa ya fahamu. Hakuna mfumo wo wote wa Televisheni unaofanya kazi yake vizuri kama sauti, sikio, na jicho la mwanadamu. Hakuna kiyoyozi kikuu cho chote (central air conditioning) wala mfumo wa kuipasha joto nyumba uwezao kushindana na kazi inayofanywa na pua, mapafu, na ngozi yetu. Mfumo wenye sehemu nyingi za ajabu wa mwili wa mwanadamu unadokeza kwamba mtu fulani alihusika katika kuubuni, na Mtu huyo fulani ni Mungu.
Mwili wa mwanadamu ni mfumo kamili wa viungo mbali mbali - vyote vikiwa vinashirikiana, vyote vikiwa vimeumbwa kikamifu. Mapafu na moyo, mishipa ya fahamu na misuli, hiyo yote hufanya kazi za ajabu mno kiasi cha kuwa vigumu kusadikika ambazo hutegemezwa juu ya kazi nyingine zilizo za ajabu mno kiasi cha kutufanya sisi tushindwe kusadiki.
Endapo ungetakiwa kuzipa nambari sarafu kumi kuanzia moja mpaka kumi, na kuziweka mfukoni mwako, na kuzitikisa-tikisa huku na huku, kisha kuzitoa mfukoni mwako na kuziweka tena mfukoni moja moja, je, kuna uwezekano gani kwamba ungefanya hivyo kwa kufuata mfuatano wa nambari zake sawa sawa? Kwa sheria ya mahesabu unayo bahati moja tu katika bilioni kumi ya kuzitoa kwa mpangilio wake kuanzia ya kwanza mpaka ile ya kumi.
Sasa, basi, hebu fikiria ni bahati ngapi tumbo la chakula, ubongo, moyo, ini, arteri, vena, figo, masikio, macho, na meno vingekuwa nazo vikikua vyote pamoja na kuanza kufanya kazi yao kwa dakika ile ile ya wakati mmoja.
Hivi maelezo ya busara kabisa ni yapi kuhusu ubunifu huo wa mwili wa mwanadamu?
"Kisha Mungu akasema, 'Natumfanye mtu kwa mfano wetu, kwa sura yetu,'..............Hivyo Mungu Akamwuumba Mtu Kwa Mfano Wake,...... mwanamume na mwanamke aliwaumba" - (Mwanzo 1:26,27).
Mwanaume na mwanamke wa kwanza wasingeweza kuwa wametokea wenyewe tu. Biblia inathibisha kwamba Mungu alitubuni sisi kwa mfano wake. Alituwaza katika mawazo yake na kutuumba.
2. Kila Kitu Kilichoumbwa Kina Muumbaji Wake
Lakini ushahidi wa kuwako kwake Mungu haufungamani tu na ubunifu wa miili yetu; pia umetandaa huko mbinguni. Acha taa za mjini, angalia juu katika mbingu ya usiku. Wingu lile jeupe kama maziwa lenye nyota, tunaloliita Mkanda wa Nuru (Milky Way) ambalo kwa kweli ni kundi la mabilioni ya majua (galaxy) yanayotoa mwanga mkali wa moto sawa na ule wa jua letu ambao unaweza kuonekana hapa duniani kwa kupitia katika darubini kubwa zilizopo hapa duniani kama ile darubini iitwayo "Hubble Telescope" iliyo katika anga za juu.
Si ajabu, basi, kwamba mtunga Zaburi alihitimisha kwa kusema kwamba nyota zinamtangaza Muumbaji Mtukufu:
"Mbingu zatangaza utukufu wa Mungu, anga ladhihirisha kazi ya mikono yake" (Zaburi 19:1-3).
Je, hivi sisi twaweza kutoa hitimisho gani la busara kwa kuangalia mpangilio huo unaotatanisha sana na ukubwa wa malimwengu yote?
"Hapo mwanzo Mungu aliziumba mbingu na nchi" (Mwanzo 1:1).
"Yeye [Mungu] alikuwako kabla ya vitu vyote; vyote hudumu mahali pale kwa uwezo wake" (Wakolosai 1:17).
Viumbe vyote humshuhudia yule Mungu Mbunifu Mkuu na Muumbaji asiye na Mwisho. Katika maneno haya rahisi, "Hapo mwanzo Mungu," tunalipata jibu la siri ile ya uhai. Yuko Mungu aliyeumba kila kitu.
Wanasayansi wakuu wengi siku hizi wanamwamini Mungu. Dk. Arthur Compton, mwanafizikia mshindi wa tuzo ya Nobel, akitoa maoni yake juu ya fungu hilo la Maandiko, siku moja alisema hivi:
"Kwangu binafsi, imani huanza ninapotambua kwamba yule aliye na akili isiyo na kifani ndiye aliyeyaweka hayo malimwengu na kumwumba mwanadamu. Kwangu mimi si vigumu kuwa na imani hii, kwa maana ni dhahiri kwamba po pote pale palipo na mpango yupo Mungu mwenye akili. Malimwengu yaendayo kwa utaratibu, na kujifunua kwetu hushuhudia ukweli wa usemi huu adimu mno uliopata kunenwa - 'Hapo mwanzo Mungu'"
Biblia haijaribu kumthibitisha Mungu inatangaza kuwako kwake. Dk. Arthur Conklin, mwana biolojia, siku moja aliandika hivi: "uwezekano kwa uhai kutokea kwa ajali ni sawa na uwezekano kwa kamusi kamili kutokea kutokana na mlipuko katika kiwanda cha kuchapisha vitabu".
Twajua kwamba wanadamu hawawezi kutengeneza kitu cho chote bila kutumia kitu kingine. Twaweza kujenga vitu, kuvumbua vitu, kuunganisha vitu, lakini kamwe hatujapata kufanya kitu cho chote bila kuwa na kitu kingine cha kuanzia, awe ni chura mdogo kabisa ua la kawaida kabisa. Vitu vituzungukavyo pande zote hupiga kelele vikisema Mungu ndiye aliyevibuni, Mungu ndiye aliyeviumba, Mungu ndiye anayevitegemeza. Jibu pekee linaloaminika kuhusu chimbuko la malimwengu hayo, dunia hii, na wanadamu - ni Mungu.
3. Mungu Huingia Katika Mahusiano Na Watu Binafsi
Mungu yule aliyezibuni mbingu hizo na nyota, aliyeyaumba malimwengu hayo, anatafuta kuwa na uhusiano nasi binafsi. Alikuwa na uhusiano wake binafsi na Musa: "Bwana akasema na Musa....kama vile mtu asemavyo na rafiki yake" (Kutoka 33:11). Mungu Mwenyewe anataka kuingia katika uhusiano nawe na kuwa Rafiki yako. Yesu aliwaahidi wale wanaomfuata, akisema "Ninyi mmekuwa rafiki zangu" (Yohana 15:14).
Sisi sote tumeshughulika sana na wazo hilo la Mungu, kwa kuwa wanadamu kwa asili wanapenda dini. Hakuna mnyama yeyote ajengaye madhabahu kwa ajili ya ibada. Lakini kila mahali unapowakuta wanaume na wanawake, unawakuta wakiabudu. Ndani ya kila moyo wa mwanadamu kuna ufahamu kuwa Mungu yuko, tamaa ya kuwa rafiki wa Mungu. Tunapoitikia hiyo tamaa yetu na kumpata Mungu, hatuwi na mashaka tena juu ya kuwako kwake na hitaji letu.

