Waweza Kuishi na Yesu, lakini huwezi kuishi bila Yesu.Yohan 3:16



JINSI MAJASUSI WALIVYOANZISHA MATUMIZI YA VIDONGE
Utumiaji wa vidonge ulianzishwa na majasusi , ili kutengeneza faida
bila kujali kwamba vidonge ni sumu kwa afya ya mtumiaji.

    

    
Miaka ya 1930, Morris A. Bealle aliyekuwa mhariri wa zamani gazeti la Washington Times and Herald nchini marekani,alikuwa msimamizi wa gazeti maarufu ambalo liliingiza mapato makubwa sana kwa matangazo ya Kampuni ya nishati kila wiki.

Katika mapato yaliyokuwa yakikusanywa mwisho wa mwezi, kampuni hiyo ilionekana kama tegemeo kubwa la gazeti hilo.
Siku moja habari za malalamiko ya wananchi dhidi ya huduma mbovu za kumpuni hiyo yalianza kuandikwa na gazeti hilo.

Bealle,  alipata vitisho,vikali kutoka kwa kampuni iliyotengeneza matangazo ya kampuni hiyo ya nishati kuambiwa kama ataendelea kuandika habari “zilizo nje ya mfumo”  wa kampuni hiyo, si kwamba ataondolewa katika mkataba wa matangazo tu, bali kusitishwa katika huduma za kampuni ya gesi na ya huduma za simu.

Hapo ndipo macho ya Bealle yalifunguka kuhusu “uhuru wa vyombo vya habari”,hatimaye akaacha kazi kwasababu alikuwa na uwezo mzuri kiuchumi.

Kupitia uzoefu wake kitaaluma aliamua kufanya utafiti kuhusu uhuru wa vyombo vya habari na kuja na tafiti kuu mbili
1.   Habari kuhusu Vidonge (The Drug Story)
2.   Nyumba ya Rokifila. (House of Rockefeller)

Kitabu kilichofunua siri kali ,jinsi jamii ya siri ya Majasusiwalivyosambaza
 utumiaji wa madawa ya kisasa (vidonge)ambayo ni hatari kwa afya
 yamwanadam



Pamoja na uzoefu katika ulimwengu wa uhariri  hakuweza kuandika mafunuo yake mpaka alipoanzisha kampuni yake binafsi iliyoitwa Idara ya uchapishaji –Kolombia, Washinton D.C.,mwaka 1949.

Pamoja na kitabu cha Habari kuhusu Vidonge  kuwa katabu cha pekee katika masuala ya Siasa na Afya nchini Marekni, kamwe hakijawahi kupelekwa katika maktaba kuu za vitabu wala kuzungumziwa katika magazeti ya marekani.
Kwa upande wa uuzaji , kitabu hiki pekee kiliuzwa kwa njia ya mizigo iliyosafirishwa kupitia shirika la Posta. Pamoja na hayo , kitabu hiki baada ya kuingia sokoni katika toleo lake la 33 kilikuwa kikitoka katika lebo tofauti kama vile Biworld Publishers, Orem na Utah

Baelle alibainisha kuwa kwa miaka 1960, biashara iliyoingiza faida asilimia sita (6%), ilikuwa ni biashara kubwa sana.

KAMPUNI YA JAMII YA SIRI (MAJASUSI) ILIYOITWA NGOME YA MADAWA YA ROKIFILA (The Rockefeller Drug Empire) iliingiza faida Dolla za marekani Milioni 23.4 baada ya kulipa Kodi katika mali za thamani ya Dola milioni 43.1. sawa na asilimia hamsini na nne (54%) .
Kampuni ya Skwibu (Squib) amayo pia iko chini ya  Rokifila (Kampuni ya majasusi) iliingiza faida ambayo si asilimia 6 bali asilimia 576 (576%) katika thamani
Faida hii ilitokana na juhudi za Daktari mkuu wa Upasuaji  , ofisi ya Jemedari wa jeshi pamoja na Taasisi ya Madawa Na Upareshei ya Navi (Navy Bureau of Medicine and surgery)   Taasisi hizi hasikuwa tu  zikihimiza wattu watumie vidonge, lakini walilazimisha  sumu za vidonge katika damu za Wanajeshu wa Marekani , wasafiri wa majini na mabaharia.
“Je ni ajabu , kwamba Rokifila, na vitengo vyao vya vya biashara (mbovu) ya vyakula na madawa, Jumuiya ya Afya Ulaya, Taasisi Kuu ya Biashara,  Taasisi ya Madawa ya Navi, na maelfu ya maafisa wa dawa nchi nzima , kuunganika na kupinga aina zote za tiba zipingazo matumizi ya vidonge?” Aliuliza baelle.
Baelle aliendelea kubainisha kwamba katika kipindi hicho “Ropoti ya mwisho wa mwaka ya Faundesheni ya Rokifila”, ilionyehsa zawadi (tuzo) ilizotoa katika vyuo na taasisi za umma katika miaka 44 iliyopita, thamani yake ilizidi dola nusu bilioni.
Vyuo hivi vilianza kufundisha ujuzi wa kutumia madawa ambayo Famasi za Rokifila zilihitaji ufundishwe.  Tofauti na hapo hukukuwa na tuzo, kama vile vyuo visivyo vya kawaida 30 katika jumuiya ya Ulaya vilivyokosa tuzo kwa kutofundihsa tiba zilizoegemea katika utumiaji wa vidonge.
Baadhi ya vyuo maarufu vilivyopewa fedha na kampuni hii ya Kijasusi ili kuhimiza utumiaji wa madawa ya kisasa ni:
·       Havadi, pamoja na shule yake ya Tiba ambayo maarufu sana , ilikuwa imepokea  Dola Milioni 8.7 kutoka Taasisi ya Fedha za Madawa ya Rokifila.(Rockefeller’s Drug Trust Money )
·       Yale, chuo kilipewa Dola Milioni 7.9
·       John Hopkinss, kilipokea Dola Milioni 10.4
·       Chuo Kikuu  cha Washintoni huko Mt.Louis, kilipewa Dolla Milioni 2.8
·       Chuo Kikuu cha New York Kolombia , kilipewa Dola Milioni 5.4
·       Chuo Kikuu cha Korneli , kilipokea Dolla Milioni 1.7 n.k
Pamoja na “kugawa” vitita vya fedha kwa vyuo vilivyosambaza propaganda za utumiaji wa vidonge , madhumuni ya Rokifilla yaliendelea kukua katika mtandao wa dunia nzima kuliko mtu yeyote awezavyo kugunda.
Kwa zaidi ya miaka 30, ilikuwa ni kiasi cha kutosha kwa Baelle kugundua Makusudio yaliyoanzishwa na Rokifila, na kuendelezwa katika Kampuni kubwa isiyoweza kufikiriwa namwanadam.
Rokifila inamiliki jumuiya kubwa ya kuzalisha madawa ya kisasa Duniani kote, na hutumia madhumuni yao mengine yote kukuza uuzaji wa madawa. Ukweli kwamba zaidi ya aina 12,000 za madawa tofauti (ya kisasa) katika soko ni sumu, si wazo la wazalishaji wa madawa...
Itaendelea...


MBINU ZA IBILISI KUONDOA MATENGENEZO KWA WAKRISTO
Shabaha Kubwa Ya ibilisi ni kuwaondoa watu katika Utii wa neno la Mungu
kwasababu kutii Biblia ni kiini cha matengenezo, na utakaso . Yohana 17:17. 


Katika biblia, Yuda 1:3 Biblia yasema tuipiganie imani waliyokabidhiwa watakatifu mara Moja...


