Waweza Kuishi na Yesu, lakini huwezi kuishi bila Yesu.Yohan 3:16

REFORMATION OF FOOD AND DRINKS.
DEADLY OUTCOMES BROUGHT BY INDULGENCE OF TEA AND COFFEE.
By Petro Tumaini.










Though the intanke of Tea,coffee and Tobacco IS underestimated, the spiritual and Medical iplications have a great impact on human body 

  In God's eyes is Sin because God doesnt want us to use anything which destroys His dweling temple ( Your body)
  • Did You know that God is concerned with your health than you take care of yourself?
  • Did you know that the use of Tea, Tobacco, Coffee and other stimulants is sin though there is no direct prohibition which mention them in the bible?
  • Did you ever knew that worshiping and honoring god is more that atending church, it also includes Drinking, Eating and doing everything? 
For you to know the only task you have is Just to scroll down this article to discover the whole truth  of those statements.
How Does Bible show us that god wants us to be careful in whatever we eat or Drink.

1 Corinthians 6:19-20,"Do you not know that your body is a temple of the Holy Spirit, who is in you, whom you have received from God?  You are not your own; 20 you were bought at a price.  Therefore honor God with your body,"

Because God is highly concerned with the well being of our bodies, He instructed us to honor him by applying proper principles of eating, drinking and doing everything.

Eating and drinking is also a worship because that determines the presence of holly spirit in God's temple which is our body. So when you eat or drink anything which destroys your health you destroy the Temple of God in turn you chase away the presence of holly spirit in your body. Thats why the bible condemns us that we should not take alcohol.

Apart from alcohol there is other stimulants which though you can not find them in the Bible, God prohibits the use of them because they destroy your health, these are Coffee, Tea , Tobacco, Coce and others.

Forinstance there is no verse in the Bible which say's "Thou shalt not smoke cigarete" but cigarate smoking is highly condemned Why? Because it is hamful to the Temple of God (Your body)

Let us take a specific look at Biblical implication of Coffee and Tea by considering how god broadened the meaning of  1 Corinthians 6:19-20, through his revelation to Ellen g White. If you wants to know the Coplete profile of Ellen G White, go to the following link- www.whiteestate.org


These are some of Ellen G White coments on the use of Coffee, Tea and Alcohol.

There is lot of Stimulants used by human beings which cling us to despair? Satan Has put poisons in some of Plants created by God with the fixed purpose of losing as many people as possible due to indulgence of appetite.
It has been the common practice among Christians to use stimulants like Tea, Coffee, Tobacco and other related stimulants, There is a great deal and negative effects accompanied by the use of these stimulants.
Let’s consider the counsel of God’s prophet Ellen G White which reveals spiritual and Medical implications of these materials which can be found in the table manner of many people.
It must be kept before the people that the right balance of the mental and moral powers depends in a great degree on the right condition of the physical system. All narcotics and unnatural stimulants that enfeeble and degrade the physical nature tend to lower the tone of the intellect and morals. Intemperance lies at the foundation of the moral depravity of the world. By the indulgence of perverted appetite, man loses his power to resist temptation.  {MH 335.1}
It is not attractive to discover the truth unfold concerning stimulants, but so long as we keep on use of these products we can find ourselves geared toward the wilderness of sin, Satan is aware that spiritual power can be affected by the use of Tea, Coffee, and other stimulants.
These can be grouped into legalized drugs , but be watchful with what is termed Legal or Illegal drugs. All have the same effects on human body the only difference is the speed of bringing outcomes. Legal drugs like Coffee, Tea and Tobacco kills very slow and their effects can be witnessed even after ten years, twenty and above.
GOD NEEDS HIS PEOPLE TO HAVE TEMPERENCE.
Temperance reformers have a work to do in educating the people in these lines. Teach them that health, character, and even life, are endangered by the use of stimulants, which excite the exhausted energies to unnatural, spasmodic action.  {MH 335.2} 

GOD ADVISE US TO AVOID EVEN TOUCHING  STIMULANTS.
In relation to tea, coffee, tobacco, and alcoholic drinks, the only safe course is to touch not, taste not, handle not. The tendency of tea, coffee, and similar drinks is in the same direction as that of alcoholic liquor and tobacco, and in some cases the habit is as difficult to break as it is for the drunkard to give up intoxicants. Those who attempt to leave off these stimulants will for a time feel a loss and will suffer without them. But by persistence they will overcome the craving and cease to feel the lack. {MH 335.3} 

MESSAGE TO ALCOHOLIC DRINKERS AND MANUFACTURERS
"Woe unto him that buildeth his house by unrighteousness, and his chambers by wrong; . . . that saith, I will build me a wide house and large chambers, and cutteth him out windows; and it is ceiled with cedar, and painted with vermilion. Shalt thou reign, because thou closest thyself in cedar? . . . Thine eyes and thine heart are not but for thy covetousness, and for to shed innocent blood, and for oppression, and for violence, to do it." Jeremiah 22:13-17. 

 This scripture pictures the work of those who manufacture and who sell intoxicating liquor. Their business means robbery. For the money they receive, no equivalent is returned. Every dollar they add to their gains has brought a curse to the spender.  {MH 337.2} 

Coffee , Tea  and  Alcohol  destroys your health. God wants you to stay healhy because your body is the temple of god, satan wants to destroy your health because he doesnt want God's Holly Spirit to abide in you. May God bless you as you take measures to reform in food and drinks. 

References
Ellen G White, Ministry of Healing.

 




KIKAO CHA SHETANI NA AGENDA ZAKE.

MUNGU AMEAMUA KUFICHUA SIRI ZA KIKAO CHA IBILISI ILI UOKOLEWE

MKUTANO WA SIRI WA SHETANI NA WAJUMBE WAKE
ADHAMIRIA KUKOMESHA WATAKATIFU ( WAKRISTO )  DUNIANI

  • MIKAKATI 12 YA KUUA UKRISTO YAJADILIWA.
  • WAKRISTO WASIOSHIKA AMRI KUMI WANASWA
JE UMEISHANASWA?
MWENDEE YESU KWA NJIA  YA TOBA NAYE ATAKUSAMEHE.
  
         Shetani aliitisha mkutano wake wa siri ambao wajumbe wake walihudhuria ili kufanya namna  ya kukomesha  kazi ya watakatifu duniani.Mkutano huu ulikua ni wasiri sana, nahakuna Malaika wa Mungu aliye ruhusiwa kusikia kinacho zungumziwa. Lakini Mungu alijua na akamutuma YESU  iliamtume malaika ambaye alimpa taarifa  mmoja wa wajumbe wa Mungu, nabii,Ellen  G.  White mwaka 1884.