Katika miaka ile ya 1990 mamilioni ya wanaomkana Mungu katika nchi ya Urusi waliachana na imani yao hiyo ya kumkana Mungu, kisha wakamgeukia Mungu. Profesa wa Chuo Kikuu cha St. Petersburg alitoa kauli yake inayofanana na maoni yaliyotolewa na wakana Mungu wengi katika Umoja wa Kisovieti iliyopita:
"Nimetafuta maana ya maisha katika utafiti wangu wa kisayansi, lakini sikuona kitu chochote cha kutegemea. Wanasayansi wanaonizunguka mimi wanazo hisia hizo hizo za ukiwa. Nilipoangalia ukubwa wa malimwengu katika somo langu la elimu ya nyota, kisha nikaangalia ukiwa uliomo moyoni mwangu, niliona kwamba ni lazima pawe na maana fulani. Kisha nilipoipokea Biblia uliyonipa na kuanza kuisoma, ukiwa katika maisha yangu ukajazwa. Nimeiona Biblia kuwa ndiyo chimbuko la pekee la matumaini kwa nafsi yangu. Nimempokea Yesu kama Mwokozi wangu, nami nimepata amani ya kweli pamoja na kuridhika katika maisha yangu".
Mkristo anamwamini Mungu kwa sababu yeye amekutana naye na kugundua kwamba anayatosheleza mahitaji makubwa sana ya moyo wake. Mungu ambaye Wakristo wamemuona kuwa yuko, anatupatia mtazamo mpya, maana mpya, makusudi mapya na furaha mpya.
Mungu hatuahidi sisi kwamba tutakuwa na maisha yasiyo na taabu, wala mapambano, ila yeye anatuhakikishia kwamba atatuongoza na kutusaidia kama tutakuwa na uhusiano binafsi naye. Na mamilioni ya Wakristo wanaweza kutoa ushuhuda wao kwamba ingekuwa heri kwao kuacha kila kitu kuliko kuyarudia maisha yale yasiyokuwa na Mungu.
Hii ndiyo ajabu kuu kuliko zote kwamba yule Mungu Mwenyezi aliyeyabuni, aliyeyaumba na kuyategemeza malimwengu hayo anataka kufanya uhusiano na kila mwanaume na mwanamke, kila mvulana na msichana. Daudi alishangaa sana kuhusu jambo hilo alipoandika maneno haya:
"Nikiangalia mbingu, kazi ya vidole vyako, mwezi na nyota ulizozimika huko, mtu ni nini ee Mungu hata umfikirie mwanadamu ni nini hata umjali?" - (Zaburi 8:3,4).
Muumbaji wetu ana "mjali" kila mmoja wetu. Yeye binafsi anakupenda sana wewe kana kwamba wewe ulikuwa ni kiumbe chake cha pekee alichokiumba.
Basi tunaweza kumwamini Mungu:
(1) Kwa sababu ya ubunifu wake wenye sehemu nyingi katika kila kitu alichokiumba ambacho kinatuzunguka sisi.
(2) Kwa sababu shauku ile iliyomo ndani yetu juu ya Mungu inatufanya tusiwe na raha mpaka tupatapo pumziko letu ndani yake tena.
(3) Kwa sababu tunapomtafuta na kumpata, Mungu hutosheleza kila haja tuliyo nayo pamoja na shauku yetu - kikamilifu!

4. Ni Mungu Wa Aina Gani?
Ni jambo la busara tu kwamba Mungu aliye na nafsi yake apende kujifunua mwenyewe kwa viumbe wake kama vile baba atakavyo watoto wake wamjue. Na katika Biblia Mungu anatuambia yeye ni nani, tena anafananaje.
Ni mfano gani alioutumia Mungu katika kuwaumba wanaume na wanawake?
"Hivyo Mungu akaumba mtu kwa mfano wake, kwa mfano wa Mungu alimwumba" (Mwanzo 1:27).
Kwa kuwa sisi tumeumbwa kwa mfano wa Mungu, basi, uwezo wetu wa kufikiri na kujisikia, kukumbuka na kutumaini, kutafakari na kuchambua mambo - chimbuko lake lote latoka kwake. Je, tabia kuu ya Mungu ni ipi?
"Mungu ni upendo" (1 Yohana 4:8).
Mungu hufanya uhusiano wake na wanadamu kutokana na moyo wake wa upendo. Hakuna kitu cho chote alichofanya au atakachopata kufanya ambacho hakijasababishwa na upendo wake usio na ubinafsi, ujitoao mhanga.
5. Jinsi Yesu Anavyotufunulia Alivyo Mungu
Katika Biblia Mungu anarudia tena na tena kueleza habari zake Mwenyewe kwamba Yeye ni Baba.
"Je! Sisi sote si watoto wa baba mmoja"?
"Je, sisi sote hatukuumbwa na Mungu yule yule?" Malaki 2:10.
Baadhi ya mababa tuwaonao leo si cho chote, bali hawapendezi. Kuna mababa wasiojali, mababa wanaotukana matusi. Mungu si kama hao. Yeye anajali, ni Baba anayeguswa sana na mambo yetu. Ni Baba apendaye kucheza na mwanawe au binti yake, ni Baba anayewafurahisha sana watoto wake kwa kuwasimulia hadithi kabla hawajaenda kulala usiku.
Baba yetu huyo mwenye upendo alitaka kufanya zaidi ya kule kujifunua Mwenyewe kwa njia ya maneno ya Maandiko. Alijua kwamba yule mtu tunayeishi naye ni mtu halisi kuliko yule tunayesikia tu habari zake au tunayesoma habari zake. Kwa hiyo yeye akaja katika dunia yetu kama mtu halisi - yaani, yule mtu Yesu.
"Kristo mfano wa Mungu asiyeonekana" - (Wakolosai 1:15).
Basi kama wewe umemwona Yesu, utakuwa umemwona Mungu. Alijishusha hadhi yake na kuwa sawa sawa na sisi akawa kama sisi - ili apate kutufundisha jinsi ya kuishi na kuwa na furaha, ili kwamba sisi tupate kuona jinsi Mungu alivyo hasa. Yesu ni Mungu aliyeonekana kwa macho. Yeye mwenyewe alisema, "Aliyeniona mimi amemwona Baba" (Yohana 14:9).
Usomapo kisa cha Yesu katika vitabu vinne vya Injili, yaani, vitabu vinne vya kwanza vya Agano Jipya, utagundua picha ya kuvutia sana ya Baba yetu aliye mbinguni. Wavuvi wale wa kawaida tu walizitupa nyavu zao ili kumfuata Yesu, na watoto wadogo wakasongamana kwenda kwake kupokea baraka zake. Aliweza, kumfariji mwenye dhambi aliyeharibika kabisa na kuzivunja nguvu za mnafiki sugu aliyejihesabia haki yeye mwenyewe. Aliponya kila maradhi kuanzia upofu hadi ukoma. Katika matendo yake yote Yesu alidhihirisha kwamba Mungu ni upendo! Alikidhi haja ya mwanadamu kwa namna ambayo hakuna mtu ye yote aliyepata kufanya hivyo kabla yake au tangu wakati wake!
Ufunuo wa Yesu wa mwisho ambao unaonyesha utukufu wa jinsi Mungu alivyo ulitokea pale msalabani.
"Kwa maana jinsi hii Mungu aliupenda ulimwengu, hata akamtoa Mwanawe pekee, ili kila mtu amwaminiye asipotee, bali awe na uzima wa milele" - (Yohana 3:16).
Yesu alikufa sio tu kutupatia maisha yenye furaha sasa, bali kutupa uzima wa milele pia. Kwa vipindi virefu watu walishangaa, na kutumaini, na kuota
ndoto juu ya Mungu. Waliiona kazi ya mikono yake mbinguni na katika uzuri wa viumbe vya asili. Kisha pale msalabani, Yesu alikivunjilia mbali kimya cha vizazi vingi, na watu wakajikuta wanautazama ana kwa ana uso wa Mungu, wakimwona yeye kama alivyo hasa - yeye ni upendo, wa milele, tena ni upendo udumuo milele!
Wewe waweza kumgundua Mungu sasa hivi Yesu anapomfunua kwako. Ugunduzi huo utakufanya utoe uthibitisho wako binafsi, ukisema: "Baba, nakupenda!"




NI JINSI GANI MUNGU ANAHITAJI

TUMUIMBIE?

  • Je biblia humaanisha nini isemapo "tumsifu Mungu kwa matari  na kucheza (zaburi 150:4)?
  • Je biblia humaanisha nini izungumziapo kucheza?
  • Vipi kuhusu wakristo waimbao kwa kucheza, je wanafuata kile Biblia isemacho au wamepotoshwa?
  • Ni kanuni gani za kuzingatia ili tuimbe nyimbo zikubalikazo mbele za Mungu?
  • Je uimbaji ulianza lini katika Biblia?
  • Biblia hutoa muongozo gani kuhusu matumizi ya vyombo vya muziki?
  • Kuna usahihi wowote kuwakataza watu wasicheze katika Ibada wakati biblia humuonyesha daudi na wakati Miriam akicheza?  

Majibu ya aswali haya na mengine mengi yahusuyo mziki waweza kuyapata katika somo hili, fuatiliasomo hili kwa makini mpaka mwisho na Bwana atakufunulia siri ya pekee sana juu ya muziki ukubalikao mbele zake kwa mujibiu wa Biblia.

Uimbaji ni mojawapo ya huduma takatifu zinazoendeshwa katika ibada au mikutano ambapo watu hukusanyika ili kumwabudu Mungu Mwenyenzi aliye mkuu na muumbaji wa vitu vyote vilivyo hai na visivyo hai hapa duniani na mbinguni. Mungu mwenyewe ametoa miongozo ndani ya neno lake takatifu ni jinsi gani watu waenende mbele zake wakati wa ibada. Miongozo hiyo inapaswa iangaliwe na kufuatwa kwa makini sana ili ibada iweze kupata kibali machoni pa Mungu na hao waabuduo waweze kupata kibali machoni pake vile vile na Baraka tele. Ibada ni tendo(worship is a verb).