Miongoni mwa mambo makubwa aliyhoyafanya Ibilisi, ni kuondoa hali ya matengenezo kwa watu wa Mungu, zifuatazo ni agenda kuu kumi zilizoandaliwa na jamii za siri ili kuwafanya Wakristo wabweteke , na kuachana na juhudi ya kufanya matengenezo. 

Mambo aliyopangilia Ibilisi kupitia kikao cha siri, kama utakavyoyasoma utagundua kwamba ni udhihirisho katika yale yaendeleayo miongoni mwa Wakristo wengi.

Hizi ni agenda za kikao cha siri

  1. Kuzusha magombano baina ya waombezi ili kuwavunja wasiendelee kumtafuta Mungu wao.
  2. Sababisheni hadithi kwa wingi watakapoingia ndani ya makanisa yao wakati wa kuja kumuomba Mungu wao.
  3. Msiwaruhusu kuomba wakati wa kulala kwao (Janatus) maana hamuwezi kuwaona wakifunikwa na nguvu za Mungu wao.
  4. Msiwape nguvu au nafasi ya kusoma Biblia, baadala yake wapeni wakati mwingi wa kusoma magezeti na kuangalia televishini zao.
  5. Sababisheni ufukara, mateso na pesa zao kupotea bila wao kujua ili wasimtolee Mungu wao, na walio na pesa roho ya ubahili ya kutokutoa.
  6. Inueni nguvu za kuzimu makanisani kwao baina ya viongozi na washirika wao na vijana kwa wasichana ili kupata nafasi ya kuzima nguvu zao.
  7. Ibada zao ziwe baridi kabisa ili Roho wa Mungu wao asipate nafasi ya kuongea na kusikia kutoka kwake.
  8. Tumieni ajali maana damu yao tutaitumia katika vikao vyetu.
  9. Akina mama wajawazito wazalishwe kwa operesheni ili kupata damu.
  10. Tumieni Ukimwi wa kutengeneza kama pigo kwao ili kuwamaliza na kuwaletea aibu katika vifo vyao.
  11. Vurugeni umoja wa nyumba zao kati ya mke na mume, wazazi na waatoto wao ili maombi yasipatikane.
Hayo ni Baadhi ya Mambo yhaliyoorodhesha katika barua ya kikao hicho.

Ukristo ni gharama, kujikana nafsi. Je katika hayo ni lipi ambalo walitenda na kumpatia mwanya Ibilisi katika maisha yako? 

Habari njema ni kwamba , ukimtegemea Yesu kwa moyo wote bila kujichanganya na mabo ya dunia ,kwake ushindio ni wa Lazima. 

Yohana 3:16 Kwa maana jinsi hii Mungu aliupenda ulimwengu, hata akamtoa mwanawe pekee, ili kila mtu amwaminiye asipotee, bali awe na uzima wa milele. 

Biblia izungumziapo Mbinu za ibilisi dhidi ya wale wamtegemeao Yesu huishia na kauli ya ushindi , hii ni kutokana na Ukweli kwamba KUPITIA KIFO CHA YESU PALE MSALABANI IBILISI ALINYIMWA UWEZO DHIDI YA WOTE WAMTEGEMEAO YESU

Ufunuo 12:11. Nao wakamshinda kwa damu ya Mwana-Kondoo, na kwa neno la ushuhuda wao; ambao hawakuyapenda maisha yao hata kufa.



KUFUNGA, IBADA ISIYOKWEPEKA KWA

 MKRISTO

“Akafunga siku arobaini mchana na usiku , mwisho akaona njaa. Mjaribu akamjia akamwambia , Ukiwa ndiwe mwana wa Mungu, amuru kwamba mawe haya yawe mkate.” Mathayo 4:2,3
“Baadhi wamekweza kitendo cha kufunga kuliko maandiko yote na makusudi; japokuwa , wengine wamepuuzia kitendo hicho.” John Wesley.
KWANINI MUNGU ALILETA WAZO LA KUFUNGA
Kwa Yesu, kama vile kwa ndoa takatifu pale Edeni, tamaa ya chakula kilikuwa ni kigezo cha jaribu kubwa la kwanza. Pale anguko lilipoanzia, kazi ya ukombozi wetu lazima ianzie hapo. Kwa kuendekeza tama ya chakula Adam alianguka, kwahiyo kwa kuikana tamaa ya chakula Yesu lazima ashinde anguko. “Akafunga siku arobaini mchana na usiku , mwisho akaona njaa. Mjaribu akamjia akamwambia , Ukiwa ndiwe mwana wa Mungu, amuru kwamba mawe haya yawe mkate.”[1]

JE BIBLIA HUONYESHA KUWA KUFUNGA NI LAZIMA AU UAMUZI.
Japokuwa Biblia haijaonyesha kuwa kufunga ni amri, huonyesha kuwa kufunga ni suala litarajiwalo kwa mfuasi makini wa Mungu .Katika Mathayo 6:17-18 husema “ufungapo” Ysu hakusema “kama ukifunga” badala yake akasema “ufungapo” ili kuonyesha kwamba anatarajia tufunge na kuomba kama kama wafuasi wake.
Kwa nfuasi wa Yesu, swali la kujiuliza si kwamba Je naweza kufunga bali Je nitafunga, na kama nikifunga nifunge vipi?
“Siwezi kusaidia bali kushangaa kwamba matukio makubwa hayawezi kutokea kwasababu tunapuuzia kufunga” K. Neill Foster

Katika biblia suala la kufunga na kuomba, hutajwa mara nyingi sana japokuwa uelewa wa watu kuhusu suala hili nyeti umekuwa ni tofauti na limepuuziwa kuliko Mungu alivyolipa uzito wa Kiroho .Kumekuwa na dhana potofu kuhusiana na ibada ya kufunga.
  • Wapo wadhanio kwamba kufunga ni kuacha kula matokeo yake wanashinda na njaa badala ya kufunga.
  • Wengine hudhani kwamba kwa kuacha kula wanaongeza nafasi ya kupata upendeleo kwa Mungu ili awajibu maombi yao.

Lakini swali bado linabakia:
  • Nini maana ya kufunga?
  • Kwanini maombi ya kufunga husisitizwa sana katika biblia?
  • Kufunga kuna faida gani?
  • Hivi kuna mambo ambayo hatuwezi kuyapata bila kufunga?

Hayo na mengine mengi yatajibiwa katika somo hili “Kufunga na maajabu yake kiroho”

KUFUNGA HUMAANISHA NINI?

Kufunga , ni neno lililotokana na neno la limaanishalo kuacha kula chakula, eidha kwa madhumuni ya kidini au kwasababu ya ukosekanaji wa kiebrania \suÆm, chakula, au kipindi cha kufanya jambo hilo.[2]
Kufunga humaanisha kuweka kando starehe yoyote ile au shughuli ya muhimu kwa kipindi fulani ili kumtafuta Mungu kwa juhudi.

Hapa jambo la msingi tutakaloliangazia ni kufunga kwaajili ya maombi katika Biblia, suala la kufunga huonekana pote katika biblia kuanzia agano la kale hadi agano jipya.

  1. Musa alifunga siku 40 mara mbili hadi uso wake ukabadilika na kuangaza utukufu wa Bwana. (Kumbukumbu la Torati 9:9,18)
  2. Yoshua alifunga baada ya ushindi pale AI.(Yoshua 7:6)
  3. Daudi alifunga kabla ya kuteuliwa kuwa mfalme, wakati mwanae ailpougua, na kwasababu ya dhambi za watu wote (Zaburi 35:13; 69:9-10)
  4. Yehoshafati na watu wake walifunga mpaka Bwana akasema hawatapigana vita  hatimaye wakashinda vita kwa kufunga na kuomba tu (2 Mambo ya Nyakati 20:17)
  5. Danieli alifunga na kuomba mpaka Gabrieli akagizwa kumfariji na kumpatia majibu ya njozi ambayo hakuielewa. (Danieli 9:3,21-23)
  6. Yesu alifunga siku 40 na kupata nguvu ya kumshinda majaribu shetani kwa niaba ya mwanadamu na kuukomboa ulimwengu.