 MIKAKATI 12 YA SHETANI DHIDI YA WATAKATIFU(WAKRISTO)
1.Kadri watu wa Mungu wanavyokaribia dhoruba kuu ya siku za mwisho, Shetani anaitisha mashauri nyeti na malaika wake ilikuweka mipango ya mafanikio zaidi ilikupindua imani zao. Anaona kwamba makanisa  mashuhuri yanayopendwa na watu  tayari yameshalala kutokana na nguvu ya udanganyifu wake. Kwa mbinu ya vivutio na kuyatia kwenye miujiza anaweza kuyafanya yaendelee chini ya utawala wake, kwahiyo anawaelekeza malaika wake waweke mitego yao hasa kwa wale wanao tazamia kurudi kwa  Yesu mara ya pili, kuwaharibu ili wasiweze kuzitunza amri zote za Mungu.


2.Alisema mdanganyifu  mkuu huyo,“Lazima tuwachunge sana walewanao waita nakuwavuta watu kwa sabatoya yehova. Watawaongoza wengi waweze kuona umuhimu wa sheria ya Mungu; nakwa nuru hiyo, inayofunua sabato ya kweli, inafunua pia huduma ya kristo yapatakatifu Mbingini, na kuonyesha kuwa kazi ya mwisho ya wokovu wa mwanadamu inasonga mbele. Shikilieni mawazo ya watu gizani hadi kazi imalizike, natutawaletea mambo ya dunia na kanisa tuyachanganye pamoja pia."


3.Sabato ndio swala kuu  litaloamua  mwelekeo wa  roho za watu . lazima tuitie nguvu ibada ya kuabudu jumapili tulioianzisha  tuliyoianzisha. Tumefanya ipokelewe na watu wa dunia na washiriki wa kanisa ; sasa kanisa lazima . lielekeze kuungana na   dunia kwa kupewa misaada . Ni lazima tufanye kazi kwa kutumia ishara na miujiza ili tuyafumbe   macho yao  juu ya   ukweli ,na tuwavute ili waachane na maswali juu ya ukweli na wasimwogope Mungu ili wafuate mila na desturi

4.Nitawatumia wachungaji mashuhuri wenye mvuto   ili  waupindue mvuto wa wasikilizaji wao   ili  kuwatoa kwenye  amri za Mungu .mahali ambapo maandiko matakakatifu yanaikiri sheria kamili ya uhuru itaonyeshwa kama ni nira ya utumwa. Watu wanayapokea maelezo ya maandiko matakatifu yanayotafsiriwa na wachungaji wao , na huwa hawasomi ili kuchunguza wenyewe. Kwa hiyo kwa kutumia wachungaji nita watawala watu kama nipendavyo .

5"Lakini hasa , kusudi letu kuu ni kulinyamazisha dhehebu hili la watunza sabato. Lazima tuanzishe chuki kuu kinyume chao tutawatafuta watu mashuhuri na wenye hekima  ili  wawe upande wetu ;  halafu na kuwapitisha ili wawe na madaraka ili waweze kutekeleza makusudi yetu ndipo ibada ya jumapili niliyoianzisha italazimiswa kwa sheria zilizokali na zilizokazwa .Wale watakao zivunja watafukuzwa watoke katika miji, navijiji na kuwafanya wateseke kwa njaa na umaskini . Mara tutakaposhika madaraka tutawaonyesha jinsi ya kuwatenda wale ambao watakuwa bado hawajakana utiifu wa kanuni za Mungu. Tumelitumia kanisa la Rumi kuwa kamata na kuwafunga, kuwatesa na kuwauwa wale waliyokataa kujisalimisha chini ya sheria zake, na sasa  tunayaleta makanisa ya kiprotestant  yafanane na dunia, maana huu ndiyo mkono wetu ; Wakulia wenye nguvu mwishoni tutaweka sheria ya kuwaangamiza wale wote watakaokataa kujisalimisha chini ya mamlakan yetu. Wakati adhabu ya kifo itakapoitishwa  kwa watakaoivunja sheria ya kuabudu jumapili tulioianzisha , ndipo wengi walio katika  nyadhifa  za washikao amri watakimbilia upande wetu .

6."Lakini kabla hatujachukua hatua kali hizo, lazima tutumie hekima  ya juu kuwadanganya na kuwanasa wale wanaoitunza sabato ya kweli. Tunaweza kuwatenga wengi kutoka kwa kristo ikiwa tutawaletea mambo ya kidunia , tamaa na majivuno. Watajidhania    wenyewe wako salama kwasababu wanaamini ukweli  kwakuzama katika  tama ya uchu wa kula na misisimko vitawachanganya ili wasiweze kupambanua na kuharibu uchaguzi mzuri na ndipo wengi tutawasababisha waanguke

7."Nendeni wafanyeni wale waliona fedha na mashamba walewe na masumbuko ya maisha yao. Wapatieni dunia iwe kitu chenye nuru ya kuvutia    zaidi ili waweze  kuleta hazina zao hapa , na waweze kukaza makusudi yao juu ya vitu vyakidunia tu.lazima tuwa chunge kwa hali zote wale wanaomtumikia mungu ili  wasiwe na mali yoyote  itakayosaidia kuwapatia njia kinyume chetu .Ziwekeni fedha mikononi mwa watu wakubwa walio upande wetu.  Kadri wanavyopata  mali zaidi na ndivyo watakavyo uharibu ufalme wetu kwa  kutuchukulia watu na vitu vyetu . wafanyeni wapende fedha zaidi ya kuujenga ufalme wa kristo na kueneza ukweli ambao tunauchukia, nahatuhitaji kuogopa mvuto wao ; maana     kila mbinafsi mchoyo ataanguka chni ya nguvu zetu , na hatimaye atatengwa na watu wa Mungu.

8.Wale waliomfano wa utauwa , lakini hawajui nguvu zozote za Mungu, tunaweza kuwatumia wengi ili walete madhara makubwa kwa adui zetu. Wapenda anasa kuliko kumpenda mungu , hawa ni wasaidizi wetu mashuhuri kuliko wote hawa waliomo kwenye kundi hili tuta watumia kama vibaraka wetu ,  maana wana akili na hekima ili kuwavuta wenzao waangukie mitego yetu. Wengi hawataogopa mvuto wao kwasababu wanaiamini na kushiriki imani moja ndipo tutakapowavuta wengi waamini na kuamini kuwa sheria za kristo sio ngumu kulingana na  mafundisho waliyofundiswa hapo mwanzo na kwa kufanana na dunia watawajaza makanisa  mvuto mkuu wa mambo ya kidunia . Ndvyo watakavyo tengana na kristo na hapo hawatakuwa na nguvu za kupingana na nguvu zetu , na hatimaye watakuwa tayari kurudia  udhaifu walioukuwa nao zamani na kuto kuomba

9.Hapo ndipo tutakapotia pigo letu la mwisho; juhudi zetu za kupambana na washikao sheria zifanywe bila kuchoka. Lazima tuhudhulie mikutano yao inapokusanyika.Hasa katika mikutano mikubwa itasababisha hasara sana kwetu, na lazima tupeleke upinzani mkubwa, na tuweke mambo yatakayozuia  roho zao zisiusikie ukweli utakao wavutia.