Ibada kamili lazima iwe na mambo
1.      Lazima tujiandae kuabudu
2.      Tujiandae kusikia neno la Mungu
3.      Kujiandaa kuitikia kile Mungu anacho tuambia na
4.      Kukubali kutumwa na Mungu
“Katika mambo hayo humaanisha kuwa, ibada ni tendo la kumwabudu na kumsifu Mungu;katika ibada Mungu sharti anenenasi na kutenda nasi;katika ibada huitkia sauti ya Mungu na kuhudumiana na viumbe wote vyote hujumuika jamopa katika ibada”Robert W.Webber uk26

 Sababu za Kuimba

Je, umewahi kuketi chini na kutafakari walao kwa muda wa nusu saa ukitafakari kwa nini unaimba nyimbo za dini? Mtu, kwaya au kikundi chochote cha uimbaji, kama hawaelewi sababu ya kutunga na kuimba nyimbo zao, basi ni rahisi sana kuifanya huduma kwa mtazamo na malengo yote ya uimbaji kinyume na mapezi ya Mungu. Ikumbukwe kwamba ‘katika muziki wa kidini Mungu ndiye kiini, na sio mambo ya ubinafsi wa mtu. Wazo la kumsifu Mungu kwa ajili ya kujiburudisha ni wazo geni katika Biblia.’[1] Vile vile kufanya huduma ya nyimbo kwa madhumini ya kujipatia fedha ni mawazo potovu yayoiharibu sana huduma hii takatifu sana.
Mfanyieni Bwana kelele za shangwe

Hindu ya rejea kwa sauti kubwa ya muziki inatukumbusha kuhusu onyo, “mfanyieni Bwana kelele za shangwe.” Usemi unajitokeza mara kwa mara katika Biblia ya tafsri ya mfalme James (KJV) lakini kwa tofauti kidogo katika Agano la Kale (Zaburi 66:1; 81:1; 95:1-2; 98:4, 6; 100:1). Mafungu haya ya Biblia yametumiwa mara kwa mara kutetea matumizi ya sauti ya juu  katika muziki wa ‘rock’ (aina ya dansi ya kurukaruka ndani ya kanisa). Man‘ruwa,’-רוע  Neno hili halimaanishi kufanya kelele za juu zisizochaguliwa kwa busara, bali ni kupaza sauti kwa furaha… mfano mzuri unapatikana katika kitabu cha Ayubu 38:7 mahali ambapo neno lilo hilo ruwa’-רוע
limetumiwa kuelezea wana wa Mungu ‘walipopaaza sauti kwa furaha’ baada ya umbaji. Uimbaji wa viumbe vya mbinguni wakati wa uumbaji hauwezi kabisa kuelezewa kuwa ni kelele za juu kwa sababu kelele huashiria sauti mbaya.’[2]

Mara nyingi watu wa Mungu wamekosa mibaraka yake kwa sababu ya vurugu nyingi na ambazo hazina maana yoyote wanapokuwa mbele za Mungu kwa ajili ya kumwabudu. Uwepo wa Mungu unakosekana. Ibada na hasa katika uibaji wa kwaya hugeuka kuwa maburudisho yenye mvuto wa kidunia.  Hivyo baraka za Mungu zinakosekana. Watu hurudi nyumbani kama walivyokuja na pengine hurudi nyumbani wakiwa wamechanganyikiwa zaidi ya walivyokuwa walipokuwa wakija kwenye ibada. Mungu hawezi kubariki fujo na machafuko hata siku moja. Kwa maana ‘Mungu si Mungu wa machafuko, bali wa amani; vile vile kama ilivyo katika makanisa yote ya watakatifu.’ (1Wakorintho 14:33). Kwa sababu hiyo mashauri yametolewa kwamba ‘Lakini mambo yote na yatendeke kwa uzuri na kwa utaratibu (1Wakorintho 14:40).
Ni jambo la muhimu sana kwa wote waabuduo kukumbuka daima kuwa kama kuna jambo nyeti na lenye uzito wa pekee ni lile la kwenda kukutana na Mungu katika ibada. Kicho na adabu halisi vinapaswa kuonekana katika maisha ya waabuduo. Sababu ni kwamba  Mfalme Mkuu, ndiyo Mungu mwenye nguvu, Muumbaji wa mbingu na nchi na vyote vilivyomo, Mwokozi wetu wa pekee Yesu Kristo, kwa njia ya Roho wake Mtakatifu anakuwa na watu wake katika ibada. Nao malaika kutoka mbinguni mahali ambapo uzuri na utaratibu kamili hutawala mile na hata milele, hujihudhurisha katika mikutano ya watu wa Mungu wakutanapo ili kutoa sifa na kumwabudu Mfalme wa milele au kufanya jambo lolote lile kwa ajili yake

Kwanza kabisa tunaona katika maandiko matakatifu habari ya wanawake wakicheza kwa mara ya kwanza katika kutoka 15:20, 21. ‘Na Miriamu, nabii mke, ndugu yake Haruni, akatwaa tari mkononi mwake; wanawake wakatoka wote wakaenda nyuma yake, wenye matari na kucheza. Miriamu akawaitikia mwimbieni Bwana, kwa maana ametukuka sana; farasi na mpanda farasi amewatupa baharini.’ Tukio hili lilitokea baada ya Mungu kuwaangamiza Wamisri kwa kuwafunika na maji katika bahari ya Shamu wakiwa katika harakati za kuwafuatia Wana wa Israeli ili kuwarudisha utumwani katika nchi ya Misri. Tunaambiwa kuwa Miriamu pamoja na wanawake wengine walicheza. 

Neno la Kiebrania lililotumika hapa ni miholah’ (מְחֹלָה) ambalo humaanisha kutembea katika mduara. Biblia, tafsiri ya KJV hutafsiri ‘dansi’ ya muduara. Lakini maana yake halisi ni kutembea (matching) katika mduara. Kwa kufafanua zaidi, miholah’-מְחֹלָה    humaanisha kucheza (kutembea)  katika mistari miwili, kucheza katika kambi la jeshi.’ Mara nyingi hueleweka kwamba jeshi au askari wanacheza gwaride. Jeshi Lichezapo gwaride halinengui bali hutembe katika mwendo maalum ambao hupangiliwa katika mistari miwili au zaid,mwendo huu huwa katika utaratibu uliokubalkikai. Hivyo wanawake waliomfuata Miriamu nyuma walikuwa wakienda kwa kumachi (kutembea) na sio kwa kukatika, kurukaruka au kunengua viuno vyao. Kutafsiri fungu hili kumaanisha kwamba ilikuwa ni ‘dansi’ ya kukatika au kunengua viuno ni kulitendea isivyo halali fungu hili la Biblia. Jambo lingine la kuzingatia katika tukio hili la Miriamu na wanawake wenzake ni kwamba hawakuwa kwenye mkutano wa ibada au mkutano wowote wa mafundisho ya neno la Mungu. Bali walikuwa safarini kutoka katika nchi ya Misri kwenda Kanaani na walikuwa jangwani.

Kwa upande mwingine neno hilo hilo ‘miholaמְחֹלָה limetumiwa katika 1Samweli 18:6 ambapo tunasoma, ‘hata ikawa, walipokuwa wakienda, hapo Daudi aliporudi baada ya kumwua yule Mfilisti, wanawake wakatoka katika miji yote ya Israeli, kwa kuimba na kucheza, ili kumlaki mfalme Sauli; wakatoka na matari, na shangwe, na vinanda.’ Katika Waamuzi 11:34, hapo napo neno ‘mihola’מְחֹלָה limetumiwa wakati binti wa Yeftha alipotoka kumlaki baba yake alipotoka vitani. Matukio yote hayo hayawezi kuchukuliwa kama kigezo cha Wakristo kuimba na kucheza dansi katika mikutano ya ibada. Matukio hayo hayakuwa ya ibada. Katika matukio yote hayo wanaoonekana wakicheza ni wanawake peke yao. Siku hizi wanaume katika kwaya mbalimbali wanaonekana wakicheza na kurukaruka kama wendawazimu.

Katika 2Samueli 6:14 Mfalme Daudi aliopkuwa analileta sanduku la agano katika mji wa Daudi, yeye alicheza mbele za Bwana kwa nguvu zake zote. Neno la Kiebrania lililotumika hapo ni kara’  כָּרַר  ambalo humaanisha kurukaruka na kuzungukazunguka (leaping and whirling) na wengine hufasiri kucheza. Hivyo maana yake halisi ni kwamba, kwanza Daudi alikuwa kwenye msafara wa kulileta sanduku la Bwana kutoka kwenye nyumba ya Obed-Edom hadi kwenye mji wa Daudi. Akiwa kwenye msafara huo, Daudi, kwa furaha kubwa alionekana akirukaruka na kuzunguka zunguka mbele ya sanduku la Bwana.