“Kwa Mkristo kufunga si suala la uchaguzi bali la msini.
Ushahidi wa vielelezo hivyo ni udhihirisho kwamba
    • Mungu hupendelea sana watu wamwelekeao kwa maombi wafunge ili kuwa karibu na yeye zaidi.
    • Kuna mambo ambayo wafuasi wa Mungu hawawezi kupata bila kufunga na kuomba kama vile imani. (Mathayo 17:21)
    • Mungu aliona kufunga ni jambo lisilokwepeka kwa kila mfuasi wake kiasi cha kulizungumzia sana katika biblia.
    • Hakuna ushindi wa Dhambi Bila kufunga na kuomba.

Pamoja na wengi kujua umuhimu wa kufunga na kuomba , bado utata umebakia katika namna ya kufunga na kuomba, wapo ambao kiukweli hufunga na kuomba huku wengine hushinda na njaa wakidhani kwamba wamefunga na kuomba. Ili kujua kuwa umefunga sawa na maagizo ya biblia, wapaswa kuelewa maana halisi ya kufunga.

KUFUNGA KULIKO SHAHIHI
  • Kufunga humaanisha kuweka akili na Moyo kwa Mungu na sio katika chakula. “Roho ya kufunga kwa kweli na maombi ni roho iwekayo akili na moyo kwa Mungu[3] Pia humaanisha “kufikiria sana chakula kutoka mbinguni kitakacotoa nguvu na uwezo katika uzoefu wa kidini[4]

“Mfungaji aachapo chakula, ubongo haushughuliki tena na jukumu la kumeng’enya au kufikiria chakula bali unamuelekea Mungu.”

  • Hitaji la Kiroho na vita ya kiroho , kusudi lako la kupatana na Mungu ni zito kiasi  kwamba umeamua uachane na mahitaji ya kimwili ili ujitoe katika maombi na kutafakari. (Zaburi 1:1) Hili ni kutokana na ukweli kwamba kati ya mambo yafanyayo tushindwe kumtafakari Mungu vizuri ni uroho na tama ya ya chakula (kukosa kiasi katia ulaji.)

MBINU SaHIHI ZA KUFUNGA
KAMA tulivyoona kufunga ni kuacha kula kwa madhumuni ya kidini, hii humaanisha kwamba kufunga hakuishii kuacha kula peke yake, bali ni kudhiirisha kwamba Hitaji lako kwa Mungu ni zito kuliko mahitaji uyapenadayo(mf chakula, usingizi n.k). Kwa ukweli huo, zifuatazo ni namna tofauti za kufunga:

  • Kuacha vyakula vya kusisimua (stimulants). “Kufunga kwa kweli kushauriwako kwa wote , ni kuacha kila chakula cha kusisimua, matumizi sahihi ya chakula rahisi, cha lishe ambacho Mungu ametoa kwa wingi. Watu wapaswa kufikiria kidogo kwamba ni nini watakula na kunywa katika chakula cha kupita, na wafikirie zaidi chakula kutoka Mbinguni.[5]
  • Kujinyima (kufunga) usingizi, kujinyima usingizi humaanisha hitaji la kiroho ni zito kuliko usingizi. Mara kadhaa Yesu alijinyima usingizi na kukesha katika maombi, waweza kufunga kwa kuacha kulala kwa sababu zilezile za kuacha kula. (Luka 6:12)

Yakobo katika Mto Jabok alijinyima usingizi usiku kucha akiomba hatimaye ombi lile aliloomba kwa miaka ipatayo 20 likajibiwa usiku ule.

  • Kujitenga na wale au vile uvipendavyo , kuna wakati ambapo waweza kujitenga na ndugu, familia na mazingira uyapendayo sana ili kukutana na Mungu tu. Waweza kwenda mlimani au sehemu ya upekee ili umtafakari Mungu bila muingiliano na jambo lolote. Kuna wakati Yesu alijitenga na jamii (Mathayo 14:23)
  • Kula kidogo chakula rahisi , “Sasa na kuendelea mpaka mwisho wa wakati watu wa Mungu wapaswa kuwa makini sana, wawe macho zaidi, wasitegemee hekima zao wenyewe…Watenge siku kwaajili ya kufunga na kuomba. Kuacha kula kabisa kwaweza kusihitajike, lakini wale kwa kidogo (sparingly) chjakila rahisi.[6]
  • Waweza kuacgha kula kabisa na kunywa, waweza kuacha kula tu ukanywa maji, waweza kuacha chakula ukala matunda.Kwa ujumla kufunga ni kuacha yote tuyapendayo katika dunia hii (vyakula,kazi, matamanio) kwasababu twaelekeza akili katika ulimwengu mwingine  (Mbingu).

AINA ZA KUFUNGA ZIPATIKANAZO KATIKA BIBLIA
  • Kufunga kwa kawaida(Normal Fast), huku ni kuacha vyakula vya aina zote na kunywa maji tu.
  • Kuacha kula kabisa (Absolute Fast) ,ni aina ya kufunga ambapo mfungaji huacha kula na kjunywa kabisa I Wafalme 19:7-10

  • Kufunga kidogo (Partial Fast) , huambatana na kuacha kula vyakula ambavyo wapendelea kuvitumia. Danieli na wenzake walifunga hivi kwa kunywa maji na mtama tu kwa siku kumi.Danieli 1:15. Wakati mwingine danieli alifinga hivi wiki tatu. Danieli10:3.

“Kufunga kwa aina zote tatu kunakubalika mbele za Mungu jambo la msingi ni kuelekeza akili kwa mungu pekee wakati wa mfungo”

YAPO MAMBO AMBAYO KAMWE  HATUWEZI KUFANYA BILA KUFUNGA.
  • Tiba dhidi ya baadhi ya magonjwa, “kula bila kiasi husababisha magonjwa, na asili huhitaji zaidi kupumzishwa kutoka katika mzigo mzito ambao umebebeshwa. Katika matatizo mengi ya magonjwa, tiba ya pekee ni mgonjwa kufunga mlo mmoja au miwili. [7]  
“Wapo wawezao kunufaika zaidi kwa kuacha kula siku moja au mbili kila wiki kuliko …ushauri wa kitabibu. Kufunga siku moja ya wiki kwaweza kuwa ni faida isiyokifani kwao.”[8]   
  • Kuishinda dhambi, “Yesu aliingia katika jaribu juu ya suala la tama ya chakula, na karibia wiki sita alishinda jaribu kwa niaba ya mwanadam. Kule kufunga kurefu katika nyika ni fundisho wakati wote kwa mwanadam aliyeanguka dhambini…Alitoa fundisho mkwa mwanadam kwamba ataanza kazi ya kushinda pale anguko lilipoanzia, katika suala la tama ya chakula.[9]
  • Kuelewa maandiko. “Kuna baadhi ya maandiko na mambo ambayo ni magumu kuelewa…Muda utafika chini ya upaji wa Mungu kwa dunia kujaribiwa kwa ukweli wa wakati huo, akili zitafanyiwa mazoezi kwa Roho Yake ya kuchunguza maandiko hata kwa kufunga na kuomba …kila ukweli unaohitajika haraka kwa wokovu utawekwa wazi kiasi kwamba hakuna atakayehitaji kukosea...[10]
  • Kupata majibu kwa maombi, kuomba pekee hakutoshi kupata majibu kwa mahitaji yote bali baadhi ya mambo hujibiwa kwa njia ya kufunga na kuomba. “Kwa baadhi ya mabo , kufunga na kuomba hushauriwa na ni sahihi.Katika mkono wa Mungu ni njia ya kusafisha moyo na kuhamasisha…mfumo wa akili. Tunapokea majibu kwa maombi yetu kwasababu tumenyenyekeza mioyo yetu kwa Mungu”[11]
  • Maombi ya kufunga pekee yaweza kuwaokoa waliotekwa katika umizimu, “baadhi ya roho zilizoshangazwa na maneno ya kuvutia kutoka kwa walimu wa umizimu, na kufuata msukumo wake, baada ya hapo wakatambua tabia yake ya mauaji, wataacha na kuukimbia, lakini hawataweza.Shetani kawashikilia kwa nguvu zake, na hayuko tayari kuwaachia huru…shetani atawaimarisha malaika wake waovu ambao wamewaendesha watu hawa, lakini kama watakatifu wa Mungu wakifunga na kuomba kwa moyo wa dhati maombi yao yatashinda.Yesu atatuma malaika watakatifu kumpinga shetani...[12]
  • Kutambua mapenzi ya Mungu katika mipango yetu, “kuna nyakati ambapo mkristo anahitaji umakini wa mawazo na uamuzi madhubuti, aweza kuwa na maamuzi muhimu ya kufanya, au anahitaji kutambua zaidi mapenzi ya Mungu. Katika mazingira hayo kufuka kutathibitisha mbaraka mkubwa.kufunga huko kwaweza kusiwe kuacha chakula kabisa, lakini mlo uloandaliwa na virutubisho rahisi kwaajili ya kuendeleza afya na nguvu… (Dan 10:3, Matt. 6:16.)[13]