10.Nitajipatia watu wawe ni watumishi wangu wa siri, wale walio tayari kupokea mafundisho ya uongo na ukweli wa kutosha, wauchanganye ili kuzidanganya roho za watu. Pia nitawatumia watu wasio amini miongoni mwao wawe pale, watakao elezea na kuleta mashaka juu ya ujumbe wa Bwana wenye onyo kwa kanisa lake. Kama watu watasoma na kuamini maonyo hayo basi tutakuwa na matumaini kidogo sana ya kuwashinda. Kama tutaupindua mvuto wao wasifuatilie maonyo haya watabaki kwenye giza la nguvu zetu za ujinga na kutoamini na hatimaye tutawapatia nafasi na vyeo vyetu mwishowe.

11.Mungu hataruhusu maneno yake kuchanganywa na takataka kama tutazivuta roho za watu gizani, baada ya muda Fulani, rehema ya Mungu itawaacha na hapo ndipo atatuachia uwezo kamili ili tuwatawale.

12. Lazima tusababishe ugomvi na mgawanyiko. Lazima taharibu ile kiu ya kupenda mambo ya kiroho, ili tuwafanye wawe wabishi, wagomvi, kushitakiana na kuhukumina ili wadumishe uchoyo na uadui. Na dhambi hizo Mungu alitufukuza mbele zake na wote watakao fuata mfano wetu yatawapata yaleyale yaliyo tupata.




Rejea :
Ellen. G . White, Testimonies to Ministers uk  472 – 475
Spirit of Prophecy, volume 4, 1884, uk 337-340
The great  Controversy, 1884 Sura ya 27 uk 337- 340.

Imeandaliwa na George  Masambu
george.joseph45@yahoo.com
+255759366966 au +255719048480 




UKWELI KUHUSU SABATO


Sabato ni kielelezo cha uumbaji wa Mungu


KWELI 100 KUHUSU SABATO YA BIBLIA

è Kwanini unapaswa kutunza sabato?
è Ni nani unayeabudiwa kaatika siku ya sabato?
è Nani aliiianzisha?
è Ilianzishwa lini na kwaajili ya nani?
è Ni siku gani ambayo ni sabato?
è Wengi hutunza siku ya kwanza ya juma au jumapili je wanamamlaka gani kimaandiko?
è Baadhi hutunza siku ya saba au jumamosi Je wana mamlaka gani ya kimaandiko kwa hilo?
è Je ibaada ya jumapili ilianza lini, ni nani aliyeianzisha, biblia husemaje kuhusu kuadhimisha siku ya jumapili kama siku ya Ibada?
è Hapa kuna ukweli kuhusu siku hizo zote, kama inavyoelezewa wazi na neno la Mungu.