Mambo ya kuzingatiakatika muktadha wa uchezaji wa Daudi:
1.      Daudi hakuwa na maandalizi yoyote ya namna ya kucheza. Yeye alizunguka zunguka huko na huko na kuruka kuruka huko na huko jambo ambalo mtu yeyote anaweza kulifanya apatwapo na furaha isiyo na kifani. Mfano mzuri ni pale mtoto apatapo matokeo ya mtihani na kuona kuwa amefauru kwa kiwango cha juu sana. Anaweza kuruka ruka na kucheza cheza bila ya maandalizi yoyote ni jinsi gani angeruka ruka endapo angefauru vizuri. Na kucheza kwa Daudi kulikuwa ni tukio la papo hapo. Halikuwa tukio la kuendelea au mtindo wa ibada ya uimbaji.
2.      Hakuwa na timu au kikundi cha watu ambacho alifanya nacho maandalizi kwa ajili ya kucheza.
3.      Hakuwa Hekaluni au kwenye mkutano wa ibada au mafundisho yoyote ya neno la Mungu. Alijua wazi kwamba ndani ya nyumba ya ibada hakuna kurukaruka au kuzunguka zunguka kwa namna iwayo yote maana imeandikwa, ‘Lakini Bwana yumo ndani ya hekalu lake takatifu; dunia yote na inyamaze kimya mbele zake (Habakuki 2:20).
4.      Daudi hakuwa anacheza kama ni sehemu ya ibada mbele za Mungu aliye hai. Pia hatuoni kama alikuwa anaimba wimbo wowote wakati alipokuwa anarukaruka na kuzunguka zunguka mbele ya sanduku la Bwana. Wala haikuwepo kwaya yoyote ikiimba nyimbo. Kurukaruka na kuzunguka zunguka kwa Daudi mbele ya sanduku la Bwana au Miriamu  pamoja na wanawake waliomfuata nyuma, hakuwezi kuchuliwa kuwa ni kigezo cha kuhalalisha dansi katika kanisa la Mungu aliye hai au katika ulimwengu wa Kikrsito.

Katika Zaburi 149:3 na 150:4, kuna neno jingine la Kiebrania linalofasiriwa kama ‘dansi’ ambalo ni ‘maholi’- מָחוֹל . Haya mafungu ya Biblia ni ya muhimu sana kwasababu Ibilisi na makanisa yachezayo dansi huyatumia kuunga mkono hoja ya watu wengi kuwa ‘dansi’ ni sehemu ya ibada kanisani. Ikiangaliwa kwa makini sana itaonekana kuwa neno ‘dansi’ katika mafungu haya mawili ya Biblia linabishaniwa sana na wana-eliungu (Theologians). Baadhi ya wana-eliungu huamini kwamba ‘maholi’-מָחוֹל  hutokana na neno ‘chuwl’ amabalo humaanisha ‘fanya uwazi.’ Kwa maelezo hayo inawezekana ni chombo cha muziki chenye uwazi kama vile bomba. Tafsiri hii yaweza kuwa sahihi kwa sababu ukiangalia kwa makini sana, tunaweza kuona kuwa ‘maholi’-מָחוֹל  ni chombo cha muziki kwa sababu katika  Zaburi 149:3 na 150:4 kuna mlolongo wa vyombo vya muziki kama ifuatavyo:

Zaburi 150:3- Kwa mvumo wa baragumu……kwa kinanda na kinubi
             150:4-kwa matari   na kucheza (maholi)-מָחוֹל
             150:4-Kwa zeze     na    filimbi
             150:5- Kwa matoazi yaliyao………kwa matoazi yavumayo

Katika sura hii sehemu zote za mafungu kuna usambamba (parallelism) wa vyombo vya muziki tu isipokuwa chombo cha muziki ‘matari’ ndiyo huambatanishwa na kucheza. Msambamba wa vyomvo vya muziki katika sura hii ni wazi kuwa neno lililofasiriwa kama ‘kucheza’ kutoka katika neno la Kiebrania ‘maholi’-מָחוֹל  si sahihi. Neno ‘maholi’-מָחוֹל  linaonekana kuwa chombo cha muziki katika Zaburi 149:3 na Zaburi 150:4. Neno hilo linatokea katika mlolongo wa vyombo vinavyoweza kutumika katika kumsifu Bwana. Kwa kuwa mtunga zaburi anaoorodhesha vyombo vyote vinavyoweza kutumiwa katika kumsifu Bwana ni vyema kuelewa kuwa ‘maholi’- מָחוֹל  ni chombo cha muziki, kwa namna yoyote kinavyoweza kuonekana.[3]

Katika Muongozo wa ‘The Study Bible,’ tafsiri ya Mfalme James, katika ‘footnote,’ inatafsiri neno ‘maholi” מָחוֹל kuwa ni chombo cha muziki aina ya ‘bomba’ (pipe).[4] Zamani, katika shule za msingi, bendi za shule zilikuwa na wapiga filimbi ambazo zilikuwa ni bomba refu kidogo na matundu kama matano au sita . Ngoma ilipopigwa na wapiga filimbi walipiga muziki kusindikiza mlio wa ngoma. Chombo cha jinsi kama hiyo hiyo chaweza kutumika katika kumsifu Mungu. Izingatiwe kwamba, ‘neno la Kiebrania lilofasiriwa “Zaburi” linatokana na neno la asili linalomaanisha ‘kuimba kwa kutumia vyombo vya muziki.’[5] Katika Zaburi 81:2 tunasoma, ‘pazeeni Zaburi (vyombo vya muziki), pigeni matari, kinubi chenye sauti nzuri, na kinanda.’ Hapa anataja kupaza Zaburi ambayo humaanisha chombo chochote kinachoweza kutumiwa katika kumsifu Mungu. Kwa hiyo dhana ya kwamba Zaburi 150:4 huelekeza watu kucheza dansi mbele za Mungu ni dhana potofu na tafsiri iliyopotoka.

Bila shaka watu wengi wanaweza kuibuka na hoja kwamba, ni kweli ‘maholi’-מָחוֹל   chaweza  kuwa ni chombo cha aina fulani cha muziki na hasa chombo cha muziki abamcho ni kama aina ya bomba (pipe); lakini je mfalme Daudi hakuwahi kucheza mbele za Bwana Mungu? Jibu liko wazi kabisa. Ni kweli aliwahi kucheza. Neno la Kiebrania ‘karar’-כָּרַר  lililotumika katika 2Samweli 6:14 kama tulivyoona hapo awali, humaanisha kurukaruka na kuzunguka zunguka. Davidson anaeleza karar’-כָּרַר  kuwa ni kurukaruka. Pia kwamba mwana-kondoo anaitwa hivyo (karar) kwa sababu ya kurukaruka kwake.’[6]

Maana halisi ya neno kucheza katika Biblia
Kwa wale wote wenye dhana potofu kwamba Daudi alicheza dansi katika 2Sameli 6:14 ;Zaburi 149:3 na 150:4 anasistiza kwamba watu wamwimbie Bwana kwa matari na kucheza, wanapaswa kuelewa kuwa :
  • Katika 2Samweli 6:14 neno la Kiebrania lilotumika ni ‘karar’- כָּרַר  humaanisha kurukaruka na kuzunguka zunguka.
  • Katika Zaburi 149:3 na 150:4 neno la Kiebrania lilotumika ni ‘maholi’ -מָחוֹל  humaanisha chombo cha muziki cha aina kama ya bomba (pipe). Maneno haya yana maana tofauti na vile watu waelewavyo kuwa ni uchezaji dansi
  • Daudi hakucheza dansi katika 2Samweli 6:14 bali ali-‘karar’-כָּרַר   yaani alirukaruka kama mwana-kondoo aliyenenepeshwa anavyorukaruka akiwa nje ya zizi. Na wala hakuwa ana- ‘maholi,’- מָחוֹל  yaani akipiga chombo cha muziki. Mwana-kondoo huwa hana maandalizi au mafunzo ni namna gani arukeruke. Mwana-kondoo anarukaruka bila ya kufuata mwelekeo wa aina fulani na wala hafuati mapigo au mudundo fulani. Hivyo ndivyo ilivyokuwa kwa Daudi. Hakuwa na muda wa kujifunza na wala hatuambiwi ya kwamba aliwahi kwenda kwenye shule yoyote ya kujifunza namna ya kucheza mbele za Bwana kwa ustadi wa mwelekeo fulani kama kwaya nyingi zifanyavyo siku hizi.
  • Daudi hakujikaririsha njia iwayo yote ile kwa ajili ya kurukaruka na kutupa mikono na miguu huko na huko kama kwaya za leo zifanyavyo kwa kushinda ndani ya jengo la kanisa au kwenye viwanja fulani na kujikaririsha ni namna gani wataruka kwa pamoja na kutupa mikono kwa pamoja. Na ieleweke tu kwamba kwaya za siku hizi hazipo kumwimbia na kumsifu Mungu bali zipo kwa ajili ya kutimiza kiu yao kali ya dansi ya dunia huku wakiwa wameivika dansi yao vazi la Kikrsito. Kwa lugha rahisi, kile kinachofanywa na kwaya za siku hizi ni ‘upagani mambo kikristo.’ Kwa upande mwingine lazima tukubali kuwa pepo mchafu ameingia katika fani ya uimbaji na muziki kwa ujumla na ni lazima akemewe kwa nguvu zote ili atoke katika mioyo ya waimbaji ili wabaki wakimwimbia Bwana na kumtukuza yeye tu.