MAMBO YA KUZINGATIA KUHUSU KUFUNGA
  • Hatupaswi kufunga kwa kujionyesha kwa watu, “kama mtu anafunga ni suala lake binafsi. Kwakweli, msingi wa kufunga ni utambuzi wa hitaji binafsi wa kufanya hivyo.Fundisho la Yesu ni kwamba kufunga kunapaswa kuwa uzoefu binafsi unaofanywa kwasababu ya utambuzi wa hitaji, na sio…kujipatia sifa ya umahiri…”[14] Kufunga ni njia ya kumtafuta mungu na kusogezwa karibu naye
  • Hatupaswi kufunga kama desturi, wapo wanaofunga ili kutimiza wajibu au kutekeleza tu ratiba Fulani na sio kutokana na hitaji, msukumo wa kiroho uletwao na shauku ya kutaka kuwa karibu zaidi na Mungu. Usifunge kwa kufuata tu ratiba iliyopangwa ,huko ni kushinda na njaa, hata kama kuna ratiba sharti uwe na shauku na msukumo wa dhati kufanya hivyo. Kufunga si tendo la neema kwa lenyewe tu, bali lifanywapo katika moyo wa upendo, hitaji na kujitoa huwa mbaraka.
  • Usichukulie kufunga kama kitendo cha kupata upendeleo kutoka kwa Mungu, wengine hudhani akifunga Mungu atasikiliza ombi kwa makini zaidi wanasahau kwamba sikio la mungu liko wazi siku zote.
  •  Kufunga ni kwaajili ya kubadilisha hali zetu na kutubadili sisi, sio kumbadilisha Mungu. (Isaya 58:1-9).
  • Kufunga si mbadala wa utii, wana wa Israeli walizingatia sana kufunga wakapuuzia majukumu yao kiroho na kimwili wakidhani kwamba kufunga kungemfanya Mungu apuuzie Dhambi zao walizoendelea kuzitenda.(Isaya 58:1-11) Mungu aliwadhihirishia kuwa pamoja na kufunga pia huzingatia utii na kujitoa.


“Maombi ya kufunga ni silaha pekee kwa kila mkristo  kwa maana Ukristo ni kuenenda kwa Imani sio kwa kuona tu, na pasipo Imani haiwezekani kumpendeza mungu, na Imani ya kushinda vita ya kiroho hupatikana kwa kufunga pekee.”



[1] Ellen G White.(1898) Tumaini la Vizazi Vyote,uk 117,118.

[2] Horn, Siegfried H., Seventh-day Adventist Bible Dictionary, (Washington, D.C.: Review and Herald Publishing Association) 1979.
[3] Ellen G White(1938) . Counsels on Diet and Foods
[4] Ellen G White (1932). Medical Ministry
[5] Ellen G White(1932) . Medical Ministry,pg 283
[6] Ellen G White (1904) Review and Herald.
[7] Ellen G White (1905) Ministry of Healing.pg 134
[8] Ellen G White (1902) Testimornies for the Church.vol7.pg 134
[9] Ellen G White(1938) . Counsels on Diet and Foods.pg 186
[10] Ellen G White (1870) Testimornies for the Church.vol 2.pg 692
[11] Ellen G White(1938) . Counsels on Diet and Foods. pg 187
[12] Ellen G White (1855-1868) Testimonies For The Church. vol 1, pg
[13]Nichol, Francis D., The Seventh-day Adventist Bible Commentary, (Washington, D.C.: Review and Herald Publishing Association) 1978.
[14]Nichol, Francis D., The Seventh-day Adventist Bible Commentary, (Washington, D.C.: Review and Herald Publishing Association) 1978.

NJIA TATU ZINAZOELEKEA  MBINGUNI

 JE ZOTE ZINAFIKA?

(1) IJUMAA :- WANAYOPITA WAISLAMU
(2)JUMAMOSI – WANAYOPITA WAADVENTISTA – WASABATO
(3)JUMAPILI – MADHEHEBU ZOTE ZA JUMA PILI?

Je , Mungu anazikubari zote?
Zakaria 12:6 “Siku hiyo itawafanya wakuu wa Yuda kuwa kama Kigae chenye  moto katika kuni na kama kinga cha moto katika miganda ; Nao watatekeleza watu kila kabila wazungukao pande zote, upande wa mkono wa kuume na upande wa mkono wa kushoto ; Na baada ya hayo Yerusalem utakaa mahali pake, naam Hapo Yerusalem”

-          Njia ya kwanza Jumamosi (sabato):- ilianza kupitika  mnamo tarehe ya 7/1/1 wa uumbaji Mwanzo 2:1-3 “Basi mbingu na Nchi zikakamilika . Na siku ya saba Mungu alimaliza akaibariki siku ya saba akaitakasa kwa sababu katika siku hiyo Mungu alistarehe” (mwanzo – 2: 1- 3)
-          Yuda 1:3 Njia hii ilitolewa Mara moja tu. “Wapenzi nilipokuwa nikifanya bidii kuwaandikia habari ya wokovu ambao ni wetu sisi sote, naliona imenilazimu kuwaandikia ili niwaonye kwamba Muishindanie imani waliyokabidhiwa watakatifu mara moja tu. (Yud 1:3) Imani hii ilitolewa na Mungu mara moja “kama mlivyoitwa katika tumaini moja la mwito wenu. Bwana mmoja, imani moja, ubatizo mmoja. Mungu mmoja naye ni Baba wa wote, aliye juu ya yote na katika yote na ndani ya yote. (Efe. 4: 4 – 6). njia ya kwanza ni sabato (jumamosi) ambaye mwanzilishi wake ni Yesu kristo “Akamwambia sabato ilifanyika kwa ajili ya mwanadamu . Basi mwana wa Adamu ndiye bwana wa sabato pia. “Marko 2:27-28) yeye huyu Yesu anao uhakika wa kuwafikisha watu mbignuni ndio maana anasema “Msifadhaike mioyoni mwenu; Mnamwamini Mungu niaminini na mimi, Nyumbani kwa Baba yangu mna makao mengi kama si hivyo ningaliwaambia; maana naenda kuwaandalia makao. Basi mimi nikienda na kuwaandalia makao nitakuja tena niwakaribishe kwangu ili nilipo mimi nanyi muwepo. (Yoh. 14:1-3) “Yesu akamwambia Mimi ndimi njia na kweli na uzima mtu haji kwa Baba ila kwa njia ya mimi. (Yoh14:6.) Hivyo anawaalika wote kupita katika njia hii. “Na kondoo wengine ninao ambao si wazizi hili, Na hao nao imenipasa kuwaleta na sauti yangu wataisikia; kisha kutakuwako na kundi moja na mchungaji mmoja (Yoh 10:16) watu wote hata wewe msomaji mnaitwa kupita njia hii.