ZIFUATAZO NI KWELI 100 ZA BIBLIA KUHUSU SABATO.
1)Baada ya kuumba dunia kwa siku sita, Mungu akapumzika siku ya saba. Mwanzo 2:1,3.
2)Jambo hili lilitia muhuri siku hiyo kama Siku ya Mungu ya mapumziko , au siku ya sabato , kama sabato imaanishavyo pumziko. Mtu azaliwapo siku fulani, siku hiyo huwa siku yake ya kuzaliwa (birthday). Kwahiyo Mungu alipopumzika katika siku ya saba, siku hiyo ikawa kumbukumbu ya kuzaliwa/ kuumbwa kwa dunia na vyote vilivyomo au siku ya sabato.
3)Kwahiyo siku ya saba lazima iwe siku yua sabato ya Mungu. Waweza kubadilisha birthday yako  kutoka siku ambayo ulizaliwa mpaka siku ambayo  hukuzaliwa? Hapana, pia huwezi kubadili siku ya Mungu ya pumziko ikawa siku ambayo mungu hakupumzika. Kwahiyo siku ya saba bado ni sabato ya Mungu.
4)Mungu aliibariki Siku ya Sabato (Mwanzo 2:3.)
5)Mungu aliitakasa Siku ya Sabato. (Kutoka 20:11.)
6)Aliifanya kuwa Siku ya Sabato katika Bustani ya Edeni. (Mwanzo 2:1-3)
7)Ilianzishwa kabla ya anguko, kwahiyo haikuwa kivuli kwa maana vivuli (vielelezo) vilianzishwa baada ya anguko. Kwasababu hiyo haijakomeshwa kwasababu ni kumbukumbu ya uumbaji wa mungu.
8)Mungu alisema ilifanyika kwaajili ya Mwanadam (Marko 2:27.) Hii humaanisha kwa wanadamu wote, kama vile neno mwanadamu hapa halina kikomo; kwahiyo ni kwaajili ya myahudi na mmataifa.
9)Ni kumbukumbu ya uumbaji . (Kutoka 20:11; 31:17.)Kila tupumzikapo siku ya sabato, kama Mungu alivyopumzika tunaadhimisha (sherekea) uumbaji.
10)Ilikabidhiwa kwa Adamu, Baba wa jamii ya wanadam. (Marko 2:27; Mwanzo 2:1-3.)
11)Kwahiyo kupitia kwake, kama Muwakilishi wetu, ni kwa mataifa yote. (Matendo 17:26.)
12)Si siku ya Waayahudi kwani ilianzishwa miaka 2,3000 kabla ya kuwepo Wayahudi.
13)Kamwe Biblia hahiiti sabato ya Wayahudi, lakini mara zote “sabato ya Bwana Mungu  wako.” Wanadamu wanapaswa kujihadhari na kuikanyaga sabato ya Mungu
14)Kielelezo cha sabato kama siku ya saba ya wiki , kinawekwa katika kiipindi cha wazee wa imani. (Mwanzo 2:1-3; 10:10,12: 29:27, 28 n.k)
15)Ilikuwa ni sehemu ya Sheria ya Mungu kabla ya Sinai. (Kutoka 16:4, 27-29.)
16)Kisha Mungu akaiwake kama kiini (Moyo) cha sheria yake ya maadili. (Kutoka 20:1-17.) Kwanini aliiweka pale kama haikuwa sawa na amri nyingine tisa ambazo hazibadiliki. Yesu alipoangikwa msalabani hakufuta amri kumi ,ndo maana uzinzi, wizi n.k bado ni dhambi, iweje uvunjaji wa sabato isiwe dhambi?
17)Siku ya saba ya Sabato iliamriwa kwa sauti ya Mungu aliye hai. (Kumbukumbu La Torati 4:12,13.)
18)Kisha Mungu akaandika amri hiyo kwa vidole vyake mwenyewe. (Kutoka 31:18.)
19)Akaitia muhuri katika jiwe lisilofutika, ikiashiria kwamba inaasili ya kutokuharibika. ( Kumbukumbu La Torati 5:22.)
20)Ilitunzwa katika sanduku lilioko Patakatifu Pa Patakatifu. ( Kumbukumbu La Torati 10:1-5.)
21)Mungu alikataza kufanya kazi siku ya sabato, hata katika nyakati ngumu zenye kazi nyingi.(Kutoka 34:21.)
22)Mungu aliwaadhibu wana wa Israeli jangwani kwasababu waliihalifu Sabato.(Ezakieli 20:12,13.)
23)Sabato ni ishara ya Mungu wa kweli, ambaye kupitia hiyo tunamtofautisha na miungu wa uongo. ( Ezekieli 20:20.), Wana wa israeli walipokuwa wakitoka Misri Sabato iliwatofautisha na waabudu miungu, hii inatokana na ukweli kwamba Amri ya nne Kutoka 20:8-...ndiyo amri pekee imtambulishayo Mungu kama muumbaji.
24)Mungu aliahidi kwamba Yerusalemu ingedumu milele endapo wayahudi wangeitunza sabato.(Yeremia 17:24,25.)
25)Mungu aliwaacha (Israeli) utumwani babeli kwasababu waliivunja Sabato. (Nehemia 13:18)
26)Aliiangamiza Yerusalemu kwa kuivunja Sabato.(Yeremia 17:27.)
27)Mungu ameahidi mibaraka maalumu kwa wamataifa na wote watakaoitunza Sabato.(Isaya 56:6,7.)
28)Hii ipo katika unabii , ambayo kwa ujumla inahusu ukristo. (Isaya 56.)
29)Mungu ameahidi kuwabariki wote waitunzao sabato. (isaya 56:2.)
30)Mungu anatuhitaji sisi tuiite siku takatifu ya heshima. (Isaya 58:13.) Iweni na tahadhari ninyi mnaoiita “Sabato ya zamani ya Wayahudi”, “nira ya utumwa.”
31)Baada ya Sabato takatifu kukanyagwa chini “vizazi vingi” itarejeshwa tena katika siku za mwisho. (Isaya 58:12,13.)Hapa Sabato inaelezewa kama mojawapo ya matengenezo ya ibada ya kweli katika siku za mwisho.
32)Manabii wote watakatifu waliitunza Sabato.
33)Mwana wa Adam (Yesu Kristo) alipokuja, aliitunza Sabato maisha yake yote. (Luka 4:16; Yohana 15:10.) Kwa  kufanya hivyo alifuata kielelezo cha Baba yake cha uumbaji. Je hatuwezi kuwa salama zaidi kwa kufuata kuelelezo cha Baba na  Mwana?
34)Siku ya Sabato ni siku ya Bwana ( Ufunuo 1:10,Marko 2:28, Isaya 58:13; Kutoka 20:10.)
35)Yesu Kristo ni bwana wa sabato (marko 2:28.), hii inamaanisha kuipenda na kuitunza, kama mume ni Bwana wa mke , kwa kumpenda Yesu ambaye ni Mume na kichwa ca kanisa(Waefeso 5:22-27) , tunamtii kwa kuitunza sabato ambayo ni agizo lake (si ombi) kwetu .
36)Yesu aliifunua Sabato kama taasisi ya neema iliyoundwa kwa kumtakia mema mwanadam. (Marko 2:23-28.)
37)Yesu Badala ya kuihalifu sabato , kwa umakini mkubwa alifundisha namna ya kuitunza.(Mathayo 12:1-8,Marko 3:1-5,Luka 14:1-5.),Mafarisayo walifanya sabato kuwa ngumu kwa kuzuia hata shughuli njema zisifanyike,Yesu akasema shughuli njema yaani za kuokoa uhai kama vile kutibu wagonjwa, kumpikia mwenye njaa ni halali kuzifanya Siku ya Sabato (Mmat 12:12.)
38)Yesu aliwafundisha wanafunzi wake wasifanye kitu Siku ya Sabato kilicho kinyume na sheria. (Mathayo 12:12.)
39)Yesu aliwasisitiza wanafunzi wake kwamba waombe baada ya kunyakuliwa kwake hata siku watakapokimbia maangamizi ya Yerusalemu, isiwe sabato maana wangeihalifu.(Mathayo 24:20.)Hili linadhiirisha kwamba hata Yesu alijua kwamba atakapo kufa, atakapo fufuka na kunyakuliwa sabato haitasitishwa.
40)Wanawake walioambatana na Yesu kwa umakini waliitunza sabato baada ya kifo cha Yesu.(Lika 23:56.)
41)  Miaka thelathini, baada ya Yesu kunyakuliwa , Roho Mtakatifu kupitia Paulo anaitaja kama “Siku ya Sabato,” (Matendo ya Mitume 13:14.)
42)Paulo, Mtume kwa watu wa mataifa, “aliita Siku ya Sabato” katika mwaka 45.A.D ( Matendo ya Mitume 13:14) Je Paulo hakujua? Au tuwaamini walimu wa sikuhizi wasemao iligongomelewa msalabani yaani iliishia kipindi Yesu aliponyakuliwa Mbinguni?
43)Luka, mwanahistoria wa Kikristo aliyevuviwa, akiandika miaka ya 62 A.D anaiita “Siku ya Ssabato.”(Matendo 15:21.)
44)Waongofu wa mataifa waliita Sabato. (Matendo ya Mitume 13:42.)
45)Katika baraza kubwa la Wakristo mwaka 49 A.D mbele ya mitume na maelfu ya wanafunzi , Yakobo anaiita “Siku ya Sabato.” ( Matendo ya Mitume 15:21)
46)Ilikuwa ni desturi kufanya maombi kufanya kusanyiko la maombi siku hiyo.( Matendo ya Mitume 16:13.)
47)Pauo  alisoma maandiko matakatifu katika kusanyiko takatifu katika Siku ya Sabato. ( Matendo ya Mitume 17:2,3.)
48)Ilikuwa ni desturi ya Paulo kuhubiri Siku ya Sabato.( Matendo ya Mitume 17:2,3.)
49)Kitabu cha Matendo ya Mitume kinatoa rekodi ya Paulo kufanya mikutano ya ibada 84, katika siku ya sabato.( Matendo ya Mitume 13:14,44; 16:13 ; 17:2 ; 18:4,11.)
50)Hapakuwa na ugomvi wowote kati ya Wayahudi na Wakristo juu ya Sabato.Huu ni uthibitisho kwamba wakristo waliitunza sabato ileile iliyotunzwa na Wayahudi.
51)Wakristo walipomshtaki Paulo, kamwe hawakumshtaki kwa suala la kutunza Sabato. Kwanini hawakumshtaki kama si kwasabau walikuwa wakiitunza?
52)  Lakini Paulo mweyewe alikiri kwamba aliitunza sheria. (Matendo 25:8.) Je hili lawezaje kuwa sahihi kama Paulo hakuitinza Sabato?
53)Sabato hutajwa katika aganojipya mara hamsini na nane,, na marazote kwa heshima ikibeba jina lile lile ililokuwanalo katrika Agano la Kale kama “Siku ya Sabato.”,na matendo ya kupumzika,ibada na matendo mema.Mathayo 10,Marko 11,Luka 18, Yohana 10 na Matendo  ya Mitume 9.
54)Katika agano jipya hakuna neno lionyeshalo kuwa Sabato ilisitishwa, kuondolewa, kubadilishwa , au kitu chochote cha aina hiyo.
55)Mungu kamwe hajaruhusu mwanadamu yoyote kufanya kazi katika siku hiyo, ndugu msomaji ni kwa mamlaka ya nani unaitumia siku ya sabato kwa kazi za kawaida?
56)Katika Biblia Hakuna Mkristo katika agano jipya, eidha kabla au baada ya kunyakuliwa kwa Yesu, ambaye alifanya kazi za kawaida Siku ya saba ya Sabato.Kwanini wakristo wa leo hufanya tofauti na Wakristo wa kwenye Biblia?
57)Hakuna rekodi kwamba Mungu ameondoa Mbaraka na Utakaso wa Siku ya Sabato.
58)Kama vile Sabato ilivyotunzwa Edeni kabla ya Dhambi (Anguko), vivyohivyo itatunzwa mbinguni baada ya dhambi kuangamizwa.(Isaya 66:22,23.)
59)Sabato ya Siku ya Saba ilikuwa na nafasi muhimu katika amri kumi za Mungu, kama ilivyotoka katika kinywa cha Mungu, na kuandikwa kwa kidole chake mwenyewe juu ya jiwe pale Sinai (tazama Kutoka 20.) Yesu alipoanza kazi alisema kwa uwazi kabisa Hakuja kuitangua Torati (sheria). “Msidhani ya kwamba nalikuja kuitangua torati, au manabii.” (Mathayo 5:17.)
60)Yesu aliwakemea vikali Mafarisayo  kwamba ni wanafiki wakiigiza kama walimpenda Mungu, na bado wakati huohuo wliihalifu sheria moja kati ya Amri kumi za Mungu kwa kufuata mapokeo yao. Uutunzaji wa jumapili kama siku ya Ibada ni mapokeo ya wanadam.