Mashauri ya nabii Ellen G white kuhusu uimbaji
Makelele na midundo na kucheza ni ishara ya ukaribu wa kufungwa kwa mlango wa rehema . Mjumbe wa Mungu anaelezea kile ambacho Bwana alimwonyesha kuhusu ibada ya ghasia na makele ambazo huonekana katika ibada siku hizi.

‘Mambo yale umeyaelezea…Bwana amenionyesha kwamba yatatokea tena kabla ya kufungwa kwa mlango wa rehema. Kutakuwepo na kupiga makelele, pamoja na ngoma, muziki, na kucheza. Akili za mwanadmu zitachanganyikiwa kiasi cha kwamba hazitaweza kuaminiwa kufanya maamuzi sahihi.’[7]

White pia anasema kuwa, ‘Bwana amenionyesha kwamba nadharia na mbinu potovu vitaingizwa katika makambi yetu, na kwamba historia ya zamani itarudiwa…Mambo yale yaliyokuweko wakati wa nyuma yatakuwepo siku za mbele (ndio sasa). Shetani ataufanya muziki kuwa mtego kwa namna unavyoendeshwa. Mungu anawaita watu wake, amabao wana ushuhuda, kusoma na kutafakari kwa makini, na kuchukua jukumu la kusikia.’[8]

Ni muhimu kwa watu wa Mungu kuelewa kuwa uimbaji wajinsi hiyo kamwe hauongozwi na uwezo wa Mungu Roho Mtakatifu. Mjumbe wa Mungu anasema tena kwamba, ‘Roho Mtakatifu kamwe hajidhihirishi mwenyewe kwa njia kama hii, katika ghasia za makelele. Huu ni ubunifu wa shetani ili kufunika werevu wa mbinu zake ili kuufanya ukweli ulio safi, ulionyoka, wenye kuinua, wenye kunfanya mtu kuwa mungwana, ukweli wenye kutakasa kwa wakati huu usiwe na matokeo mazuri. Ni vema kutokuwa na ibada ya Mungu iliyochanganywa na muziki kuliko kutumia vyombo vya muziki kufanya kazi ambayo mnao January lilionyesha kwangu kwamba italetwa katika makambi yetu…Ghasia za makelele hushitua akili na hupotosha kile ambacho kama kingeendeshwa vizuri kingeweza kuwa Baraka…Mambo yote yaliyokuwepo siku za nyuma yatajitokeza siku za usoni. Shetani ataufanaya muziki kuwa mtego kwa jinsi uanvyoendeshwa.’[9]

Kucheza, midundo ya muziki na midundo ya ngoma na kadhalika vimetawala na kuwa chanzo cha machafuko katika ibada.
Mjumbe wa Mungu anasema kuwa,
 ‘Roho Mtakatifu hana sehemu yoyote katika makelele na milio mikubwa kama ilivyopita mbele zangu… Shetani anafanya kazi katika makelele na machafuko ya muziki, ambao kama uingefanywa kwa usahihi, ungekuwa ni sifa na utukufu kwa Mungu. Anafanya madhara ya       huo muziki kama sumu kali ya nyoka.’[10]
Naliona ya kwamba utaratibu wa Mungu umebadilishwa, na miongozo yake muhimu imepuuzwa na wale wote wanaoiga utamaduni wa Amerika. Nilirejeshwa kwa fungu la Kumbukumbu la Torati 22:5 kwamba mwanamke asivae mavazi yampasyo mwanamume…kumekuwapo na hali ya wanawake katika mavazi yao na mwonekano wao kuwa karibu sana sawa na ule wa wanaume kwa kadiri iwezekanavyo, na wanashona mavazi yao karibu sana na yale ya wanaume, lakini Mungu anasema wazi kuwa hayo ni machukizo.’[11] 1T 457
Wakati kanisa zima au kwaya maalumu inapoimba nyimbo za kumsifu na kumtukuza Mungu Aliye Mkuu kwa kuimba kwa uzuri , utaratibu na utakatifu wote, malaika nao huunganika nao katika kumsifu Mungu huku wakivipiga vinubi vyao Mara nyingi, kwenye mikutano ya jinsi hiyo waabuduo wanatoka wakiwa wamepata burudiko la Kiroho na ‘ruwa,’-רוע  Neno hili halimaanishi kufanya kelele za juu zisizochaguliwa kwa busara, bali ni kupaaza sauti kwa furaha…
Katika kitabu cha Ayubu 38:7 mahali ambapo neno lilo hilo ‘ruwa’-רוע   limetumiwa kuelezea wana wa Mungu ‘walipopaaza sauti kwa furaha’ baada ya umbaji. Uimbaji wa viumbe vya mbinguni wakati wa uumbaji hauwezi kabisa kuelezewa kuwa ni kelele za juu kwa sababu kelele huashiria sauti mbaya.’[12]

Waimbaji wapaswa kuadabishwa
 E.G. White alikutana na tatizo hili siku za maisha yake na utumishi akasema  ‘lakini wakati mwingine ni vigumu zaidi kuwaadibisha waimbaji na kuwaweka katika utaratibu wa kazi…Wengi wanataka kufanya mambo kwa kufuata mtindo wao wenyewe; wanakataa kushauriwa; na hawako tayari kusikiliza uongozi.’[13]


Mahali na Wakati wa Kuimba

Biblia haituelekezi tu kuimba katika nyumba ya Mungu, bali pia miongoni mwa wasioamini, katika nchi za kigeni, na wakati wa mateso, na katikati ya watakatifu mwandishi wa kitabu cha Waebrania anasema, ‘nitalihubiri jina lako kwa ndugu zangu; katikati ya kanisa nitakuimbia sifa (Waebrania 2:12).

Mtunga Zaburi anasisitiza kwa kusema, ‘mwimbieni Bwna wimbo mpya, sifa zake katika kusanyiko la watauwa (Zaburi 149:1). 

Naye mtume Paulo imeandikwa, ‘kwa hiyo nitakushukuru kati ya mataifa, nami nitaliimbia jina lako (Warumi 15:9).

Katika kitabu cha nabii Isaya imeandikwa, ‘jangwa na miji yake na ipaze sauti zao, vijiji vinavyokalia na Kedari, na waimbe wenyeji wa Sela, wapige kelele toka vilele vya milima, na wamtukuze BWANA, na kutangaza sifa zake visiwani (Isaya 42:11, 12). 

Wakiwa gerezani, Paulo na Sila ‘walilkuwa wakimwomba Mungu na kumwimbia nyimbo za sifa, na wafungwa wengine walikiuwa wakiwasikiliza (Matendo ya Mitume 16:25).

Kwa mafungu hayo machache ni wazi kuwa nyimbo za kumsifu Mungu zaweza kuimbwa popote pale. Gerezani, katikati ya mataifa, kanisani na katika kusanyiko lolote la watakatifu. Mwanadamu anaitwa kumwimbia na kumsifu Mungu mahali popote pale alipo. Kwamba ana furaha au huzuni, ana njaa au shibe na amwimbia na kumsifu Mungu Muumbaji.

Hindu za rejea za mara kwa mara kwa ajili ya kumsifu Mungu miongoni mwa wapagani au watu wa mataifa (2Samewli 22:50; Warumi 15:9; 108:3) huashiria kuwa uimbaji ulionekana kuwa njia ya kumshuhudia BWANA kwa watu wasioamini. Hata hivyo hakuna uthibitisho wowote katika Biblia kwamba Wayahudi au Wakristo wa kwanza walifuatisha sauti na nyimbo za kidunia ili kuweza kuwahubiri watu wa mataifa.

Wayahudi na Wakristo wa kwanza waliamini kuwa muziki wa kidunia ulikuwa hauna nafasi katika nyumba ya ibada.[14] 

Mwanzo wa Huduma ya Muziki Katika Biblia:
Kabla ya wana wa Israeli kuingia katika nchi ya Palestina, huduma ya muziki wakati wa ibada kwa kusudi la kukidhi mahitaji ya waabuduo haikuwepo. Kabla ya wakati huo hindu za rejea kwa muziki kimsingi zilihusiana na wanawake kuimba na kucheza kwa ajili ya kusherehekea tukio fulani maalumu. Mfano wa kwanza kabisa ni ule wa Miriamu akiongoza kundi la wanawake ambao walikuwa wakiimba na kucheza kwa sababu Bwana Mungu aliwatupa Wamisri katika bahari ya Shamu na kuwangamiza huku akiwaokoa wana wa Israeli kwa muujiza wa ajabu kabisa (Kutoka 15:1-2). Pia, wakati Daudi alipomua Goriathi ambaye alikuwa ni tishio kubwa kwa wana wa Israeli, wanawake walicheza wakishangilia ushindi huo mkuu (1Samuli 18:6-7). Na mfano mwingine ni ule wa binti wa Yefta ambaye alimlaki babaye kwa matari na kucheza aliporudi kutoka vitani (Waamuzi 11:34).