Hata katika kitabu cha Mkusanyiko wa madhehebu ya kiprotestandi kiitwacho METHODIST. Kinasomeka:- “Madhehebu sio ya Mungu, hayajawahi kuwa na hayawezi kuwa kamwe , ni roho mbaya anaewatenganisha watu wa mungu katika madaraja ya makasisi na washiriki.
Kwa hiyo basi ni roho mbaya anayewabagua watu wa watu .
Hivyo ndivyo shirika na Madhehebu yafanyavyo. Katika kujiundia madhehebu . wao hujitenga na neno la mungu na kujiingiza katika uzinzi wa kiroho na kulikataa neno la kiroho (Methodist Uk 197 aya 2.


Askofu Peter Kitura wa AIC katika kitabu cha Jumapili au Jumamosi ameandika. “Neno sabato /shabath kwa kiebrania au sabatoo kwa kiyunani lina maana ya mapumziko au siku ya mapumziko asili ya mapumziko yaani sabato haya ni katika kitabu cha mwanzo (Mwanzo 2: 1-3. kama tulivyosoma hapo kwanza ) anaendelea kwa nuru ya mistari hii Mungu mwenyewe alipumzika alihitaji siku moja ya kustarehe baada ya kazi yake ya uumbaji iliyomchukua siku sita. Kutokana umuhimu wa kupumzika kwake akaitakasa siku hiyo ya saba . Neno takasa lina maana ya kuweka wakifu au kutenga kwa ajili ya matumizi matakatifu, yaani matumizi maalum yanayokusudiwa na Mungu au kuondoa unajisi (sura 1 aya 1)
Yeye mwenyewe nalielewa ingawa najaribu kutafuta sababu za kukwepa.
Si wakiristo tu walijua hii lakini hata katika vitabu wa ndugu zetu waislamu limeandikwa.
Njia ya kwanza ya sabato ya J.mosi koroani sura 4 aya 4 (4:47) “Enyi mliopewa kitabu Aminini tuliyowatelemshia yanayosadikisha yaliyondani kabla hatujazigeuza nyuso zenu tukazipeleka kisogoni au kabla ya kuwalaani kama tulivyowalaani watu walioharibu utukufu wa J.mosi na amri ya mwenyezi Mungu ni lazima kufanywa. Ingawa ndugu zetu Waislamu hili hawajalitii (koroani sura 4:154 ufafanuzi ‘c’ ) Na baada  ya kutoka katika hiyo miji na vijiji ya shamu waliambiwa waazimishe hiyo siku ya jumamosi kuwa waifanye kuwa siku ya Ibada na siku ya kufanya kazi”
Hata waislamu wameagizwa kutii Amri hii ya kutofanya kazi siku ya sabato (Jumamosi) “Na kwa yakini mmekwisha kujua habari za wale walioasi miongoni mwenu katika Amri ya kuheshimu Jumamosi. Basi tukawaambia kuweni manyani madhabilifu (koroani 2:65)
Hivyo kwa mujibu wa koroani wale wote wasioiheshimu Amri ya kuitunza Jumamosi ni manyani wasio na akili. Siamini nawe mpendwa kama unaridhika kuwa hivyo. Njoo ujiunge na wasafiri waendao mbunguni.

NJIA YA PILI : JUMA PILI
Njia hii ilitumika mwaka 150 B.K. Dondoo  kutoka katika kitabu cha Muongozo wa wakatoriki.
Misala ya Waumini yana msingi wake katika maandiko ya Mtakatifu Yustino Mzaliwa wa Nchi ya Siria, ambaye alikuwa Mwalimu wa Filosofia katika muji wa Roma. Ndiye yeye aliyeeleza mkutano wa siku ya bwana ndio Dominica au Jumapili mnamomwaka 150 B.K