KWELI AROBAINI ZA BIBLIA KUHUSU SIKU YA KWANZA YA JUMA.

61)Kitu cha kwanza kurekodiwa katika Biblia ni kazi iliyofanyika siku ya kwanza ya juma.(Mwanzo 1:1-5.) Muumbaji mwenyewe alifanya hili.Kama Mungu aliiumba dunia siku ya jumapili,je yaweza kuwa dhambi kwa sisi kufanya kazi siku ya jumapili?
62)Mungu huwaamuru wanadamu wafanye kazi siku ya kwanza ya juma.( Kutoka 20:8-11.) Je ni dhambi kumtii Mungu?
63)Hakuna Mzee wa imani aliyeitunza Jumapili kama siku ya Ibada.
64)Hakuna Nabii Mtakatifu aliyeitanza (jumapili) kama siku ya ibada.
65)Kwa maelekezo ya sheria ya Mungu  ,kutoka  uumbaji hadi kifo cha Yesu watakatifu Wake wameitunza siku ya kwanza ya juma kama siku ya kawaida ya kazi angalau kwa miaka 4,000.
66)Mungu mwenyewe huiita siku ya kazi .(Ezekieli 46:1.)
67)Mungu hakupumzika katika ya kwanza (Jumapili).
68)Mungu hakuibariki siku ya kwanza (Jumapili.)
69)Yesu alikuwa fundi seremala (Marko 6:3) na alifanya biashara yake mpaka alipofikisha miaka 30. Aliitunza sabato na kufanya kazi kwa siku sita za wiki. Kwahiyo alifanya majukumu yake mazito siku ya Jumaapili.
70)Yesu hakupumzika siku hiyo ya jumapili.
71)Mitume walifanya kazi jumapili.
72)Mitume hawakupumzika jumapili.
73)Yesu kamwe hakuibariki.
74)Kamwe haijabarikiwa na Mamlaka Takatifu kutoka Mbinguni.
75)Kamwe haijatakaswa.
76)Hakuna sheria iliyoagiza kuitunza siku ya kwanza ya juma (jumapili) kama siku ya Ibada, kwa hiyo si dhambi kufanya kazi katika siku hiyo. “kwa maana pasipo na sheria, hakuna dhambi .” (Warumi 4:15. Pia 1 Yohana 3:4.)
77)Katika agano jipya hakuna sehemu ikatazayo kufanya kazi siku hiyo.
78)Hakuna adhabu itolewayo kwa kufanya kazi jumapili (ikionyesha kama imehalifiwa.)
79)Hakuna mbaraka ulioahidiwa kwa kuitunza.
80)Hakuna maelezo yaliyotolewa kwamba ni kwa namna gani inapaswa kutunzwa.Je hili lawezekana endapo mungu anekuwa anataka tuitunzw kama siku ya Ibada.
81)Kamwe haijaitwa Sabato ya wakristo.
82)Kamwe haijaitwa Siku ya Sabato.
83)Kamwe haijaitwa siku ya Bwana,wanadam ndio walioiita Siku ya Bwana.
84)Kamwe haijaitwa siku ya pumzinko.
85)Hakuna jina takatifu ililopewa. Sasa kwanini tuiite  siku takatifu?
86)Kwa urahisi huitwa “siku ya Kwanza ya juma.”
87)Yesu hakuitaja kwa namna yoyote,kamwe hakulitamka jina la siku hiyo kwa midomo yake, kwa rekodi yote tuliyonayo.
88)Neno jumapili kamwe halionekano kwenye Biblia, labda biblia ya kiswahili cha kisasa, lakini katika Biblia nyingine imetajwa kama siku ya kwanza ya juma.
89)Kamwe Mungu, Yesu , hata waliovuviwa kuandika  maandiko ya Biblia hakuna aliyewahi kuongea akiisifia jumapili kama siku ya Ibada.
90)Siku ya kwanza ya juma inatajwa mara nane tu katika Agano Jipya.(Mathayo 28:1, Marko 16:2,9; Luka 24:1. Yohana 20:1,19; Matendo ya Mitume 20:7; 1 Wakorintho 16:2.)
91)Mafungu sita huelezea siku ya kwanza ya wiki.
92)Paulo aliwaagiza watakatifu wajishughulishe na mambo yao katika siku hii ya kwanza ya wiki, (1 Wakorintho 16:2.)
93)Katika agano jipya tuna kumbukumbu ya mkutano mmoja tu wa kiroho uliofanyika katika siku hiyo, nao ulifanyika usiku (matendo 20:5-12.)
94)Hakuna maandiko yaonyeshayo kwamba walikuwa na mkutano kama huo kabla au baada ya hapo.
95)Haikuwa desturi yao kukusanyika katika siku hiyo(jumapili).
96)Hakukuwa na agizo la kuumega mkate katika siku hiyo.
97)Tuna kumbu kumbu ya tukio moja tu ambapo waliumega mkate. (Matendo ya Mitume 20:7.)
98)Tukio hilo lilifanyika usiku wa manane. (Matendo ya Mitume 20:7-11.) Yesu alifanya tukio kama hilo Ijumaa jioni (Luka 22), Na wanafunzi wakati mwingine walilifanya tendo hilo kila siku.(Matendo ya Mitume 2:42-46.) Ingekuwa ni Ibada rasmi ya kielezo kwa kawaida isingefanyika usiku bali kuanzia asubuhi.
99)Kamwe Biblia haijaonyesha sehemu yoyote kwamba jimapili (siku ya kwanza) ni siku ya kukumbuka kufufuka kwa Yesu, Haya ni mapokeo ya wanadam ambayo ni kinyume na neno la Mungu. (Mathayo 15:1-9.)
100)Ubatizo ndiyo tendo  litukumbushalokifo na ufufuo wa Yesu. (Warumi 6:3-5.), na jambo jingine ni kitendo cha kuumega mkate (Pasaka ) tofauti na ile ya mwezi wa nne kwasababu pasaka ya biblia na Easter ni vitu viwili tofauti. Yesu aliacha mabo hayo kama vielelezo vya kukumbuka na kuadhimisha ukombozi aliotufanyia na sio kusali siku ya kwanza ya juma.
101)Mwishowe, Agano jipya liko kimya kabisa kuhusu badiliko lolote la siku ya sabato au utakatifu wa siku ya kwanza.