Jambo la kuzingatia hapa ni kwamba wote hao waliimba na kucheza wakati ambao sio wa ibada na nje ya mahali pakuabudia au kanisa/hekalu.  Kulingana na taarifa ipatikanayo katika kitabu cha Mambo ya Nyakati kitabu cha kwanza, mfalme Daudi alianzisha huduma ya uimbaji katika hatua tatu:
1.Aliagiza vichwa wa familia za Kilawi kuchagua watu wapigao vyombo vya muziki na kwaya kwa ajili ya kulisafirisha sanduku la Agano kutoka kwa Wafilisti hadi hemani kwake katika mji wa Yerusalemu (1Nyakati 15:16-24).
2.Hatua ya pili ilitokea wakati sanduku la Agano lilikuwa limewekwa katika hema lake katika mahali pake (1Nyakati 8:11), kwaya moja ilikuwa ikiimba chini ya uongozi wa Asafu mbele ya Sanduku la Agano katika Jerusalemu  (1Nyakati 16:37-42).
3.Hatua ya tatu ya uanzishaji wa huduma ya muziki ilitokea  mwishoni mwa utawala wa mfalme Daudi wakati mfalme alipoandaa kwa undani kabisa huduma ya muziki ambao ungetumika katika hekalu ambalo Sulemani angelijenga (1Nyakati 23:2 hadi 26:32). Daudi aliunda kundi la Walawi 4000 kuwa waimbaji wa pekee (1Nyakati 15:16; 23:5). Kutoka kwenye kundi hili mfalme Daudi aliunda kwaya ya Kilawi yenye waimbaji 288.

Daudi mwenyewe alihusika pamoja na maofisa katika kuchagua viongozi 24 kuwa walinzi, kila mmoja alikuwa na wanamuziki 12. Jumla yao ilikuwa ni wanamuziki 288 (Nyakati 25:1-7). Hao nao waliajibika katika kuchagua wanamuziki wengine.[15]
Huduma ya Wanamuziki
Ili kuhakikisha kuwa kusiwepo machafuko au mgongano kati ya huduma ya makuhani na huduma ya wanamuziki ya Walawi, mfalme Daudi, kwa uangalifu mkubwa sana alifafanua nafasi, cheo, na kusudi la huduma ya wanamuziki (1Nyakati 23:25-31). Utendaji wa huduma ya wanamuziki ulikuwa chini ya makuhani (1Nyakati 23:28).

Viongozi wa kwaya au walimu wa kwaya wanapaswa kuelewa fika utendaji wao ili kusiwepo mgogoro baina yao na wachungaji. Ukweli ni kwamba mchungaji ndiye kiongozi wa kwaya. Tatizo kubwa linalojitokeza katika kanisa ni lile la walimu wa kwaya kutaka kumtawala mchungaji na kutaka mchungaji akubaliane na kufuata matakwa yao hata kama yako kinyume na neno la Mungu au kanuni za kanisa. Walimu wa kwaya wengi hukanyaga chini taratibu za kanisa na kufanya mambo kama wapendavyo kwa ajili ya faida yao wenyewe na familia zao badala ya kufanya kazi ya uimbaji kwa ajili ya Mungu.

Walimu wengi sana wa kwaya wamejaa kiburi na ukaidi usio wa kawaida. Wanadharau neno la Mungu, wanadharau uongozi wa kanisa na taratibu zake zote. Roho hiyo hiyo inaingizwa kwa waimbaji wote ambao nao hawako tayari kuheshimu wazee wa kanisa na wachungaji. Wanadharau taratibu zote za kanisa. Kiongozi wa kwaya anageuka kuwa mungu wao. Hili halikuanza leo. Tangu zamani roho ya ukaidi na kiburi, ikianzia na shetani mwenyewe kule mbinguni, imeonekana katika maisha ya waimbaji.

 Mjumbe wa Mungu E.G. White alikutana na tatizo hili siku za maisha yake na utumishi na aliandika, ‘lakini wakati mwingine ni vigumu zaidi kuwaadibisha waimbaji na kuwaweka katika utaratibu wa kazi…Wengi wanataka kufanya mambo kwa kufuata mtindo wao wenyewe; wanakataa kushauriwa; na hawako tayari kusikiliza uongozi.’[16]

Hili ni tatizo kubwa ambalo huleta giza na laana isiyo ya kawaida katika kanisa la Mungu.
· Kwaya nyingi sana zinafanya maamuzi zenyewe ni namna gani wataimba ili kukidhi haja yao ya muziki wa kidunia ambayo wengi waliipata kabla ya kuingia kanisani.
· Kwaya haziko tayari kuwasikiliza wazee wa makanisa labda kama naye mzee awe ametekwa na kuingia katika ukafiri wa jinsi hiyo hiyo.
· Kwaya haziko tayari kusikiliza wachungaji na adui yao mkubwa ni Roho ya Unabii na Biblia kwa ujumla. Kwaya nyingi zimekuwa ni mashirika yanayojitegemea ndani ya kanisa. Na wanaofaidika na kile kinachotokana na uimbaji huo ni wachache sana. Wengine wanakuwa ni bendera fuata upepo. Pale uongozi unapojaribu kusahihisha na kerekebisha uimbaji wao, na wakiona mafundisho yanapingana na matakwa yao na maslahi yao kwa ujumla, utajionea mwenyewe roho ya uasi iliyo ndani yao. Ndipo utajua kuwa wamevaa ngozi ya kondoo lakini ndani ni mbwa mwitu wakali mno. Wako tayari kupigana, kutukana na kubeza uongozi. Kweli hata ibilisi alipoona mambo yake yanapingwa kule mbinguni, aliazimia kupigana na roho hiyo hiyo imeipandikiza ndai ya waimbaji na hasa walimu wa kwaya walio wengi (Ufunuo 12:7-12). Ibilisi hakushinda kule mbinguni. Akatupwa chini. Kama Bwana aishivyo, waimbaji wote pamoja na walimu wao wanao kaidi neno la Mungu na kushindana na uongozi wa kanisa, muda si murefu watatupwa chini na wala hawatalishinda neno la Mungu.

VYOMBO VYA MUZIKI NA MATUMIZI YAKE KATIKA AGANO LA KALE NA JIPYA

Haiwezekani kuongelea habari ya vyombo vya muziki katka ulinasi wa Kikrisito siku hizi na upigaji wake katika ulinasi wa Kikrsito wa sasa bila ya kuchunguza katika Agano la Kale kama vilitumikaje. Kama tulivyokwisha kuona katika sura iliyotangulia, ‘Daudi hakuanzisha tu muda, mahali, na maneno kwa ajili ya huduma ya kwaya ya Walawi, lakini pia alitengeneza vyombo vya muziki ili vipate kutumiwa kwa ajili ya huduma yao.[17] Tunasoma, ‘na elfu nne walikuwa mabawabu; na elfu nne walimsiu BWANA kwa vinanda, nilivyovifanya, alisema Daudi, vya kumsifia (1Nyakati 23:5). ‘Wakasimama makuhani sawasawa na malinzi yao; Walawi nao pamoja na vinanda vya BWANA, alivyovifanya Daudi mfalme, ili kumshukuru BWANA, kwa maana fadhili zake ni za milele, hapo aliposifu Daudi kwa mikono yao; nao makuhani wakapiga panda mbele yao; nao Israeli wote wakasimama (2Nyakati 7:6). Hii ndiyo sababu inayofanya viitwe vyomb vya Daudi (2Nyakati 29:26-27).

Kwa mapanda ambayo Bwana aliyaamuru kupitia Musa, Daudi aliongeza matoazi, vinubi na vinanda (1Nyakati 15:16; 16:5-6). Mapanda yalipigwa na makuhani na idadi yao ilianzia mawili katika ibada ya kila siku (1Nyakati 16:6; Hesabu 10:2) hadi saba au zaidi wakati wa matukio maalumu (1Nyakati 15:24; Nehemia 12:33-35; 2Nyakati 5:12).

 ‘Wakati wa ibada pale Hekaluni mapanda yaliaashiria kusanyiko la waabuduo kusujudu wakati wa kutoa sadaka ya kuteketezwa na wakati wa kuitikia (Choral service) huduma ikiendelea (2Nyakati 5:12; 7:6).’[18]

 
“Mpangilio huu ulionyesha umuhimu wa wapiga mapanda kutoa ishara kwa ajili ya mkutano kusujudu na kwaya kuimba.[19]
‘Vyombo vya nyuzi vilitumika sana kusindikiza uimbaji kwani vilikuwa havifuniki sauti au maneno ya Yehova yaliyokuwa yakiimbwa.’[20] Uangalifu mwingi ulifanyika ili kuhakikisha kwamba sauti za sifa za kwaya hazikufunikwa na sauti za vyombo vya muziki.[21]

Kusudi hilo hilo la vyombo kusindikiza sauti za waimbaji linapaswa kufuatwa kwa makini leo. Lakini kwa bahati mbaya tena kwa makusudi kabisa vyombo vinapigwa na watu wasio na ujuuzi kabisa kwa sauti ya juu sana na midundo mizito na kufunika sauti za maneno ya sifa zinazotolewa na waimbaji hazisikiki na wala kueleweka. Badala ya waabuduo kutoka katika ibada na Baraka na kicho mbele za Mungu, wanatoka na vichwa vinavyouma na masikio yanayonyita kwa sababu ya midundo na kelele za juu sana za vyombo vya muziki tena vinavyopigwa bila utaratibu wala kicho mbele za Mungu.