Mimi  ndimi njia na kweli na uzima”
Maelezo haya yanaonyesha dhahili hakuna ukubali wa Biblia juu ya Ibada ya jumapili isipokuwa ni mapokeo kutoa kwa watu huku akijiita ndiye njia.
Tazama ushahidi mwingine katika kitabu cha AIC Jumapili au J,mosi Uk.45.
“Siku ya sabato au Jumamosi yesu alikuwa kaburini. Siku ya kwanza ya juma Yaani Jumapili alifufuka kutoka kwa wafu. Kwa kuwa sabato ilikuwa Jumamosi kwa kalenda ya kiyahudi siku ya pili yake iliyotengwa na Mungu kuwa siku ya Pentekoste ilikuwa siku ya  Jumapili. Wayahudi walijijua hivyo na kanisa linajua hivyo. Huko Troa Wakristo walianza kuabudu siku ya kwanza ya juma (Juma pili) pamoja na kumsikiliza Paulo akihubiri neno la Mungu walikuwa na Ibada ya ushirika kwa kusema, hata tulipokuwa tumekutana hata kuumega mkate mwandishi wa kitabu cha matendo ya mitume Luka alionyesha ilikuwa siku ya ibada haikuwa siku ya kuagana tu kama Wakristo wenzetu Wasabato wanavyodai” Nukuu hii ni katika kutafuta namna ya kutafuta kupindisha maandko matakatifu. Hebu tuangalie katika Biblia Luka ameandika nini? “jumamosi jiono tulikutana ili kuumega mkate, kwa vile Paulo alikuwa amekusudia kkusafiri kesho yake; aliendelea kuwahutubia watu hata usiku na kuendelea kuongea nao hadi usiu wa manane” Mat 20:7. (Kiswahili cha kisasa) hii inaonyesha kuwa  ilikuwa ni ibada ya kuhitimisha siku ya Sabato. Wala haikuwa jumapili bali siku ya jumamosi.
Jumapili ni siku ya kwanza ya juma, siku ya kufanya kazi wala sio siku ya Ibada. “Naye alipofufuka siku ya kwanza yajuma alimtokea kwanza Mariamu Magdarena ambaye hapo kwanza alimtoa pepo saba, huyo akashika njia akawapasha habari wale aliokuwa pamoja naenao wakali wanaomboleza na kulia. Lakani hao waposikia kwamba yu hai hawakusadiki. Baada ya hayo aliwatoke watu wawili miongoni mwao akiwa na sura nyingine; nao walikuwa wakishika njia kwenda shambani” Mark. 16:9-16. (Kiswahili cha kisasa.)  hivyo ni dhahili kuwa jumapili ni siku ya kufanya kazi ndio maana hata hawa wanafunzi wa yesu walikuwa wanakweda shambani.
Lakini Jumapili inaonekana kushamili sana siku za leo kama siku ya Ibada, chini ya kiongozi wa Madhehebu zote za j,pili. Kamusi ya Kiswahili  sanifu inasomeka hivi. “mtaguso: mkutano maalumu wa wakuu wa kanisa la katoriki ambao unawea kubadiri sheria kwa ruhusa maalum ya papa.” Uk. 327.
Papa anayetajwa hapa ndiye kiongozi wa kanisa Katoriki. Kitabu cha muongozo wa kanisa katori; Katekisimu ndogo uk. 26. “Siku hizi nanai ni mwandamizi wa viongozi hao? Jibu: Papa… Askofu wa Roma ndiye mwandamizi wa mtume Petro na maasikofu ndio waandamizi wa Mitume.”
Kiongozi wa wakatoriki wote ni Papa na ndiye amekuwa mstari wa mbele katika kupindua na kupotosha maandiko Matakaatifu.tazama jinsi anavyojichukulia cheo cha Mungu Mkuu. Katika kitabu cha Papa ni nani? Uk.26. kinasomeka “Kwa kuwa Askofu wa Roma kwa haki ya kimungu anao Ukuu wa kitume na kanisa zima tunafundisha hivyona kutangaza yey ndiye  hakimu mkuu wa waumini wote. Ambaye kwake rufaa ya mambo yote yaliyo katika uchaguzi wa kanisa yanaweza kufanywa. Hukumu ya papa haina rufaa, kwa kuwa mamlaka iliyo kuu zaidi”  Je, mpendwa neon hili ni dogo na jepesi kiasi cha kutolitafakali vuzuri? Kitendo cha mwanadamu mwenye kufikiwa na kifo kujitangaza kama hakimu mkuu. Nafasi  na cheo cha Mungu aliye BWANA pekee?
Hii ndio sababu hata ya kudiriki mkubadil sheria takatifu za Mungu. Amri ya NNE ya Mungu inatutaka kuitakasa na kuitunza sabato ya jumamosi wao wakatangaza ibada ya jumapili kinyume na Mungu.
Kitabu cha Wakatoriki. Misale ya waumini uk.1) “… kwa hiyo tangu siku ile aliyofufuka bwana kanisa linatuita siku ya kwanza ya juma ndiyo dominika” maana yake siku ya bwana j,pili.
Wameliacha Kanisa la BWANA na Amri zake nakugeukiaka miungu mingine ya jua na sanamu. “Ndipo akanileta mpaka mlangoowa kuingilia katika nyumba ya BWANA, uliolekea upande wa Kaskazini, na tazama wanawake wameketi wakimlilia Tamuzi. Akaniambia mwanadamu umeyaona haya? Utaona tena machukizo makubwa kuliko hayo. Akaniletaa mpaka hua wa ndani wa nyumba ya BWANA, na tazama mlango pa Hekalu la BWANA, kati ya ukumbi na Madhabahu, walikuwapo watu kama ishirini na watanowamelipa kisogo Hekalu la BWANA, na nyuso zao wameelekeza upande wa mashsriki, nao wanaliabudu jua, kwa kuelekea upande wa mashariki. BAsi akaniambia umeyaona haya Ee, mwanadamu? … wafanye machukizo wanayofanya hapo? Kwa maana wameijaza nchi hii kwa udhalimu, tena wamerejea nyuma ili kunikasirisha; na tazama wanaliweka tawi puani. Kwa sababu hiyo Mimi nami nitatenda kwa ghadhabu; jicho langu halitachilia wala sitaona huruma, na wajapolia, na wajapolia masikioni mwangu kwa sauti kuu, sitawasikia.” Eze. 8:14-18.
Maneno haya ya Biblia yako wazi yakionyesha jinsi gain watu wameacha maagizo ya Mungu na kugeukia ibada za miungu. Tazamaa kitabu hiki cha Wakatoriki (Katekisimu kubwa uk.484.) kinavyosomeka. “Sisi sote tunakkusanyika siku ya jua, ndio siku ya kwanza baada ya Sabato ya Kiyahudi lakini pia siku ya kwanza ya juma.”
Nji hii inayoongozwa na Papa ambaye hana hatima ya wafuasi wake ila katika hukumu ya milele, maana ndio mwisho wa njia yake. Kitabu cha Wakatoriki (Mungu na Wanadamu toleo la pili. Uk.195. “Kanisa katoriki litadumu  mpaka lini? Jibu: litadumu mpaka mwisho wa Dunia.” Mwanzilishi wa njia hii ni mroma na ndiye anaye elezea mwisho wa njia yake kuwa ni pale Yesu atakaporudi mara pili, wala haitaingia mbinguni wala haitakuwepo tena.  Unajua kwa nini? Kwa sababu hata mafundisho yake ni ya mapokeo ya wanadamu yaliyochanganywa na Neno la Mungu kidogo ili kuwapumbaza watu Kitabu cha mwongozo wa wakatoriki, (katekisimu ndogo. Uk. 12) “Kanisa Katoriki uchota mafundisho ya Mungu wapi? Jibu: Kanisa katori uchota mafundish ya Mungu :-
1: Maandiko matakatifu.
2: Na katika mapokeo.

Uf. 22:18 inasomeka “Namshhudia kila anayesikia maneno ya unabii wa kitabu hiki, mtu yeyote akiyaongeza Mungu atamwongezea, hayo mapigo yaliyoandikwa kitabu hiki. Na mtu yeyote akiondoa lolote katika neon la unabii wa kitabu hiki Mungu atamwondolea sehemu yake katika mti wa uzima, na katika ule Mji mtakatifu ambao habari zake azimeandikwa katika kitabu hiki.
Wameacha Neneo la Mungu wameandama Mapokeo yaliyo maneno ya wanadamu. Nao wamelitimiza neneo la BWANA alilonena kwa kinywa cha Nabii Isaya. “Wawaambiao waonaji msione; na manabii msitoe unabii wa mambo ya haki, tuambieni maneno laini, hubirini maneno yadanganyayo.” Isa. 30:10.
“Maana utakuja wakati watakapo yakataa mafundisho yenye uzima; Ila kwa kufuata nia zao wenyewe watajipatia walmu makundi makundi, kwa kuwa wana masikio ya utafiti; nao wataiepusha wasisikie yaliyo kweli; na kuzigeukia hadithia zaz uongo.” 2Tim. 3:3-4.
Hii ndio njia ya pili. Juma pili inayobebamafundisho ya mapokeo ya watu (viongozi wa dini) Nao wanawapeleka watu katika upotevu. “kwa maana wawaongozao ndio wawakoseshao, na hao waliongozwa na waatu hao wameangamia.” Isa.9:16.