Maelezo zaidi kuhusu Sabato.
                  ISHARA YA UHUSIANO WETU NA MUNGU.
                  Sabato ni Ishara ya taifa la Mungu, Kutoka 31:13,17,16.Imeandikwa , 13“Kisha, nena wewe na wana wa Israeli, na kuwaambia, Hakika mtazishika sabato zangu kwa kuwa ni ishara kati ya mimi na ninyi katika vizazi vyenu vyote; ili mpate kujua kuwa mimi ndimi BWANA niwatakasae ninyi. 17Ni kati ya mimi na wana wa Israeli milele; kwani kwa siku sita Bwana alifanya Mbingu na nchi, akastarehe siku ya saba akapumzika. 16Kwaajili ya hayo wana wa Israeli wataishika sabato katika vizazi vyao vyoyte, ni agano la milele.
                  Sabato ni ishara kati ya waumini wa Mungu na Mungu iashiriayo kwamba wanamtii na kushika sheria yake.Utunzaji wa sabato ni njia aliyoiweka Mungu ili kutunza maarifa kumhusu Yeye na kutofautisha waumini wanaomtii na wale wavunjaji wa sheria yake. Shetani atafanya kila mbinu kuhakikisha kwamba mafundisho ya Imani iliyokabidhiwa kwa watakatifu hapo mwanzo isilete matokeo kwa watu wa kizazi hiki.              
                  Mungu asingeweza kusema kuwa ni agano lake la milele halafu aje kubadilisha, sabato itaendelea kuwepo milele zote hata katika Mbingu mpya na nchi mpya soma Isaya 66:22,23.
                  Msomaji yeyote wa Biblia sehemu ya agano jipya, kuanzia mathayo 12:1-13, akifuatilia kila kisemwacho kuhusu sabato na msimamo ambao Yesu na Mitume waliuchukua kuhusu sabato, hatashindwa kutambua kwamba Kanisa la kipindi cha agano jipya lilitunza Sabato kutokana na mfano wa mafundisho ya Yesu mtunzaji wa sabato. “Bwana wa Sabato”  alifundisha sehemu yake halisi na tabia ya sabato katika ufalme wake.

IBADA YA JUMAPILI ILIANZA LINI?
     
                  Kabla ya yote ikumbukwe kwamba Biblia huitaja siku ya saba (Sabato ) kama siku ya Bwana. Kutoka 20:10. “lakini siku ya saba ni Sabato ya Bwana...”, Marko 2:28. Basi Mwana wa Adam ndiye Bwana wa Sabato.Isaya 58:13...ukiita sabato siku ya furaha, na siku takatifu ya BWANA yenye heshima... Baada ya Kostantino kuanzisha Ibada ya jumapili aliita siku hiyo Siku ya Bwana jambo ambalo halina ukweli wa kimaandiko, wote waiitao jumapili siku ya Bwana huo ni uongo wa shetani kuwapofusha wasijue udanganyifu wa sabato bandia aliyoanzisha. Hivyo hata vitabu vya historia huiita sjumapili siku ya Bwana kwa mtazamo huo kama ifuatavyo.

VITABU VISIVYO VYA KISABATO HUELEZEAJE?
                  Kitabu cha (International Standard Bible Encyclopedia, Vol 3, pg 158, na Vol 4 ukurasa 251,252) kimnaelezea mabo yuafuatayo:-
                             
                  “Katika Mwaka 321 A.D Costantino, ambaye pia alikuwa na muumini wa mungu-jua, aliifanya siku ya kwanza kuwa siku ya kawaida kwa jamii kupumzika, akisema kwamba, Majaji, watu wa mijini, na wachongaji wapumzike katika siku hii ya mungu jua,lakini aliwaruhusu wakulima kuhudhuria mashambani hali ya hewa ikiruhusu.Sheria hii kwa asili ilisababisha uwepo wa Ibada ya Kikristo.”