Swali linaweza kuulizwa, ‘je tupunguze sauti za vyombo ili midundo isikike kwa chini kabisa? Jibu liko wazi kabisa. Sumu ni sumu tu. Kwamba iko kwenye pipa la lita 100 au ipunguzwe hadi kuwa katika nusu ya kijiko cha chai uwezo wake wa kufiisha uko pale pale. Kama mtu haelewi hata hilo basi na aelewe kwamba kinyesi ni kinyesi tu. Kwamba kimechotwa chooni na kuwekwa na kujazwa kwenye debe au kimewekwa kwenye kijiko cha chai madhara yake ni yale yale. Hivyo ndivyo ulivyo muziki wa midundo. Kwamaba imepigwa kwa sauti ya chini au ya juu madhara yake ni yale yale. Mungu haitaki kwa sababu inafiisha hali ya mtu kuyaelewa na kuyapokea mambo ya kiroho. Inalewesha wale ambao huipenda kiasi cha kwamba hawako tayari kusikia ushauri wowote utokao kwenye neno la Mungu na Roho ya unabii. Inapumbaza na kuilaza akili hata isitamani mafundisho yatokayo kwenye neno la Mungu.
Na izingatiwe kuwa ‘kamwe hakukuwa na vyombo vyovyote vya midundo vilivyoweza kuruhusiwa kusindikiza nyimbo za kwaya ya Walawi ilipokuwa ikitoa huduma ya nyimbo Hekaluni au kundi kubwa la wapiga muziki pamoja (Orchestra) pale Hekaluni (Ezra 3:10; Nehemia 12:27, 36). Waimbaji na vyombo vya muziki pale Hekaluni vilikuwa tofauti kabisa na vile vilivyotumiwa katika maisha ya kila siku ya watu.[22]

Kupitia fani ya muziki, laana na giza limeingia kanisani. Katika ibada nyingi malaika wa Mungu huwa wanaamua kuondoka pindi wanapoona nyimbo za zisizofaa na muzuki wa usiofaa unapoanza kupigwa.

 Mjumbe wa Mungu White anasema:
Mambo ya milele yana uzito kidogo sana kwa vijana. Malaika wa Mungu wanatoa machozi wanapoandika maneno na matendo ya Mkrisito. Malaika wanazunguka zunguka huko na huko. Vijana wamekutanika pamoja, kuna mlio wa sauti na vyombo vya muziki. Wakrisito wamekusanyika hapo, lakini ni nini unachokisikia? Ni wimbo, wimbo wa upuuzi, ufao katika ukumbi wa dansi. Tazama malaika wanaiondoa nuru kutoka kwao, na giza nene linawagubika wote walio katika eneo hilo. Malaika wanaondoka kutoka kwenye tukio hilo. Huzuni ijuu ya nyuso zao. Tazama, wanalia. Hili nililiona likirudiwa mara nyingi katika makundi yote ya watunzao Sabato…muziki ni sanamu ambayo wengi wa Wakrisito wa wanaokiri kuitunza Sabato. Shetani hana kipingamizi kwa muziki kama anaweza kuufanya kuwa njia ya kuyafikia mawazo ya vijana…Vijana wanakutana kuimba, na ingawaje wanakiri kuwa ni Wakristo, mara kwa mara wanamvujia Mungu heshima na imani yao kwa mazungumuzo ya upuuzi na uchaguzi wao wa muziki.[23]

Midundo ya muziki wa lege, jazz, rock za aina zote, na mingineyo, pale tu inapoanza kupigwa, malaika wa Mungu hawabaki hapo tena. Wanaondoka mara moja kwenye mkutano huo. Ni mkutano wa laana huo. Na malaika wa Mungu wakiondoka, mara moja shetani na malaika zake huja na kuchukua nafasi na kuongoza mkutano huo.

Nuru ya Mungu huondolewa kwenye mkutano huo. Giza nene huwafunika hao waliokusanyika kwa ibada mahali hapo. Badala ya kuwa mkutano wa Baraka unageuka kuwa mkutano wa laana kubwa ajabu. Rubani wa mikutano hiyo anakuwa ni ibilisi yule nyoka wa zamani. Je, hapo mahali ambapo ibilisi anongoza, unategemea waimbaji na wapiga vyombo na hasa keyboard wataitikia maonyo yoyote? Kamwe hawawezi kusikia maana roho mchafu wa shetani anakuwa ametawala na kuongoza mkutano huo. Jua wazi kwamba kabla hata malaika wa Mungu hawajaoondoka, Roho Mtakatifu anakuwa amekwisha ondoka zamani. Pepo mchafu anakuwa ametawala mkutano au ibada hiyo asili mia moja. Kwa sababu hiyo kanisa zima linakuwa chini ya chuki ya Mungu kwa sababu tu ya hao wachache ambao wamekataa neno la Mungu bali hufuata mapenzi yao.
Mungu anawaita watu wake kuwa watulivu na wenye msimamo. Wanapaswa kuwa waangalifu sana wasije wakamwakilisha vibaya na kuyavunjia heshima mafundisho makuu ya ukweli kwa njia ya maonyesho ya kigeni, kwa machafuko na makelele. Kwa haya, wale wasioamini wataongozwa kufikiri kuwa Waadventista wa Sabato ni kikundi cha ulokole…wakati waumini wanapohubiri ukweli kama ulivyo katika Yesu, wanadhihirisha utakatifu, utulivu, na sio dhoruba ya machafuko.[24]
Wote tunajua kuwa uimbaji wa kilokole ni wa midundo ya ngoma, kucheza na kurukaruka na sauti ya makelele ya juu sana. Kuna hitaji kubwa kwa mtu yeyote anayeijua kweli kusimama na kukemea uimbaji huu ambao ibilisi ameuingiza katika kanisa la Mungu kwa makusudi ya kuwapoteza watu Mungu yamkini hata walio wateule.
Ulokole, mara unapokuwa umeanza na kuachwa bila ya kuzuiwa, ni vigumu kuuzima kama vile moto ambao tayari unakuwa umeanza kuteketeza nyumba. Wote ambao wameingia katika hali ya ulokole na kukuubali huu ulokole, ni vyema sana waingie katika kazi za kidunia; kwa maana kwa mwelekeo huu wa matendo yasiyo sahihi wanamvunjia heshima Mungu na kuhatarisha watu wake. Mivuto mingi kama hii itainuka wakati huu, wakati ambapo kazi ya Bwana ingeinuliwa, iwe safi, bila ya kuchafuliwa na ushirikina na hadithi. Tunapaswa kuwa waangalifu, kudumisha uhusiano wa karibu pamoja na Kristo, ili kwamba tusidanganywe na shetani. Mungu anataka utaratibu na nidhamu katika huduma yake, sio msisimuko na machafuko. Kwa sasa hatuwezi kuelezea kwa usahaihi matukio ambayo yatatendeka katika ulimwengu wetu huu siku za usoni, lakini hiki ndicho tunachokijua, kwamba huu ndio wakati ambapo tunapaswa kukesha katika maombi; kwa maana siku kuu ya Bwana iko karibu sana. Shetani anaongeza nguvu zake. Tunapaswa kuwa watu makini na watulivu, na kutafakari kweli za ufunuo. Msisimuko haukubaliki kwa kukua katika neema, usafi wa kweli na utakaso wa roho.[25]

Dini ya kilokole imeuteka ulimwengu wa Kikristo na vile vile ulinasi wa kipagani. Sasa pia imeuteka ulimwengu wa Kikristo wa kanisa la Mungu la Waadvnetista wa Sabato. Ni wapi mtu ataweza kwenda asiweze kukutana na uimbaji wa midundo ya muziki na kucheza kwa namna ya kilokole? Nenda katika kanisa Katoliki ambalo miaka ya zamani lilisifika kuwa ma muziki wa dini hasa, nenda katika kanisa la Lutherani ambao walikuwa ni waimbaji mashughuli katika ulimwengu wa Kikristo, Moravian, Anglicana, na kadhalika, utakutana na muziki wa midundo na kucheza na kurukaruka.
 Nenda kweye virabu vya pombe kwamba ni vijijini au mijini utakutana na muziki wa midundo na kurukaruka iliyoimbwa na wale anaojidai kuwa ni Wakristo na ati wanamwimbia na kumchezea Yesu. Walevi waliisha acha miuziki ya wapigaji wa kidunia maana hao hawamdhihaki Yesu na wamegeukia muziki wa upagani mambo kikristo.
 Je, Roho ya Unabii inatoa maagizo gani katika fani ya uimbaji na muziki kwa ujumla?
    “‘Watu wengi, vijana kwa wazee, kwa maneno matamu wanaeleza sababu zao za kutumia muziki bandia…kuwa wanaupenda. Hii ni tabia ya kuogofya. Wavuta bangi wanaweza kutetea matumizi yao ya dawa za kulevya kwa maneno hayo hayo, tunaipenda.’ Je, kusema vile kunaweza kuhalalisha matumizi yao? Je, jema na baya‘Muziki umechukua muda ambao ungetumiwa kwa maombi. Muziki ndio kinyago kinachoabudiwa na wengi wa Wakristo watunzao Sabato. Shetani hapingi muziki wowote ikiwa anaweza kupitia hapo kufikia kwenye mawazo ya vijana. Muziki ukitumiwa vibaya huongoza moyo kuwa na kiburi, upuuzi na upumbavu. Muziki kama huo ni laana ya kutisha.’[26]