NJIA YA TATU IJUMAA-WAISLAMU.
Njia hii ya alah nayo inaelekea mbinguni, na watuwanaoipitia wanamfuata mtume Mahamad.
Njia imejikita katika Mafundisho ya watu. Maana Muhamad mwenyewe hakuwa anajua kusoma wala kuandika. Basi alitoa wapi mafundisho yake. “Na wakasema ni ni visa vya watu wa zamani alivyo viandikisha Muhamad kwani yeye mwenyewe hajui kuandika wala kusoma hajui. Alivyosimuliwa asubuhi na jioni kasha yeyeanawasimulia watu akisema ,ameyatelemsha haya yule ajuaye siri za mbinguni na ardhini. Bila shaka yeye ni mwingi wa msamaa.’ Koroani sura 25 aya5-6. “ Ambao wanamfuata mtume. Nabii aliye Umi(maamuma) asiyejua kusoma wala kuandika , na juu ya hili atafundisha mafundisho mafundisho  hayo ya ajabu ya iuslamu.” (koroan. Sura 7 aya 157.)
 Njia hii ilianza kufuatwa mwaka wa 610 B.K. “Tarehe 17 mwezi 12 mwaka 610. Utume uliletwa.” (kitabu cha maisha ya nabii Muhamad Uk 1). Utume huu uliletwa kwa mtu huyu ili awaongoze wanaojua kusoma na kuandika wala hawazingatii kuchunguza kile wanachoagizwa kukifuata. Yako maneno ambayo yako wazi wala hayahitaji Elimu kubwa kuyaelewa, kama hapa. “Je, nimfanye mola wangu asiye kuwa mwenyezi Mungu, ambaye ni muumba wa mbungu na ardhi ambaye ulisha wala harishwi? Hakika mimi nimeamrishwa niwe wa kwanza katika wenye kusilimu. Na nikaambiwa nisiwe miongoni mwao wanaomshirikisha  Mwenyezi Mungu.”  Je, mtu huyu awezakuwa kweli nabii wa BWANA Mungu aliye muumba wa mbingu na nchi? Ikiwa hana uhusiano naye tena amezuiwa kumshirikisha yeye aliye Mola? Mmu! Inatia shaka.
“Kwa maana kuna wengi wasiotii wenye maneno yasiyo na maana., wadanganyaji, na hasa wale wa tohara ambao yapaswa wazibwe vinywa vyao. Wao wanapindua watu wa nyumba zima, wakifundisha yasiyo pasa kwa mapato ya aibu, mtu wa kwao nabi wao wenyewe… Wanakili kwamba wanamjua Mungu, lakini kwa matendo yao wana kana: ni wenye machukizo, waasi wala kwa kila tendo jema hawafai.” Tit. 1:10-12,16. Kwa namna hii hata mafundisho yao hayatokani na MUNGU.
“Na wengi kati yao hawamwamini Mwenyezi Mungu, isipokuwa na huku wanatia ushirikina. (ufafanuzi: Na haya hata hapa petu tunayo japo tunafuata uislam lakini lakini tunatia ushirikina pia, tunakwenda makaburini tukayaambia Ee, bwana nimezongwa na …… ukinifungua ….. nitaleta hapa pesa au kombe la harua. Anasikia wapi huyu maiti?...”) koroani. Sura 12 aya 106.
“wala hawawi sawa walio hai na wafu. Kwa yakini mwenyezi Mungu umsikilizisha yeye amtakaye, na wewehuwezi kuwasikilizisha waliomom makaburini, na hao kama wamekufa wamo makaburini.” Koroan. Sura 35 aya 22.
Kumbuka mpendwa mtu yule asiyejua kuandika wala kusoma ndiye aliyeandikisha haya iili wale wanajua kusoma na kuandika wasome. Je, litakuwa kosa lake au kosa la waliandikiwa kutosoma na kutafakali hayo waaliyoandikiwa? Ili wajiepushe hata kujiponya nafsi dhidi ya udanganyifu mkubwa huu wa kumtumainia mungu asiyekuwa muumba wa mbingu na nchi. Maana mungu huyo wanayeelekezwa kumuabudu ni mungu wa mji wa dunia hii ya dhambi tu. “Bila sha nimeamlishwa nimwabudu mola wamji huu wa Maka.” Koroan. Sura27aya91.
Lakini Mungu wa kweli yeye yko Mbinguni. “Lakini MUNGU wetu yuko Mbinguni, alitakalo lote amelitenda.” Zab.115:3.
Ujajua Muhamad hata ukitafuta katika Koroan hakuna maali alipoitwa na Mungu kuwa nabii il yeye ndiye anajita kwa nabii. Lakini Manabii wa Mungu waliitwa na Mungu.
“…Ambao wanamfuata nabii aliye umi (maamuma) asiyejua kusoma wala kuandika na juu ya haya atafundisha mafundisho hayo ya ajabu ya uislamu.” Koroan. Sura 7aya157. Mafundisho yasiyokuwa na wokovu maana hayafundi kumtii Mungu wa Mbinguni, leea aya tuliyoisoma katika koroan hapo nyuma.
Ukisoma katika Koran sura ya 3aya ya 19. wanasema kuwa dini ya haki ni Uislam (wa ijumaa). Lakini ni nani aliyeanzisha dini hii. “Hawaabudu baada ya kumuacha Mwenyezi Mungu, ila waungu wanawakw.Wala hawamuabudu (Mungu) ila Shetani asianayewaanzishia hayo., ambaye Mwenyezi Mungu amemlaani. Naye shetani alisema kumwabudu Mwenyezi Mungu kwa hakika niashika sehemu maalum katika waja wako na nitawapoteza nanitawatumainisha na nitawwaaminisha ninavyotaka mimi. Basi watakata masikio ya wanyama wawafanye kuwa wanyama watukufu. (kama wanavyofanya ngamia waislamu) nitawaamuru pia, nao wataibadii dini yako Mwenyezi Mungu.” Koroan. Sura 4aya117-121. sasa unaweza kujua kuwa watu hawa wamebadilishwa na Shetani hata kuacha kumuabudu Mungu wa Mbinguni Katika dini yake na kutunza utakatifu wa sabato (jumamosi) na kugeukia ijumaa. Na hapa wamejipatia mafundisho ya uongo ili kuwapoteza. “Na miongoni mwao kuna baadhi yao wanaopinda ndimi zao kwa kusoma vitabu ili mppate kuyafikiri maneno yao hayo kuwa ni ya kitabu cha Mwenyezi Mungu, … kumbe si sio kitabu cha Mwenyezi Mungu, wanasema haya yametoka kwa Mwenyezi Mungu kumbe hayatoki kwa Mwenyezi Mungu. Wanamsingizia … uongo na hali wanajua kwamba huo ni uongo.” Koroan. Sra3aya78. Je, ni uongo gain wanaoufanya.  “Yeye Alah ndiye aliyetelemsha kitabu. Ndani yake zimo aya mukamu(nyepesi kufaamika) na zipo nyinine stashabiha yaani za kubabaishia, kama habari za ahela na za peponi na za motoni na mengineyo yanayohusika na roho. Wale ambao moyoni mwao mna upotovu wanafuata wanafuata zile ambazo zinababaishia. Kwa kutaka kuwaharibu watu…” koroan. Sura 3aya 7.
Je, unajua huko peponi na ahela ni wapi? Au ni mbinguni Ebu tuone koroani inatuambiaje!
Tuanze kungalia Peponi: Mfano wa pepo walioahidiwa Wacha mungu ni itakuwa hivi. Imo mito ya maji yasiyovunda na mito ya maziwa yasiyoharibika radha yake na mito ya ulevi yenye radha kwa wanywao na mitoya Asali iliyosafishwa, tena humo watapata matunda ya kila namna na zamaradi kuttoka kwa mola wao. Basi wale watakuwa sawa na walio motni na kunyweshwa maji yachemkayo. Koroan. Sura 47aya15.
 Ooh! Nmna hiihakuna hja ya kusumbuka kuifuata njia hii maana ni kujitesa bule na mwisho ni adhabu sawa na watenda dhambi wengine.
Habari gain kuhusu Ahela. (‘fafanuzi: jehanamu ni jina la moto maalumu huko ahela)” koroani sura 78aya 21. basi kama  ahela kuna moto wa jehanamu  hukumu ya hao watakkao kuwa huko itakuwa kuangamia kwa moto wa huo. Kwa hakika hakuna tumaini la wokovu kwa wanao ifuata njia hii maana ni njia ya uangamivu. Maana ikiwa uko usawa kati ya wadhambi na wema siku ya hukumu, njia gain hiii kuifuata isiyo na tumaini la Uzima.