Mwaka 363 A.D.Baraza la Laodikea(Council of Laodecia)
                  Baraza hili lilikataza kupumzika katika siku ya saba (Sabato) na kuagiza watu wapumzike katika siku ya Bwana  kama ijulikanavyo kuwa siku mbadala ya Ibada.

Mwaka 451 Baraza la Karthage(Council of Carthage)
                  Baraza hili lilikaataza watu wasihudhurie katika michezo siku ya  Bwana (jumapili.)

Karne ya 16. Baraza la Oreansi (Council of Orleans) 
                  Baraza hili liliongeza sheria ya kukataza watu wasifanye kazi siku ya Bwana.(jumapili).

                  Pia kitabu cha Roman Katoliki kiitwacho “Historia ya Kanisa Vipindi Vyake saba, kilichoandikwa na F.Potmani. Ukurasa 24, kinaelezea yafuatayo;
                  Mwaka 306,  Kostantino alitangazwa Kaisari wa Magharibi, ilipofika mwaka 312 alimshinda mpinzani wake karibu na Roma. Mwaka 313, Kaisari Kostantino hakukawia kutangaza uhuru wa kanisa kwa “Tangazo la Milano”.Basi Wakristu walipata uhuru uleule wa dini kama wapagani.Walirudishiwa makanisa na mali waliyokuwa wamenyimwa wakati wa udhalimu.Kaisari alitangaza pia jumapili iadhimishwe kama “Siku ya Bwana”, na watu wakumbuke ufufuko wa Kristu wala wasifanye kazi.

                  Katika maelezo hayo yote  ni wazi kwamba kuanzishwa kwa Ibada ya jumapili, kusudi lake na hata muanzilishi wake havitokani na Biblia bali ni sababu za kibinadam. Kostantino alikuwa mpagani muabudu jua, na alipokuwa kaisari aliongoka kiuongo alitaka kupata waumini wa kipagani na kikristo . Kwa hitaji lake aliona njia pekee ya kuwavuta ni kuchanganya ukristo na upagani.
                  Mchanganyiko huu ulikamilika pale alipoanzisha ibada katika siku ya wapagani ya kuabudu mungu jua (Sun day-sunday/siku ya jua), kwa kuagiza watu wafanye pumziko la sabato aliyoihamisha kinyume na maagizo ya Mungu, kwa kufanya hivyo aliwapata Wakristo na wapagani na kuanzisha Romani Katoliki . Wkristo wasalio Jumapili hufuata amri yakanisa la Roman Catholic kama tutakavyoona.Sababu kwamba Wakristo wafanye Ibada kukumbuka ufufuo wa Yesu si ya kibiblia .Hata yesu mwenyewe hakusema wakristo wafanye ibada siku ya kwanza ya juma wakikumbuka ufufuo wake.
                  Ilipofika mwaka 1234 A.D . Papa glegory IX aliidhinisha rasmi mapumziko ya siku ya jumapili.
Biblia ilitabiri kuja kwa Uvunjwaji wa sabato
                  2 Wathesolanike 2:3,4. Mtu awaye yote asiwadanganye kwa njia yoyote; maana haiji, usipokuja kwanza ule ukengeufu,  akafunuliwa yule mtu wa kuasi, mwana wa uharibifu. 4 yule mpinzani ajiinuaye juu ya kile kiitwacho Mungu...
                  Japokuwa fungu hili linamaana nyingine kubwa ila kwa sehemu linazungumzia kitendo cha waanzilishi wa kanisa la Roman catholic walivyobadili sheria ya mungu toka sabato hadi jumapili, hapa walivunja amri ya 4 katika amri 10 za Kutoka 20:8->.Danieli 7:10 Inaitaja dola ya rumi kama pembe iliyoinuka na kunena maneno makuu (Kufuru) neno ambalo pamoja na maana yake kubwa ni kuchukua cheo cha mungu kwa kubadili alichoagiza (Utunzaji wa sabato) na kuweka agizo la kibinadam. (ibada ya Jumapili).

Wakristo wote wasaliojumapili hufuata amri ya Roma si ya Mungu
                              Hebu tuone kauli za baadhi ya maandishi ya Roman Catholic kuhusu wakristo watunzao jumapili:-
1)      Nithibitishie katika bibliapekee kwamba napaswa kuadhimisha jumapili kama siku takatifu.Hakuna sheria kama hiyo katika Biblia.Ni sheria ya kanisa takatifu la Romani Katoliki pekee. Biblia inasema 'Ikumbuke siku ya sabato uitakase.' Kanisa Katoliki linasema, Hapana. Kwa mamlaka yangu tukufu naiondoa sabato na kukuagiza wewe utunze siku ya kwanza ya juma. Na kumbe, Ulimwengu wote uliostaarabika unasujudu kwa kicho ukitii amri ya Kanisa Takatifu Katoliki. - Thomas Enright, CSRR , President, Redemptorist college (Roman Catholic) , Kansas City, MO.,February 18, 1884.
2)      Utunzaji wa jumapili kwa Waprotestanti ni gharama wailipayo, badala ya wao wenyewe, kwa mamlaka ya kanisa la Romani Katoliki. - Monsignor Louis Segur , Plain talk About the Protestantism of today (1868),p.213.
3)      Kama Waprotestanti wangefuata Biblia, wangepaswa kumuabudu Mungu katika siku ya Sabato (Jumamosi). Kwa kutunza jumapili wanafuata sheria ya Kanisa la Romani Katoliki.-Albert smith, Chancellor of the Archdiocese of Baltimore, replying for Cardinal in a letter of february 10, 1920.
4)      Waprotestanti...wanakubali Jumapili kuliko jumamosi kama siku ya ibada ya jumuiya baada ya Kanisa la Romani Katoliki kufanya mabadiliko...lakini akili za Waprotestanti hazionyeshi kutambua  kwamba...kwa kuitunza jumapili, wanakubali mamlaka ya mzungumzaji mkuu wa kanisa, Papa.-Our sunday Visitor, February 5, 1950.