   ‘Mara nyingi nimeumia moyoni kusikia sauti kali za juu mno zikiharibu maneno matakatifu ya nyimbo za sifa. Sauti kali zinazokwaruza hazifai kabisa katika ibada yenye furaha mbele za . nilitaka kuziba masikio au kukimbia kutoka mahali hapo.’[27]

‘Muziki unaweza kuwa na uwezo mkubwa sana kwa wema ingawa hatutumii uwezo huo wote upasavyo kama sehemu ya ibaada. Mara nyingi uimbaji hutendwa kutokana na hisia au kukidhi malengo maalum na nyakati zingine waimbaji huachwa kusitasita hatimaye muziki huwa na matokeo mabaya katika mawazo ya wasikilizaji. Lakini wakati mwingine huwa vigumu zaidi kudhibiti waimbaji na kuwa fanya wafuate utaratibu kuliko kuboresha mazoea ya maombi. Wengi wa waimbaji hupenda kufanya vitu katika mitindo yao wenyewe, hukataa kushauriwa wala hawavumilii kutawaliwa.’[28]

‘Mazoea mabaya na mwelekeko wa dhambi hutiwa nguvu na kuimarishwa na burudani hizi. Nyimbo za dunia, kuyumbisha sehemu fulani za mwili kunakoashiria hisia za msisimko wa mapenz, maneno na mwelekeo mwovu uaathiri mawazo na kushusha maadili. Kila kijana mwenye mazoea ya kuhudhuria matamasha kama hayo tabia zao huchafuliwa. Katika nchi yetu [Marekani] hakuna kitu kingine chenye mvuto mkubwa kinachotia sumu mawazo yanayoharibu moyo wa kupenda mambo ya kiroho na kupunguza hamu ya utulivu na furaha ya kweli maishani kama tamasha la burudani.’[29]

‘Shetani anaelewa ni kiungo gani cha mwili cha kushitua ili mwili wote usisimke na kuchangamsha akili kisha Kristo hatamaniki tena moyoni.[30]

‘Muziki mbaya hujaa lugha isiyoeleweka na sauti zisizolingana. Mungu hapendezwi na mvurugano.’[31]

‘Nawezaje kuvumilia fikira hii ati “wengi wa vijana wetu wa kizazi hiki hawatafikia uzima wa milele. Oh! Ningalipenda kuwa hizo sauti za vyombo vya muziki zikome ili vijana wasiendelee kutumia muda wa thamani kubwa kwa kujifurahisha tu.[32]

Malaika wanavinjari karibu na nyumba ambamo vijana wanakutana. Kuna mvumo wa sauti za vyombo vya muziki. Wakriso wanakutana pale, lakini unasikia kitu gani pale? Ni nyimbo za pambio za kipuuzi tu zisizositahili kuimbwa katika ukumbi wa ibaada. Tazama malaika watakatifu hukunja mbawa zao karibu nao, ndipo wale walio nyumbani hufunikwa gizani, kasha malaika huondoka pale, nyuso zao zikijaa huzuni, wanalia. Haya niliyaona mara nyingi yakitokea kati ya makundi ya watunzao Sabato.’[33]

Katika uzoefu wa wale ambao maisha yao hutawaliwa na nyimbo za “pop”, “Regge”, nk. Swala la mema na mabaya hufikiriwa juu juu tu.’[34]

‘Muziki mbaya huimbwa na kwaya za kidunia ambazo hutegemea kupata fedha.’[35]

‘Kujionyesha sio dini wala utakaso. Hakuna kinachomchukiza Mungu kulko muziki ambao unaotolewa na vyombo wakati ambapo wanaopiga vyombo hivyo hawakujitoa kamili kwa Mungu.’[36]

‘Mtindo wa mavazi yavutiayo sana, nyimbo zisizo fuata taratibu za maadili ya uimbaji, hazikaribishi kwaya za malaika wa mbinguni makanisani namachini pa Mungu, vitu hivi vyote ni matawi ya mtini usiozaa matunda bali majani mabichi tu.’[37]




[1] Samuele Bacchocch, The Chrsitian and the Rock Music: A Study on Biblical Principles of Music, ‘Biblical Principles of  Music, p. 193.
[2] Samuele Bacchiocchi,  The Christian and the Rock Music: A Study on Biblical Pricinciples of Music, Biblical Pricnicples of Music, pp 194-5 cf. Bible Works; Benjamin Davidson, The Analytical Hebrew and Chaldee Lexcon (Grand Rapids, Michigan: Zondervan Publishing House, 1993), p. 679
[3] Samuelle Bacchiocchi, p. 223.
[4] King James Version, The Study Bible Presenting The Old and The New Testament in the E.G. White Scripture  Comments (Maryland: Review and Herald Publishing Association, 1993), p. 670.
[5] Rosalie H. Zinke, Adult Teachers Sabbath School Bible Study Guide: Worship in the Psalms, Lesson 7, p. 77.
[6] Benjamin Davidson, The Analytical Hebrew and Caldee Lexicon (Grand Rapids, MG: Zondervan Publishing House, 1993), p.394.
[7] Ellen G. White, Selected Messages (3Vols, Washington, D.C.: Review and Herald Publishing Association, 1958), vol. 2, p. 36.
[8] Ellen G. White, Selectd Messages, vol. 2, p. 37, 38.
[9] Ellen G. White, Selected Messages 93vols, Washington, DC: Reviewe and Herald Publishing Association, 1958), vo. 2, pp. 36-37.
[10] Ellen G. White, Selected Messages, vol. 2, p. 37.
[11]Ellen G. White, Testimonies for the Church (9Vools, Cal: Pacific Press Publishing Association, 1948), vol. 1, p.457
[12] Samuele Bacchiocchi,  The Christian and the Rock Music: A Study on Biblical Pricinciples of Music, Biblical Pricnicples of Music, pp 194-5 cf. Bible Works; Benjamin Davidson, The Analytical Hebrew and Chaldee Lexcon (Grand Rapids, Michigan: Zondervan Publishing House, 1993), p. 679
[13] Ellen G. Whtie, Evangelism, p. 505
[14] Samele Bacchiocchi, The Christian and the Rock Music: A Study of Biblical Priinciples of Music, Biblical principles of Music, p. 198.
[15]Samuele Bacchiocchi, The Christian and the Rock Music: A Study on Biblical Principle of Music, Biblical Principles of Music, p. 201-2.
[16] Ellen G. Whtie, Evangelism, p. 505
[17] Samuelle Bacchiocchi,  p. 206
[18]John W. Kleinig, p. 80 (Samuelle Bacchiocchi p. 206).
[19] Samuelle Bacchiocchi, p. 206.
[20] Garen L. Wolf, Music of the Bible in Christian Perspective (Salem, OH, 1996), p. 287 cf. Samuelle Bacchiocchi, p. 207.
[21] Samuelle Bacchocchi, p. 207.
[22] Samuelle Bacchiocchi, p. 208.
[23] Ellen G. White, Testimonies for the Church (9Vols, Cal. : Pacific Press Publishing Association, 19480, VOL. 1, 506.
[24] Ellen G. White, Selected Messages, vol. 2, p. 36.
[25] Ellen G. White, Selected Messages, vol. 2, p. 35.
[26] Ellen G. White, Testimonies for the Church (9vols, ), vol. 1, p. 506.
[27] Ellen G. White, Evangelism, p. 508.
[28] Ellen G. White, Evangelsim, pp 507-8
[29] Ellen G. White, Testimonies for the Church (9vols, ), vol. 4, p. 653.
[30] Ellen G. White, Testimonies for the Church (9 vols,  ), vol. 1, p. 497.
[31] Ellen G. White, Evangelism, p.510.
[32] Ellen G. White, Testimonies for the Church (9vols,  ), vol. 2, p. 144.
[33] Ellen G. White, Messages to Young People, p. 97, 297.
[34] Review and Herald, Decewmber 2, 1972.
[35] Ellen G. White, Evangelism, p. 509.
[36] Ellen G. White, Evangelism, p. 510.
[37] Ellen G. White, Evangelism, p. 511.