Unafahamu hili kuwa hata Mtume muhamad hakujua hatima ya njia aliyoinzisha. “Mimi sio kiloja mpya katika mitume, wala sijui nitakavyofanywa mimi  wala sijui mtakavyo fanywa ninyi.” Koroani. Sura 4 6aya 9.
Kwa kuwa hajui hatima yake kama Mitume wa Yesu walivyojua. Ni nini hatima yautume wake? Maana Mitume wa Yesu wao walijua hatima yao “ Kwa maana Mimi sasa namiminwa, na wakati wa kufariki kwangu umefika. Nimevipiga vita vilivyo vizuri, mwendo nimeumalliza, Imani nimeilinda; baada ya hayo nimewekewa taji ya haki ambayo BWANA mhukumu wa haki, atanipa siku ile; wala si mimi tu na watu wote waliopenda kufunuliwa kwake. 2Tim.4:6-8.
Lakini tazama tumaini la Mhamad aliye mtume wa uislam: “Lakini wanangojea jingine la kuwajia mfano wa siku za adhabu zilizowafika watu aliopita kabla yenu. Basi mimi nami niko pamoja nanyi katika wanaongojea.” Koroani sura10aya 102. Kwa nini wanangojea adhabu? … Hakika adhabu ya kuivunja taadhima ya Jumamosi iliwekwa juu ya wale waliohitarafiana kwa ajili ya hiyo Jumamosi na kwa hiyo Mola wako atahukumu baina yao siku ya kiyama.” Koroan. Sura 16 aya 124.  Kwa sababu ya kuikataa sheria aliyopewa Musa Nabii wa Mungu, ingawa waliijua.
“Amekupeni shria ya dini ile ile aliyomhusia Nuhu na tuliyokufunulia wewe na tliyomhusia Irahimu na Musa na Isa, kwa simamisheni dini wala msifarakane kwayo.” Koroani sura 42aya13. Lakini rafiki unajua kuwa hata Alah mungu wa Waislamu atachomwa katika moto wa jehanamu? Tazama kitabu cha waislam cha Hadthi za mtume: uk.1071. “ … Jehanamu itaendelea kusema, je, kuna nyongeza? Mpaka alah subuana wataalaatakapoweka mguu wake na hapo atasema  inatosha? Inatosha na hapa kwa nguvu yako na zile sehemu zake nyingine zitakaribiana.” Ikiwa yeye aliye mungu wao ataangamia katika moto wa milele?! Si zaidi hao wafuasi wake? Njoo kwa Yesu yeye amekwenda kuwaandalia makao wote wamchao na kutoka huko atakuja kuwachukua akaishi nao milele zote.
Lakini habari gain kuhusu Jumapili? Katika kitabu cha muunganiko wa Madhehebu ya kipentekoste, kiitwacho: METHODIST. Uk.191 na 192. kinasomeka hivi:- “Unajua nini tunaelekea katika upande huo leo. Kanisa Katoriki la Rumi ujiita kanisa mama; linajiita kanisa la kwanza ama kanisa la awalli. Hivyo ni kweli tupu. Lilikuwa ndilo kanisaasi la kwanza la Rumi llililoanguka na kuuingia dhambini, lilikuwa la kwanza  ambalo liliunda madhehebu  ndani yake kulionekana matendo ya Wanilolai na aadae mafundisho ya wanikolai.
Hakuna mtu anaweza kukana kuwa ndilo mama. Hilo ni mama na llimeza mabinti, basi binti utokana na mwanamke. Mwanamke aliyevaa mavazi ya nyekundu na anketi juu ya vilima saba. Yeye ni kahaba na amezaa mabinti (Ufu. 17:3-5akanichukua katika roho hata jangwani nikaona mwanamke, ameketi juu ya mnyama mwekundu sana, mwenye kujaa majina ya makufuru menye vichwa saba na pembe kumi. Na mwanamke yule likuwa amevikwa nguo za rangi ya Zambarau, na nyekundu… alikuwa na kikombe cha dhahabu mkononi mwake klichojawa na machukizo . na katika kipaji cha uso wake aliuwa na jina lililoandikwa kwa siri, BABELI MKUU, MAMA WA MACHUKIZO NA MACHUKIZOYA NCHI.)  Mabinti hao ni makanisa ya kiprotestanti yalitoka kwake  a kasha yakarudi moja kwa moja kwenye Madhehebu ya wanikolai. Mama huyu wa makanisa binti anaitwa kahaba, huyo ni mwanamke ambaye hakuwa mwaminifu kwanadhiri yake ya ndoa, aliolewa na Mungu alafu akaenda kufanya uasherati na Ibirisi. Na katika uasherati wake amezaa mabinti walio kama yeye kabisa. Muungano huu wa mama na binti  ni upinga Neno, upinga Roho, kwa sababu hii ni upinga kristo.
            … Kabla sijaendelea mbali nataka kusema kwamba. Hawa Maaskofu wa mwanzo walidhani kuwa wao walikuwa  juu ya neon wao waliwambia watu kuwa wao waliweza kuwasamehe dhambi zao. Hiyo haikuwa kweli Walianza kubatiza watoto wachanga katika karne ya pili. Si ajiabu watu leo hii wamechanganyikiwa, ikiwa walikuwa wamechanganyikiwa  namna hiyo wakati huo karibu sana na wapentekoste wamo katika hali mbaya sana sasa kuliko nyakati zilizopita  wakiwa umbali yapata kama miaka 2000, kutoka kwake wakiwa wameacha ile kweli ya asisli.
 Hivyo ndivyo hasa kanisa katoriki lilivyo fanya wao waliwaua wale ambao wangektaa kutii utawala wa kipapa. Wale waliotaka maneno ya Mungu badala ya maneno ya watu, waliwaua mara nyingi kwa njia za kikatili. Lakini Kanisa hili ambalo lilishughulika na Mauaji lilikuwa lenyewe llimekufa na halikuwamo na uhai ndani yake wala ishara lililopata kufuatana nayo.
Sura hii inaonyesha nguvu ya kanisa Katoriki la Rumina yale litakayoyafanya kwa kupitia kwenye Shirika.  Kumbuka huu ndio ule mzabibu wa uogo  acha ulitaje tu jina la BWANA. Wanafanya hivyo kwa uongo, uongozi wao ni wake sio wa BWANA bali ni wa Shetani.” Methodist. Uk.191-2.
Kurasa hizi zinaeleza ukweli wa kile ambacho kwa wale wenye nia ya kutafutaa wokovu wataona sababu ya kuiangalia njia ya kweli. Unajua nini, kwamba ni kweli kuwa madhehebu zote za Kiprotestanti tayali zimekwisha jiunga na umoja wa Makanisa, ambayo muu wao ni Papa yule waiyetoka kwake na sasa wamerudi na kuwa nchini yake. Pengine ndio maana Mwandishi anasema wamekwisha rudi kwa mama yao. Ingawa wameziba masikio wasisikie wala kuwaambia watu wanaowaongoza juu ya hatari iliyo juu yao. “Watu wangu wamekuwa Kondoo waliopotea, wachungaji wao wamewapoteza; wamewapotosha milimani wamekwenda toka mlima hadi kilima, wamesahau mahali pao pa kupumzika (Raha). Yer.50:6. Raha yao iko wapi? “Basi, imesalia Raha ya Sabato kwa Watu wa Mungu.” Ebr.4:9.
Je, njia ipi itaingia Mbinguni?
“Kama vile mbingu mpya na nchi mpya, nitakazo zifanya, zitakavyokaa mbele zangu asema BWANA wa, ndivyo uzao wenu na jina lenu litakavyokaa. Na itakuwa mwezi mpya hata mwezi mpya, na Sabato hata Sabato,wanadamu wote watakuja kuabudu mbele zangu, asema BWANA.” Isa. 66:22-23.
Mpendwa Sabato ya siku ya saba (jumamosi) ndiyo njia ya kweli na sahii  ya kukufikisha Mbinguni, ungu mwenyewe ndiye mwanzilishi wake, Yeye ni msabato, Malaika zake ni wasabato, Manabii Musa, Eliya, Nuhu, mitume wa Yesu ni wasabato kama Yesu alivyokuwa.  Mbinguni wote ni wasabato. Njoo ujiunge na kundi la watunza sabato uwe nawe kundla Mungu.