                        Jumapili ni Chapa/Alama ya Romani Katoliki Duniani.                             
1)      Kwa kweli  Kanisa la Romani Katoliki  linasema kwamba badiliko (Kutoka Jumamosi hadi Jumapili) ni kazi yake.Na kitendo hicho ni CHAPA ya mamlaka yake ya kanisa na mamlaka katika mabo ya kidini.- C.F.Thomas, Chancellor of Cardinal Gibbons.
Onyo la Biblia
                  Ufunuo 14:9,10...Mtu awaye yote akimsujudu huyo mnyama ( hapa anamaanisha Romani Katoliki) na sanam yake (jumapili ni sanam ya sabato iliyosimamishwa na Romani), na kuipokea chapa ,(Kuabudu jumapioli badala ya sabato) katika kipaji cha uso wake, au katika mkono wake. Eye naye atakunywa katika mvinyo wa ghadhabu ya Mungu uliotengenezwa pasipo kuchanganywa na maji,katika kikombe cha hasira yake;naye atateswa kwa moto na kiberitimbele ya malaikawatakatifu,na mbele za mwana wa mungu.
                  Kama Yesu mwenyewe alisema Sabato ni siku ya Bwana ni vyema kumfuata maana Yeye ndiye njia ya kweli na Uzima hakuna mtu awezae kumfuata Baba bila kupitia yeye, utajisikiaje kushika kweli zote za Biblia halafu kwa kupuuzia sabato ambayo Mungu ameamuru uitunze ukashindwa kuirithi Mbingu. Kila tufanyalo duniani hutuandaa kuwa watahiniwa wa kuirithi Mbingu, Ibada mbinguni hufanyika na itaendelea kufanyika siku ya sabato. Isaya 66:22,23.Biblia inaonyesha kuwa sabato hata sabato wanadam wote watakaoirithi Mbingu wataenda kuabudu mbele za Bwana.

MUNGU HUTAMBUA MATENGENEZO YA IBADA  SIKU ZA MWISHO NI UTUNZAJI WA SABATO.
Ufunuo 14: 6,7. Kisha nikaona malaika mwingine ,akiruka katikati ya mbingu, mwenye injili ya milele, awahubiri hao wakaao juu ya nchi, na kila taifa nakabila na  lugha na jamaa, akasema kwa sauti kuu ,Mcheni mungu, na kumtukuza , kwa maana saa ya hukumu yake imekuja. Msujudieni yeye aliyezifanya mbingu na nchi na bahari na chemchemi za maji.
 Biblia inaposema tumsujudie yeye  aliyezifanya mbingu na nchi na bahari na chemchemi za maji.. Hutupeleka katika amri ya nne (Kutoka 20:8-). Ambayo hutuonyesha tusalipo katika siku ya sabato tunaonyesha kwamba tunamtambua mungu kama Muumbaji, watu wasalio jumapili huungana na Darwin mwanasayansi apingaye uumbaji, Wanadam wote wangekuwa watunzaji wa sabato (Birthday) ya uumbaji wasingesahau kuwa tumeumbwa na mungu.
                             
                  Sabato ni muhuri chapa ya MUNGU, kwani amri ya 4, jina (maana kwa siku sita mungu…) , hutaja cheo (…Mungu aliziumba mbingu na nchi na bahari..) na Mamlaka (ya mtoaji amri (Muumbaji). Amri ya nne hutia muhuri amri kumi na wote waitunzao hupigwa muhuri ili wasipigwe muhuri wa mrumi au Romani katoliki kwa kutunza jumapili. Utunzaji wa jumapili ni kupokea chapa ya 666 (VICARIUS FELEE DEI /makamu wa Mungu- Cheo cha papa ambacho hesabu yake huleta namba ya 666.) rumi inapanga kutimiza mpango huu kwa kuwalazimisha watu wote kusali jumapili kwasababu kwa kufanya hivyo watapokea chapa ya rumi.
                  Katika barua ya VATICAN CITY, TAARIFA YA MAENDELEO INAYOLENGA MWAKA 200.ROMA 20/02/199. TAARIFA NO.207.ILIYOFANYIKA MWAKA 1951 MWEZI WAKWANZA. Inanukuu hivi “Madhehebu yote hayana budi kuwa na siku moja ya ibada na hasa Jumapili, ambayo Roman Catholic iliipitisha kwa niaba ya Mungu kwa kubadili kuwa jumapili kutoka jumamosi…Kama biblia ndio mwongozo pekee wa mkristo. Waadventista wasabato wako sahihi kuitunza jumamosi pamoja na wayahudi.

                  Umeshaona ushahidi wa biblia na vitabu vingine ambavyo havikuandikwa na wasabato vinavyoonyesha kuwa kutunza jumapili kama siku ya ibada si agizo la biblia. Napenda ufahamu kuwa tatizo litakalofanya wengi wapotee ni kuabudu katika mfumo ambao kiasilia huwatendesha watu dhambi. Kusali jumapili ni mfumo ambao huwafanya watu waendelee kuvunja amri ya nne katika kutoka 20:8-.
                  Je kunausalama kuendelea kuvunja sheria ya mungu huku ukijua , fanya matengenezo.    Mungu anatambua kuwa wewe ni muumini mwaminifu kila upatapo ufunuo wa kweli yake, waweza kusema huokolewi kwa kuvunja sheria ya  Mungu bali kwa Neema. Kumbuka Sheria Hukuonyesha kuwa umefanya dhambi na Neema ya yesu (damu yake hukupa nafasi ya kufanya marekebisho). Amri ya nne inakuonyesha kuwa umevunja sabato , ukimjia Yesu anakupa nguvu ya kuitunza sabato na namna ya kuitunza.
Warumi 6:1,2.Tuseme nini basi?tudumu katika dhambi ili neema izidi kuwa nyingi. Hasha sisi tulioifia dhambi tutaishije tena katika dhambi?

            Unachukua uamuzi gani baada ya kutambua kweli 100 za biblia kuhusu sabato ya BWANA , Je  msingi wa Imani yako unajengwa kwa kile kisemwacho na Biblia au Mapokeo (Romani Katoliki). Kama Kweli wataka imani yuako ijengwe katika kweli (Mwamba na sio mchanga) Ifuate Ibada inayoonyeshwa wazi na Biblia , IBADA YA SIKU YA SABATO, BWANA AKUBARIKI UFANYAPO MAAMUZI KWAAJILI YA UMILELE WAKO.




            Rejea.

            Bill Hughes, The Secret Terrorists
           
F.Potmann.(1999).Historia ya Kanisa Vipindi Vyake    Saba.Tanganyika Mission Press         Kipalapala

Mark Finley, (2005).The Next Super Power.Review and Herald publishing association

A.H.Lewis D.,A Critical History of the Sabath and The Sunday in the Christian Church

Ellen G White.The Great Controversy.

Ellen g White. Patriachs and Prophets.

Ellen g White .Testimornies for the church Vol


  Somo hili limeandaliwa na , Petro Tumaini.
Sim.+255712761605